ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, April 17, 2013

LIGI KUU SOKA TANZANIA BARA MGAMBO YAIDINDIA YANGA, KAGERA YAIPIGA MSUMARI TOTO AFRICANS

Mgambo yatia Nuksi Ubingwa
Mgambo Fc V/s Yanga 


Ligi kuu Tanzania bara iliendelea leo, huku vita kubwa ikiwa kwenye uwanja wa Mkwakwani jijjini Tanga ilipoikutanisha Yanga na Mgambo Fc.

Wakicheza kwa presha kubwa kuhitaji pointi muhimu sana ili kukaribia kutangaza Ubingwa mapema, Yanga walijikuta wakipata sare ya goli moja kwa moja.

Mgambo ndio walikua wa kwanza kupata bao kabla ya Msuva kusawazisha dakika ya 87 na kuisaidia timu yake kuepuka kipigo kabisa, kwa matokeo hayo sasa Yanga wanahitaji pointi nne tu ili kutangaza ubingwa kwani watafikia pointi 57 ambazo wapinzani wao wakubwa msimu huu Azam Fc hawawezi kizifikia.

Matokeo ya mechi nyingine Mtibwa waliifunga JKT Oljoro goli moja bila majibu pia Kagera Sugar imewashindilia bila huruma msumari mmoja bila majibu majirani zao Toto Afrikans inayopigana kutoshuka daraja.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.