ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 15, 2013

PPF YAKUTANA NA WAAJIRI WA MIGODI KANDA YA ZIWA KUTOA ELIMU JUU YA MIFUKO YA JAMII

Meneja wa PPF kanda ya ziwa Meshark Bandawe akizungumza na waajili wa makampuni mbalimbali ya migodi kanda ya ziwa kuhusu shughuli mbalimbali za uendeshaji wa mfuko huo wa jamii na sheria zake.

Waajili mbalimbali kutoka makampuni ya Geita Mine, North Mara, African Barrick Tanzania, Tulawaka, Caspian Tanzania Limited, Majour Drill na Twigg Gold Mine, wamehudhuria semina jii kwa mwitikio wa asilimia 100. 

Waajili wa migodini pamoja na waandishi wa habari wakinakili point zilizokuwa zikiwasilishwa na meneja wa kanda.

Waajili ndiyo nguzo kubwa ya kuwasilisha ujumbe hivyo PPF imeona ni vyema kukutana nao hapa na kutoa seminakuwaelimisha manufaa ya kushiriki katika kuwawekea akiba ya baadaye wafanyakazi wao.

Waajili hawa watakuwa mabalozi wa PPF kuhakikisha ujumbe wa mifuko ya jamii na taratibu zake unafika kwa wafanyakazi wote waajiliwa ambao ni wanachama.

Ni safu ya wafanyakazi wa PPF tawi la Mwanza walio na dhamana ya utoaji elimu, Kutoka kushoto ni Happyness Manyenye, Zaida Mahava, Jackson Mashiku, Grace Balele, Stela Mashiku na Zaida Mahava, wakiwa wamejipanga wakisikiliza kilichokuwa kinajiri.

PPF imekuwa na utaratibu wa kukutana na waajiri kuhakikisha kwamba pamoja  na kuwa na kazi za msingi za kuandikisha wanachama kutoka sehemu zote za ajira, kukusanya michango yao, kuwekeza pamoja na kulipa mafao lakini pia kuhakikisha inatimiza wajibu wake wa kutoa elimu kwa wanachama wake kufahamu kwa undani wanachokichangia na nini wanategemea kupata kutoka kwenye mfuko wa hifadhi ya jamii.

Kumekuwa na changamoto kubwa kwa baadhi ya waajili nchini kuzembea kuwasilisha michango kwa wakati.

Katika semina hii moja kati ya mada zilizojadiliwa ni pamoja na taratibu za kisheria na adhabu zipi zitachukuliwa kwa ajili ambao hawatatekeleza majukumu yaokwa mujibu wa sheria.

Jumla ya mafao 7 yanatolewa na PPF ikiwa ni pamoja na Mafao ya uzeeni, Kinua mgongo, Mafao ya ulemavu na ugonjwa, Mafao ya kifo, Mafao ya wategemezi na Mafao ya elimu ambapo PPF kwa sasa inasomesha zaidi ya watoto 1000 nchi nzima ambao walezi wao ambao walikuwa wanachama wa PPF walitangulia mbele za haki hivyo imebeba jukumu la kuwasomesha kwa mujibu wa fao la wanachama waliofariki mpaka wafike kidato cha nne.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.