ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, January 17, 2013

WILAYA YA MASWA NA VIVUTIO VYAKE KATIKATI YA MJI.

Sanamu ya Hayati Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere iliyoko katika kipita shoto cha katikati ya wilaya ya Maswa mkoani Simiyu kama nilivyokinasa hii leo.

Mikoa mingi hapa nchini imeshindwa kujenga sanamu ya Baba wa Taifa na kubakia kujenga sanamu za malighafi zizalishwazo mikoani humo (samaki (Mwanza), ndizi (Bukoba), tembo na Mmasai (Arusha na kadha wa kadha)) pamoja na rasilimali nyingine kisa mikoa hiyo ikiogopa kupata aibu kama ile iliyolikumba jiji la Mwanza kwa sanamu ya Baba wa Taifa katikati ya kipita shoto cha jiji hilo la miamba kushushuliwa kuwa na utofauti na taswira halisi ya JK na hatimaye sanamu hilo lililogharimu pesa nyingi kupotea kusikojulikana mpaka leo...
 Swali ni Jeh Maswa wameweza?

Muonekano full wa Sanamu hiyo..

Kipitashoto kikuu wilayani Maswa.

Naam inakukumbusha historia...


Waijua TANU weye?

Na bustani yake...

Tupe maoni yako

1 comments:

  1. Nchi hii ina wahunzi wazuri wenye uwezo, tatizo tenda hazitolewi kwa watu wanaostahili, kila kitu uchochoroni.

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.