ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, August 30, 2013

DIAMOND AMFANYIA SUPRISE MZEE GURUMO KWENYE UZINDUZI WA VIDEO YAKE,AMPA GARI KAMA SHUKRANI YA MCHANGO WAKE KWENYE SANAA YA MUZIKI NCHINI TZ.

Nikikutajia Jina la Muhidini Gurumo
 basi utajua namzungumzia nani.
Nguli wa muziki wa Dansi nchini Tanzania.....
Takribani wikii imepita toka kusikika
kwa habari za kweli kuhusu kustaafu
muziki kwa Mzee Gurumo,binafsi sikuwahi 


kukutana nae hadi leo hii nilipokutana nae
kwenye uzinduzi wa Video yangu.
Nilimualika mzee huyu kwa mapenzi yote,niliskia
 juzi pia akisema amekuwa akipendezwa na
style ya muziki wangu na kucheza pia hayo ni moja wapo ya mambo pia
yaliyonivutia kutaka kumuona mzee huyu.
Nilipitia kwenye mitandao mingi uku ikiandikwa
kusemekana kutokana na kalui ya mzee
Gurumo ameweza kuwa kwenye fani zaidi
ya miaka 50 lakini akuwahi bahatika hata kuwa na Baiskeli....

Jambo ili lilinigusana na kuniumiza moyoni,
kuona nguli kama huyu wa muziki
kunena vile na kuomba msaada,
Binafsi leo usiku nimemtunuku Gari
Mpya mzee Gurumo kwenye uzinduzi wa Video yangu.

Nimeamua kutoa kwa moyo mmoja na
 kwa mapenzi yangu yote kwa mzee wangu.
Tukio ili limetokea tarehe 29.0.2013
nimeamua kukuwekea picha kadhaa
jinsi hali ilivyojri mara tu ya kumalizika
 kwa Launching ilikuwa
suprise kwa mzee wangu Gurumo....
By Diamond.

Mzee Gurumo akionesha Ufunguo juu baada ya kukabidhiwa Gari kama
zawadi toka kwa Diamond....
Furaha iliyoje ndani ya Moyo wangu (Diamond) kupewa baraka na Mzee wangu.....
Sauti yake tu.....Iliwafanya wageni wote kuimba nae muda huu....
Safari kuelekea Nje ya ukumbi kwa makabidhiano.....
Pembeni ya Diamond (kulia) ndio Gari alilomchukulia Mzee Gurumo.....

Habari zote zisome kwa kina zaidi kupitia: http://www.thisisdiamond.com/

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.