ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, December 19, 2012

KWAHERI MPENDWA MAMA YETU MAGDALENA

Mwili wa mpendwa marehemu mama Magdalena Bitindi Machumu aliyefariki mnamo tarehe 15 December 2012 umeagwa leo jijini Mwanza na kisha baadaye kusafirishwa kuelekea kijiji cha Lisoli Majita mkoani Mara kwaajili ya mazishi yanayotarajiwa kufanyika kesho siku ya alhamisi.

Kwa mujibu wa historia fupi ya marehemu iliyosomwa katika kanisa la Wasabato Mabatini jijini Mwanza, Marehemu mama Magdalena Butindi Machumu alizaliwa mnamo tarehe 5 April 1939 kijiji cha Lisoli Bwenge mkoani Mara.
Akafunga ndoa mwaka 1953 na Bwana Alex Mkama Kusaga ambaye naye ni marehemu, wakapata watoto 3.

Ndani ya kanisa hili marehemu mama Magdalena Butindi Machumu amewahi kuwa na nyadhifa mbalimbali ikiwa ni sambamba na kuwa mmoja kati ya wanakwaya wa kwaya ya akina mama wa kanisa la Sabato mabatini.

Kwaya ya akina mama Kanisa la Wasabato Mabatini jijini Mwanza ikimba wimbo kuuaga mwili wa mpendwa wao.

Sehemu ya watoto na wajukuu wa marehemu walioshiriki ibada hiyo.
Ibada ndani ya Kanisa la Wadventista Mabatini jijini Mwanza.

Mr. Mrope kutoka Clouds fm Dar es salaam alikuwa ni mmoja kati ya waliohudhuria shughuli hii ya leo kuuaga mwili wa marehemu mama Magdalena.

Ibada ndani ya Kanisa la Wadventista Mabatini jijini Mwanza

Mwili wa marehemu ukiagwa na ndugu jamaa na marafiki walio hudhuria kwenye ibada.

Heshima za mwisho kwa marehemu zikiendelea kutolewa ndani ya kanisa la Wadventista Mabatini Mwanza.

Ndugu wa marehemu wakitoa heshima za mwisho kwa mpendwa wao.

Dada Juddy ambaye ni mmoja kati ya watoto wa marehemu akiteta jambo na ndugu zake pamoja na jamaa zake wa karibu kuhusu hatua zinazofuata kuelekea kuusitiri mavumbini mwili wa marehemu mama Magdalena Bitindi Machumu.

Nje ya kanisa taratibu za safari fupi kuelekea nyumba aliyokuwa akiishi marehemu mama Magdalena kwaajili ya kuagwa mwili na wanamtaa zikiendelea kisha baadaye kuelekea mkoani.






AGIZO LA NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI LA KUHAMISHA KIVUKO CHA MV SAMAR LALETA BALAA, WANANCHI WAKERWA WAILALAMIKIA SERIKALI, MMILIKI ASIMAMISHA HUDUMA YA USAFIRI HUO.


Mkurugenzi wa Kampuni ya Meli ya MV. SAMAR Salum Ally akizungumza na vyombo vya habari. 
 ABIRIA na wananchi wanaotumia kivuko cha MV. SAMAR wamepinga vikali agizo la Naibu Waziri wa Uchukuzi Dkt. Charles Tizebar la kuamuru kusitishwa kwa huduma ya usafiri wa kivuko hicho kinachotoa huduma kati ya Mwanza mjini na Kamanga Wilayani Sengerema hali iliyopelekea wananchi kupinga vikali hatua hiyo ya Naibu Waziri na Serikali.


Wananchi na abiria hao wamesema kwamba kauli hiyo ya Naibu Waziri Dkt.Tizebar aliyoitoa hivi karibuni wakati wa kuipokea treni ya abiria ya kutoka Jijini Dar es salaam hadi Jijini Mwanza kuwasili kwa mara ya kwanza tangu kuanza kazi Desemba 9 mwaka huu baada ya kusitisha safari zake kwa miaka mitatu kwa madai kuwa wamezuia njia ya reli iendayo bandarini huku madai hayo yakionekana kupingana na Mamlaka ya Bandari ya Mwanza Kaskazini waliodai kuwa kwa sasa hawahitaji huduma ya Treni kufika Bandari hiyo na ni miaka zaidi ya kumi Treni kupita na kufika Bandari hiyo ya Mwanza Kaskazini.

Akizungumza na vyombo vya Habari Mkurugenzi wa Kampuni ya Meli ya MV. SAMAR Salum Ally alisema kwamba agizo la kusimamisha huduma na kuhamia eneo la maegesho ya Meli za Marine Service huku kukiwa hakuna matayarisho ya barabara ya magari kuingia na kutokea,abiria na daraja la meli hiyo kuweka nanga ili kuruhusu abiria na magari kupita kirahisi kama ilivyo kwenye eneo kilipokuwa kikitolea huduma awali.

Salum amesema kwamba alipokea barua ya kwanza ya Mamlaka ya Bandari ya Kaskazini (PTA) Desemba 11 mwaka 2012 yenye kumb.MN/2/3/04 iliyosainiwa na Mkuu wa Bandari hiyo Mhandisi Josephat Mutalemwa  huu ikisomeka kwamba  ‘AGIZO LA NAIBU WAZIRI LA KUHAMISHA HUDUMA YA KIVUKO KUTOKA HAPO ULIPO NA KUELEKEA NDANI ZAIDI YA BANDARI YA KASKAZINI’ ikiwa ndani ya wiki tatu za kutekelezwa kwa agizo hilo.

Barua ya kwanza.
Ameongeza kuwa wakati akitafakali juu ya uamuzi huo wa barua hiyo na Agizo la Naibu Waziri Dkt.Tizebar,Kabla ya wiki moja kumalizika ghafla akapokea barua nyingine tena ya pili ambayo pia ikitolewa na PTA Desemba 19 mwaka huu na ikisainiwa na Kaimu Mkuu wa Bandari T.S.Akile iliyosemeka 'KUSITISHA HUDUMA YA KIVUKO KUTOKA HAPO ULIPO NA KUELEKEA ZAIDI NDANI YA BANDARI YA KASKAZINI' Mamlaka ya usimamizi wa Bandari (PTA) inakutaka kusitisha mara moja shughuli za kupakia na kushusha abiria na mizingo kuanzia sasa hivi (Leo Desemba 19 mwaka huu).

Kufatia hatua hiyo hali ilikuwa tofauti kwa wananchi na abiria na kuanza kurusha mameno na kauli kali za kupinga hatua ya PTA,Serikali na Agizo la Naibu Waziri Dkt. Huku Mkurugenzi wa SAMAR alidai kuwa ameheshimu kauli ya Waziri na agizo la barua za PTA, akidai kuwa amekuwa akiilipa PTA kiasi cha shilingi milioni 2 kwa mwezi ikiwa ni makubaliano baada ya kuomba kutumia eneo hilo na kupitia Meli zake amekuwa pia akiliingizia shirika hilo kiasi cha zaidi milioni 70 kwa mwezi kwa huduma ya Bandari ya Mwanza Kaskazini na Kusini.

Mbali na kuiingizia PTA mapato hayo, kampuni hiyo imekuwa akisaidia wanawake wajane zaidi 60 kiasi cha shilingi 600,000 kwa mwezi waliopo eneo la Kamanga huku serikali ya Kijiji hicho cha Kamanga kikiingiza kila siku kiasi cha elfu 40,000/= ikiwa ni huduma za wananchi wanaotumia vyoo katika eneo la kugota Meli ya MV. SAMAR huku wanafunzi wote wakipita bure katika kivuko hicho wakiwemo wazee wa zaidi ya miaka 70 na mama wajawazito na watoto walio chini ya miaka 8 kila siku ya huduma wa Meli hiyo.

Kivuko hicho cha MV.SAMAR.
Kivuko hicho cha MV.SAMAR kinacho beba abiria wapatao 390  kwa wakati mmoja,mizigo tani 320 kwa kila safari moja ifanyayo ambapo kwa kutwa nzima ni zaidi ya abira zaidi ya 3,500 kwa siku nzima ya safari 12 za abiria na mizigo kutoka Jijini Mwanza hadi Kamanga Wilayani Sengerema tangu kukubaliwa na Uongozi wa Mamlaka ya Bandari ya Mwanza Kaskazini Septemba 17 mwaka huu hadi Septemba 17 mwaka 2013 ikiwa ni mkataba wa majaribio wa  mwaka mmoja kabla ya kusainiwa mkataba mwingine.



Njia ya reli ndani ya eneo ambayo kimsingi kwa upande wa wamiliki wa eneo la kivuko cha MV. SAMAR ambao wao wameacha nafasi ya kutosha kwa reli hiyo kupitika zaidi ya kutumia eneo la reli kama sehemu ya barabara ikatishayo kwa ajili ya magari.

 Baadhi ya abiria walikuwa wakitakiwa kupanda kivuko husika wakirejea kwenye siti zao kufanya mgomo wa kulazimisha safari ziendelee.

Ghati ya eneo ambalo huduma inapaswa kuhama kufuatia agizo la kusimamisha huduma na kuhamia eneo la maegesho ya Meli za Marine Service

Mishemishe za biashara eneo la Kamanga ferry. 

Mh. LOWASSA AZINDUA JOSHO LA KISASA KWA MIFUGO KIJIJI CHA MFEREJI MONDULI JUU

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akisalimiana na wananchi wa Kijiji cha Monduli juu,Mkoani Arusha wakati alipokuwa akiwasili kijijini hapo kwa ajili ya shughuli ya uzinduzi wa josho la kisasa la Mifugo katika kijiji cha Mfereji Monduli juu.


Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akikaribishwa kwenye kijiji cha Mfereji Monduli juu,wakati alipokuwa akiwasili kijijini hapo kwa ajili ya shughuli ya uzinduzi wa josho la kisasa la Mifugo

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akifunua kitambaa kwenye jiwe la msingi kuashiria uzinduzi wa josho la kisasa la Mifugo,lililoko katika Kijiji cha Mfereji,Monduli Juu.

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Mfereji,Monduli Juu,mara baada ya kuzindua josho la kisasa la Mifugo.

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akikata utepe kuashiria uzinduzi wa josho la kisasa la Mifugo,lililoko katika Kijiji cha Mfereji,Monduli Juu.

Mifugo ikiingizwa kwenye Josho hilo,mara baada ya kuzinduliwa.

Wakazi wa kijiji cha Mfereji,Monduli juu wakimsikiliza Mh. Lowassa (hayupo pichani).

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Monduli juu,Mkoani Arusha wakati wa hafla ya uzinduzi wa josho la kisasa katika kijiji cha Mfereji Monduli juu. ambapo ametoa wito kwa wakulima na wafugaji nchini kuacha uhasama wa kugombea ardhi.


Amesema kuwa kila mtu ana haki yake hivyo ni muhimu kwa jamii hizo kuheshimiana na kukaa pamoja kutatua tatizo la ardhi kwa ajili ya malisho ya mifugo pamoja na kilimo.Kumekuwa na matokeo mengi sehemu mbalimbali ya kupigana kuwania ardhi kati ya wakulima na wafugaji, miongoni mwa maeneo hayo ikiwa ni mkoani arusha.

Amewaambia watu wa jamii ya kimasai ambao ni wafugaji kuingia katika ufugaji wa kisasa utakaowazuia kuhama hama kutafuta malisho ya mifugo yao.''Jamani watanzania wenzetu hawatakubali mtakapovamia maeneo yao bila ya ruhusa ni lazima tuondokane na tabia hii'' alisema.

PRIME TIME PROMOTION YATOA MILIONI 105 KUFANIKISHA SHAMRA SHAMRA ZA MKUTANO MKUU WA YANGA.

Pichani kulia ni Mkurugenzi wa Prime Time Promotions Ltd,Joseph Kusaga akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi millioni 105 kwa uongozi wa timu ya Yanga kwa ajili ya maandalizi ya mkutano wao mkuu pamoja na mechi ya kirafiki ya kimataifa katika kukamilisha shamrashamra za kusindikiza mkutano huo wa kwanza wa uwazi wa kihistoria kwa Club ya Yanga.
Mkurugenzi wa Prime Time Promotions Ltd,Joseph Kusaga na Makamu Mwenyekiti wa Club ya Yanga,Clement Sanga wakikabidhiana mikataba yao ya makubaliano ya kikazi.

Mkurugenzi wa Prime Time Promotions Ltd,Joseph Kusaga akitiliana saini ya makubaliano na club ya Yanga kuhusiana na makubaliano ya timu ya Yanga  kusaini mkataba wa maelewano na kampuni ya Primetime Promotions Ltd,ambapo Prime Time Promotions imekubali majukumu ya matayarisho yote ya mkutano wa wanachama wote wa Yanga uliopangwa kufanyika Januari 19 2013.
Mkurugenzi wa Prime Time Promotions Ltd,Joseph Kusaga akifurahia jambo na baadhi ya Wanahabari mara baada ya kutiliana saini mikataba yao ya kikazi na Club ya Yanga,uliofanyika mapema leo kwenye makao makuu ya ofisi za club hiyo,Jangwani jijiini Dar

Mkurugenzi wa Prime Time Promotions Ltd,Joseph Kusaga akizungumza machache kuhusiana na makubaliano yao ya kikazi na Club ya Yanga ikiwemo sambamba na makabidhiano ya mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 105 yaliyotolewa na kampuni ya Prime Time Promotions Ltd.

Pichani kati ni Makamu Mwenyekiti wa Club ya Yanga,Clement Sanga akizungumza mapema leo kwenye makao makuu ya timu hiyo na Waandishi wa habari kuhusiana na timu ya Yanga  kusaini mkataba wa maelewano na kampuni ya Primetime Promotions Lt,ambapo Prime Time Promotions imekubali majukumu ya matayarisho yote ya mkutano wa wanachama wote wa Yanga uliopangwa kufanyika Januari 19 2013.Kushoto ni katibu mkuu wa Yanga Lawrence Mwalusako na kulia ni Mkurugenzi wa Prime Time Promotions Ltd,Joseph Kusaga.


Aidha katika mkutano huo imeelezwa kuwa matayarisho hayo yatahusisha ukumbi na viambatanisho vyote muhimu,ikiwemo Live TV coverage na matangazo mbalimbali ya kuhamasisha mafanikio ya mkutano.

Aidha katika kuongeza mapato kwa maendeleo ya club na matayarisho ya kumalizia ligi, Prime Time Promotions Ltd,imetoa milioni 105 mapato ya uhakika kwa timu ya Yanga na Prime Time Promotions  itaandaa mechi ya kirafiki ya kimataifa katika kukamilisha shamrashamra za kusindikiza mkutano huo wa kwanza wa uwazi wa kihistoria kwa Club ya Yanga. 
Habari Picha na Michuzijr Blog.

TOTO PARTY NDANI YA CINE CLUB DESEMBA 25 NA 26, 2012

Hii ni mara ya tatu kuandaa TOTO PARTY kwa ajili ya watoto wa jiji la Dar es Salaam na itafanyika Krismasi na Boxing Day ndani ya Cine Club.
Katika Tamasha hilo, watoto watapata nafasi ya kushiriki katika michezo mbalimbali kama soka la ufukweni, kuogelea, kusaka hazina (Treasure hunt) na kujipaka rangi usoni (Face painting) na mengine mengi.
Aidha watoto hao pia wataweza kufunga akaunti ya benki kwa watoto inayojulikana kama ‘Pambazuka’ kupitia benki ya Ecobank.
Mbali na watoto kucheza na kufurahi michezo mbalimbali pia wazazi wao watachuana katika mchezo wa kuvuta kamba ambapo washindi katika michezo hiyo watazawadiwa zawadi mbalimbali na viingilio ni Sh 3,000 kwa watoto na wakubwa Sh 7,000.

Tuesday, December 18, 2012

EDGAR MAPANDE ATUNUKIWA NONDO NAIBU WAZIRI NISHATI NA MADINI AHUDHURIA KUHAMASISHA ELIMU KWA VIJANA NCHINI

Edgar Mapande mara baada ya kutunukiwa pichani akiwa na Naibu Waziri wa Nishati na madini, mbunge wa Shinyanga mjini Mh. Steven Masele ambaye alikuwepo kuweka hamasa ya vijana kuthamini elimu, wengine kulia ni mwenyekiti wa serikali za mitaa eneo la Kunduchi Benedict Tibehenderwa, na kushoto ni bw. John Mbaga ambaye ni CEO wa Bayport Financial Service Ltd ambao nao walihudhulia maafali hayo.  



Edgar Mapande mara baada ya kutunukiwa katika picha ya furaha mara baada ya kutunukiwa Shahada ya Masters Of Science in Marketing kwenye maafali ya 11 ya Chuo Kikuu Cha Mzumbe Kampasi ya Dar es salaam yaliyofanyika ijumaa ya tarehe 14 Disemba 2012.

Mama mkubwa wa Edgar Mapande aitwaye Rhoda j Wasonga akimvalisha taji la maua mwanae mara baada ya kupokea Shahada ya Masters Of Science in Marketing kwenye maafali ya 11 ya Chuo Kikuu Cha Mzumbe Kampasi ya Dar es salaam yaliyofanyika ijumaa ya tarehe 14 Disemba 2012.



Mama mkubwa wa Edgar Mapande,  akimkumbatia mwanae.


Edgar Mapande akiwa na dada yake Oliver J. Ryanna (Mrs Albert Sengo), katika picha ya furaha mara baada ya kutunukiwa Shahada ya Masters Of Science in Marketing kwenye maafali ya 11 ya Chuo Kikuu Cha Mzumbe Kampasi ya Dar es salaam yaliyofanyika ijumaa ya tarehe 14 Disemba 2012.


Picha ya furaha na smile za wadau kwenye maafali ya 11 ya Chuo Kikuu Cha Mzumbe Kampasi ya Dar es salaam yaliyofanyika ijumaa ya tarehe 14 Disemba 2012.


Picha part TWO ya furaha na smile za wadau kwenye maafali ya 11 ya Chuo Kikuu Cha Mzumbe Kampasi ya Dar es salaam yaliyofanyika ijumaa ya tarehe 14 Disemba 2012.


The familly.

Edgar Mapande akipokea zawadi ya maua toka kwa Doreen, kwenye maafali ya 11 ya Chuo Kikuu Cha Mzumbe Kampasi ya Dar es salaam yaliyofanyika ijumaa ya tarehe 14 Disemba 2012.


Ni wakati wa zawadi kutoka kushoto ni Oliver Ryanna, Ibra Gobos, Fatma Kilinda na Edgar Mapande...


Hongera sana Mwanadafada Agnes Mniko.


Mtunukiwa Edgar Jonas Mapande akimlisha keki  Eva Mbaga huku mama wa mtoto huyo Gisele Mbaga akishuhudia tukio hilo muhimu la kumbukumbu.


"Hongera kijana" Says Beatrice Jairo.


Eduze akiwa na dadake Milicent Jesse Bujiku.

Furaha iliyoje kwa madadaz kwenye tukio muhimu la kaka yao.


Mhitimu Bw.Edgar akipokea tuzo ya Best student on the Highest Thesis Marks Of Msc Marketing at Main Campus Morogoro.


Picha ya familia kutoka kushoto ni Mr & Mrs Lushaka, Mr & Mrs Elias Nyamwija, Mrs Rodha Tibehenderwa, Mr & Mrs Malele, Mr & Mrs Reward Mapande na Mr &Mrs Julius Mbaga. 


Mtunukiwa Edgar Jonas Mapande akipata picha ya pamoja na familia ya Bw. John Mbaga (R) ambaye ni CEO wa Bayport Financial Service Ltd, kulia ni mkewe  Gisele Mbaga na mtoto  Eva Mbaga.