ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, August 27, 2013

BOTI YAZAMA ZIWA VICTORIA WATANO WAHOFIWA KUFA MAJI.

Watu watano kati ya nane waliokuwa wakisafiri na boti kutoka kijiji cha BUKUMBO wilayani Sengerema wanahofiwa kufa maji ndani ya ziwa Victoria.

Boti hilo lililokuwa limebeba abiria, mizigo ya shehena ya matenga ya nyanya limepinduka na kuzama ndani ya ziwa Victoria majira ya saa 9:00 usiku baada ya kupigwa na dhoruba iliyoambatana na upepo mkali. 

Taarifa iliyotolewa na Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Christopher Fuime kwa vyombo vya habari imesema kuwa watu watatu walifanikiwa kuokolewa na wavuvi wa dagaa ile hali watu wengine watano hawajulikani walipo.

Juhudi zaidi za kuwatafuta zingali zikiendelea na Kaimu Kamanda Fuime amewataka wananchi walio kando kando ya ziwa Victoria kutoataarifa iwapo wataona miili ya watu hao ikiwa imeibuka juu ya maji.

TAARIFA ZAIDI TUTAENDELEA KUWAPATIA KADRI ZITAKAVYO  TUFIKIA.
By Albert G. Sengo
Mwanza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.