ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, May 24, 2013

NCHI SIO YA RAIS NI YETU SOTE TUMSAIDIE KIFIKRA


Wanamabadiliko.
Ndugu zangu kutokana na hali ya nchi yetu kukumbwa na changamoto mfululizo na lawama zote tunambebesha Rais kusema ni nchi yake peke yake tunakosea, tujitahidi kumpa mawazo nini kifanyike wapi parekebishwe ili kujenga nchi. Tukikaa kimya eti tunasubiri sijui chama tawala king`atuliwe madarakani hivi navyo tunakosea.

Nchi ni yetu na sio ya mtu mmoja,  Rais tulimchagua wenyewe kwa mapenzi yetu, cha msingi katika hiki kipindi chake kilichobaki madarakani anahitaji msaada wa mawazo na sio lawama kama tunavyokesha kukilaumu chama tawala na uongozi wake.Kulaumu sio solution, solution ni kusaidiana wapi kakwama apate msaada na pindi tunapo fanikisha tumefanikiwa sote.

Lawama zisizokwisha kila kukicha hazisaidii ndugu zangu,Kikwete sio malaika wa kusema kila kitu anaweza na yeye ni binaadamu hajakamilika.

Nina imani kubwa hata hatakayekuja hataweza kuwaridhisha wanzatania wote mnavyotaka,cha msingi tuwe na tabia ya kutoa maoni nini kifanyike kwa viongozi wetu ili kujenga nchi na sio lawama ndugu zangu.

Nina Imani kubwa sana na watu wa jukwaa hili kwamba  wana fikra nzuri za kumshauri kiongozi yoyote yule ili kuleta maendeleo.Hata sisi kwenye jukwaa letu huwa tuna taratibu zetu tukiona kwamba fulani anakosea huwa tunajaribu kumrejesha kwenye njia iliyo sahihi na sio kumtupia lawama Moderator.

Nawaomba ndugu zangu kwa heshima zote na upendo wangu kwenu tujaribu kumsaidia huyu kiongozi wetu maana hata na yeye sidhani kama ana furaha na amani ndani ya nafsi yake kwa lawama za kila mtu.

Tujenge misingi ya kusaidiana kimawazo..najua wengi mmechoshwa na CCM na baadhi ya viongozi wao, sasa basi tujipange tusije kupoteza hata hiki tulichonacho wakati tukisubiri chama hicho kingine ambacho kitashika hatamu 2015, ila ninatoa angalizo, tusije tukaacha kuwasaidia hata hao watakaokuja kutuongoza kwa fikra kuwa wao tu ndiyo kila kitu.

Yangu ni hayo tu, nawatakia kila la heri.
                                                     Maganga One

Tupe maoni yako

1 comments:

  1. UJUMBE HUU UNGEMTUMIA NA NDUGU YETU AMBAYE TANGU NIMTAMBUE SIJAMSIKIA AKISIFIA CCM INGAWA KUNA MENGI TU CCM IMEYAFANYA NA SI MWINGINE NI SLAA

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.