ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 6, 2013

YANGA NA KCC YA UGANDA KUONYESHANA UNDAVA LEO JUMAMOSI UWANJA WA CCM KIRUMBA

Mabingwa wa soka wa Tanzania bara Dar es salaam Young African tayari wamekwishaingia jijini Mwanza na leo wanataraji kushuka dimba la CCM Kirumba kuvaana na KCC ya Uganda katika mechi ya kirafiki ya kimataifa. 

Sambamba na Yanga timu ya KCC ambao ni mabingwa wa ligi ya nchini Uganda nao tayari wamekwisha wasili salama mkoani hapa ambapo usiku wa kuamkia leo waliandaliwa chakula cha pamoja na waandaaji wa mpambano huo National Wide, iliyofanyika kwenye kiunga cha burudani Villa Park Mwanza.  
Sanjari na mchezo huo ambao unaonekana utakuwa na ushindani wa hali ya juu kwa wenyeji Yanga kutaka kuwakosha mashabiki wao vilevile KCC kutaka kudhihirisha kuwa wao ndiyo mabingwa wa Uganda taarifa toka ungozi wa timu zote zinasema kuwa timu hizo zitatumia mchezo huo kuonyesha zawadi na vikombe walivyotwaa kwenye ligi zao msimu uliomalizika.


Wakipiga stori za hapa na pale Villa Park Mwanza.


Benchi la Ufundi.


Ni mazungumzo zaidi.


Yanga.


Baadhi ya wachezaji wa KCC.


Eneo la tukio.


Chating huku wakila muziki.


Ufundi.



Akizungumza na blogu hii Mwenyekiti wa Taasisi ya Michezo ya National Wide Bw. John Kadutu, amesema kuwa mara baada ya mchezo wa leo dimba la CCM Kirumba mabingwa hao watarudiana tena tarehe 7/07/2013 kutoa zawadi ya  sikukuu ya Sabasaba kwa wakazi wa Shinyanga.

Amevitaja viingilio katika michezo hiyo kuwa ni shilingi 3,000/= mzunguko na shilingi 10,000/= jukwaa kuu.

Ratiba zaidi inaonyesha kuwa ziara hiyo ya mabingwa itahitimishwa mkoani Tabora kwa Yanga Africans kumenyana na Mtibwa Sugar. 

Yanga kwa mara ya mwisho walitimba mkoani Tabora enzi za wawakilishi  wa ligi kuu soka Tanzania bara, timu iliyoacha historia kwa kutandaza soka safi Mirambo ya Tabora.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.