ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, July 18, 2013

WADHAMINI TBL WASHIRIKI CHAKULA CHA PAMOJA NA TAIFA STARS USIKU HUU HOTEL LAKAIRO MWANZA

"Maneno ya mashabiki huwa matamu sana hasa pale ushindi unapoonekana..Leo umecheza vizuri basi kesho itakuwa neema kwako kama uko peponi kesho umepoteza mchezo watakuona hufai kabisa wala hustahili kuitwa timu ya taifa" "Hao ni wapenzi wa mpira lakini sisi ambao tunakaa na mpira tunasema kwamba matokeo ya uwanjani hayatuvunji  moyo hata siku moja bali yanatujenga kupata nafasi ya kujua matukio mengi zaidi"

" Wanasema kuwa tumejikita zaidi katika majukumu ya Uchaguzi tukaisahau timu, hilo siyo kweli Stars inamipango na ina watu na kila mmoja analijua jukumu lake, kwa mwaka mzima hatuwezi kufanya jambo moja tu! ile hali tuna ratiba na tunamgawanyo wa madaraka"

"Namshukuru Mwalimu aliomba timu ije Mwanza kupitia takwimu zake za kisaikolojia na kijiografia, hivyo tunaamini kuwa tunakila sababu ya kufanya vizuri hiyo siku ya tarehe 27 mjini Kampala"


Benchi la ufundi likisikiliza kwa makini mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea ndani ya hafla iliyoandaliwa na TBL katika Hotel Lakairo jijini Mwanza. 


Meza waliyoketi magolikipa wa timu ya Taifa.


Pamoja tutashinda.


Kutoka kushoto ni Kocha mkuu wa timu ya Taifa Kim Poulsen akitfuatiwa na Meneja kuuu wa timu ya Taifa Leopard Tasso, Kocha wa makipa Juma Pondamali na Kocha msaidizi Slyvester Mash wakijadiliana masuala makuu ya hapa na pale kwenye hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na TBL Mkoa wa Mwanza katika Hotel Lakairo usiku huu. 


Canavaro akiwa na Kiemba.


Dole.....!!!


Peace....!


Kwa upande wake kocha mkuu wa Taifa Stars Kim Poulsen, anasema kuwa anaifuatilia kwa karibu sana hali ya hewa ya nchini Uganda na kila kinachojiri mjini Kampala, kuanzia mazingira watakayofikia, hali ya ya hewa ambayo kila siku najaribu kupata data za vipimo vya majiji yote mawili Kampala na Mwanza walipopiga kambi, vipimo vikionyesha kuwa na hali joto sawa, hivyo hawatokuwa wageni pindi watakapotua Uganda.


Hapa palikuwa patamu sana wakati kila mchezaji kuitwa na kusalimiana na Wadhamini, mwendesha tukio alikuwa Juma Kaseja, eti naye alitaka wachezaji wenzake wamsalimu, inshu ilikuwa ni maneno ya chini chini yaliyokuwa yakizungumzwa na wachezaji wenzake aliokuwa akisalimiana nao... majina ya aka duh ni viroja (Siunaona wadhamini  wakicheka...) 


Wakisalimiana ni Amri Kiemba na Meneja wa TBL Mkoa wa Shinyanga Mr. Robert, huku Kaseja akichombeza kwa utani jina la Kiemba kwa style ya Kocha Kim Poulsen awaitavyo wakati wa kutangaza timu ya Taifa!!


Kelvin Yondani na Juma Kaseja.


Salaaaam...


Picha ya pamoja Stars na Wadhamini wao TBL.


Picha ya pamoja benchi la ufundi na Wadhamini TBL.


Ni flash kwa G. Sengo Blog.
Mungu ibariki Tanzania
Mungu ibariki Taifa Stars

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.