ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, May 17, 2013

MICHUANO YA SAFARI LAGER HIGHER LEANING NATIONAL POOL CHAMPIONSHIP KUANZA RASMI KESHO JIJINI MWANZA

Meneja wa Matukio wa bia ya Safari mkoa wa Mwanza Bernad Nahum (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari ambapo pia alitumia fursa hiyo kukabidhi jezi kwa washiriki, kulia ni captein wa timu ya SAUT Jimmy Nikitas,  inayotetea taji la ubingwa wa pool kwa vyuo nchini.


Mashindano ya Safari Lager Higher Leaning Pool kwa mkoa wa Mwanza yanataraji kuanza kutimua vumbi kuanzia kesho katika ukumbi wa Villa Park jijini Humo.

Kwa mujibu wa Meneja wa Matukio wa bia ya Safari mkoa wa Mwanza Bernad Nahum amesema kuwa Mashindano ya Higher Leaning Pool kwa mkoa wa mwanza yatashirikisha vyuo vinne ambavyo ni CBE Mwanza, Chuo cha Bugando, SAUT na TIA ambapo vyuo hivyo vitashindana kupata mwakilishi  mmoja atakaye shiriki mashindano ya Pool Taifa kwa mikoa mingine hapa nchini kama Mbeya, Dar es salaam, Morogoro, Dodoma, Kilimanjaro na Arusha  
Kushoto aliyesimama ni Afisa habari wa michuano ya Safari Lager Higher Leaning Pool Machel akitoa ufafanuzi juu ya mafanikio yaliyopatikana hadi sasa kwa vyuo shiriki kupitia michuano hiyo.

Zawadi kwa washindi Timu za Pool 
Mshindi wa kwanza mkoa ni shilingi laki 5
Mshindi wa pili shilingi laki 3
Mshindi wa tatu shilingi laki 2
Na mshindi wa nne shilingi laki 1

Washindi Single wanaume 
Mshindi wa kwanza shilingi laki 1.5
Mshindi wa pili shilingi laki 1

Washindi Single wanaume
Mshindi wa kwanza shilingi laki 1
Mshindi wa pili shilingi elfu 50. 



Timu captein wa timu bingwa Chuo cha SAUT Jimmy Nikitas (kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuelezea jinsi timu yake ilivyojiandaa kwa michuano ya Safari Lager Higher Leaning Pool 2013.


Meneja wa Matukio wa bia ya Safari mkoa wa Mwanza Bernad Nahum (kushoto) akimkabidhi jezi timu captein wa Chuo cha SAUT Jimmy Nikitas kwaajili ya michuano hiyo inayotaraji kuanza rasmi kesho Villa Park Resort Mwanza.


Meneja wa Matukio wa bia ya Safari mkoa wa Mwanza Bernad Nahum (kushoto) akimkabidhi jezi timu captein wa Chuo cha Bugando Bernad Okamo, kwaajili ya michuano hiyo inayotaraji kuanza kutimua vumbi rasmi kesho katika Viunga vya burudani vya Villa Park Resort Mwanza.


Meneja wa Matukio wa bia ya Safari mkoa wa Mwanza Bernad Nahum (kushoto) akimkabidhi jezi timu captein wa Chuo cha CBE Mwanza George Izengo, kwaajili ya michuano ya Safari Lager Higher Leaning Pool inayotaraji kuanza rasmi kesho Villa Park Resort Mwanza.


Meneja wa Matukio wa bia ya Safari mkoa wa Mwanza Bernad Nahum (kushoto) akimkabidhi jezi timu captein wa Chuo cha TIA Beatrice Benignus, kwaajili ya michuano ya Safari Lager Higher Leaning Pool inayotaraji kuanza rasmi kesho viunga vya burudani Villa Park Resort Mwanza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.