ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, February 2, 2013

"AKINA MAMA MWANZA MKO TAYARIiiiiiii.....!!!!?"


Mkurugenzi wa Mikaela Gateway Agency, Idda Ngaiza (kulia) akiwa na moja kati ya wadau wake kwenye matayarisho kuelekea siku ya kongamano kubwa la wanawake lijulikanalo kama Women Dialogue Front litakalo kwenda kufanyika Mwanza kwenye ukumbi wa Hotel JB Belmonte iliyoko jengo la NSSF siku ya tukio ni tarehe 10/3/2013.

Mkurugenzi wa Mikaela Gateway Agency (kushoto) akiteta na Mh. Mama Getrude Mongela ambaye anatajwa kuwa ndiye atakaye kuwa mgeni rasmi wa siku ya kongamano kubwa la wanawake yaani Women Dialogue Front litakalo fanyika Mwanza kwenye ukumbi wa Hotel JB Belmonte iliyoko jengo la NSSF siku ya tukio ni tarehe 10/3/2013.
Kwa mujibu wa mratibu wa Kongamano hilo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mikaela Gateway Agency, Idda Ngaiza amesema kuwa Mh. Vicky Kamata naye amethibitisha kuwepo kwenye kongamano hilo akiahidi pia kuikamata vyema sekta ya Burudani kwa siku hiyo hivyo amewaomba akina mama wajitokeze kwa wingi ili kufaidi mafunzo mazuri yenye manufaa kwa mstakbari wa maendeleo yao na familia zao.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.