ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, July 12, 2013

MWILI WA HUMPHREY SIMON (MASWI) WAAGWA JIJINI MWANZA: KUZIKWA KESHO MUSOMA

Jeneza lililoubeba mwili wa marehemu Humphrey Simon likiwa limewasili Nyumbani kwake Nyakato Sokoni kwaajili ya heshima za mwisho na kukesha kisha kesho asubuhi safari kuelekea Musoma kwa mazishi.

Wakati ukipokelewa nyumbani kwake toka hospitali ya rufaa Bugando.

Mc Bonke akiongoza shughuli na taratibu nzima msibani.

Mjomba wa marehemu Archtc. Tega akitoa taratibu za jinsi familia ilivyopanga juu ya safari ya mwisho ya kuuhifadhi mwili wa marehemu.

Ilikuwa ni majonzi wakati mke wa marehemu Humphrey Simon, Bi Neema akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa marehemu mumewe ambaye walifunga ndoa mwaka juzi tu (2011)

Ndugu jamaa na marafiki wakitoa heshima zao za mwisho.

Hatua za kuuaga mwili wa marehemu zikiendelea kwa upande wa akinamama.

Bibi wa marehemu alipata wakati mgumu.

Marafiki wa marehemu wakiuaga mwili wa marehemu mbele ni Mr.Dinno akifuatiwa na Mr. Chacha.

Mjomba wa marehemu akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa marehemu mwanaye.

Huzuni kwa marafiki: Dada Less akiuaga mwili wa marehemu.

Ibada ya kuuaga mwili wa marehemu ilifanyika jioni ya leo kisha mwili utalala hapa nyumbani kwa marehemu ambapo kesho jumamosi asubuhi safari kuelekea Musoma itafanyika kwajili ya mazishi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.