ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 8, 2013

GEITA KUSHUHUDIA MKALI NANI KATI YA MCHELE MCHELE NA BHUDAGALA.

Tarehe 23/03/2013 wasanii wanaotamba hivi sasa katika mahadhi ya muziki asili toka kabila la Wasukuma, Mchele Mchele pamoja na Bhudagala watapanda jukwaa moja mkoani Geita katika uwanja wa Katoro  kuonyeshana ubabe kwa mashabiki kwamba nani ni mkali katika suala la burudani.

Kipindi kirefu sasa wakali hao nyimbo zao zimekuwa zikisikika kwenye kumbi za starehe kanda ya ziwa, huku kanda zao na cd zikinunulika kama njugu hasa kwa wapenzi wa muziki asili ambao wamekuwa wakiburudishwa na vionjo asili pamoja na ujumbe unaopatikana kiasi cha wengi kutamani siku itokee nao kuwekwa kwenye mizani moja kupimwa yupi ni bora zaidi ya mwenzake. 

Kwa mujibu wa Bwana Livinus Madaraka ambaye ni mkurugenzi wa Tivol Studio Mwanza , waandaaji wa mpambano huo amesema kuwa kampuni yake imeamua kuandaa mpambano huo ili kumaliza utata kwa mashabiki pamoja na wakali hao kutambiana kwenye majukwaa tofauti kila mmoja akinasibu kuwa ni mkali zaidi ya mwenzake, hivyo anaamini kupitia mchakato huo aliyebora zaidi ya mwenzake atajulikana.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.