ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 6, 2012

LEO TUNAANZIA NDANI YA PINDI LA BONGO FLEVA KISHA SEVIS ZA MAMISOSI LIDAZ

Kama unasikiliza Blongo fleva kwa sasa Manyang'au hawa ndiyo wanakisanukisha.

Adam Mchovu na Fid Q.

Bize...
Bhaaaaassss!!

Wanachomekaje ndani ya Lidaz right now...

Chipus....

Choma za viwango vya mbele....


Vyuku saaaana...

Wambusa na inshu zingine za kukarangiza.

Chomex

Ng;ombe 25 zimechinjwa ndani ya viwanja hivi kwa mpango mzima wa leo.

Ni moja tu ya kona za mimina mimina...

The Crew.

Mishikakiz

Kumbukumbu kuwekwa leo.

MWANZA NA AJIRA.

     Hivi majuzi katika ziara ya Mh. Waziri mkuu Mizengo K. Pinda alitoa wito kwa wakazi wa jimbo la Nyamagana kuhakikisha kuwa wanafanya uvuvi endelevu ili kunusuru zao la samaki na wimbi la uvuvi haramu linalotishia biashara hiyo kuanguka lengo la kauli hiyo ni kuboresha sekta hiyo iendelee kuchangia pato la mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Mji wa Mwanza umejengwa na uvuvi. Eneo la jimbo la Nyamagana lina kilomitaza mraba ya nchi kavu 185 na wakazi wanaokadiriwa kuwa 300,000 na 3% ni wazawa na 8% ni wageni kutoka mikoa jirani.

     Kwakuzingatia binadamu hana urafiki na Nyoka basi kabila la Wasukuma limezidi kumudu maisha na kuchangia uchumi wa familia na taifa kadhalika kujipatia sifa maradufu kitaifa na kimataifa baada ya kucheza ngoma zao na Nyoka na kuwa kivutio kwa watu. Ieleweke bayana kuwa 80% ya Nyoka wote hawana sumu. 

Swali la kujiuliza Unautumiaje utamaduni wako katika kuchangia pato lako binafsi na pato la Taifa ikiwa ni mkakati wa kupunguza umaskini na kuongeza kipato cha mtu kwa kuongeza ajira kwa vijana ambapo 60% ya vijana hawana ajira?

     Kazi ni kazi ‘bhana’… Asilimia 60% ya vijana nchini hawana ajira.

     Tinga Tinga ni mapambo yaliyobuniwa kutoka mkoa wa Iringa nchini Tanzania na kuhimili soko la kitaifa na kimataifa. Chakustaajabisha biashara hii nje ya mipaka ya Tanzania inasadikika kujulikana kama ni mapambo asili ya Kenya hivyo Kenya imekuwa ikipata fedha zakigeni maradufu na watanzania wakiambulia patupu. Mjane Magreth Jaffy Mollel mmiliki wa Tinga Tinga arts Gallery ambaye marehemu mumewake

Swala la ajira nchini Tanzania limekuwa mtambuka na kuwezesha sector binafsi kufikia 35% isiyo rasmi ambapo sheria za nchi imeziainisha na kuweka utaratibu unaomuwezesha mtu kufanya biashara kulingana na mtaji wake. Miongoni mwa ajira hiyo Boda boda kuchangia vijana kujiajiri japo kama Boda Boda wa jiji la Mwanza hawana Bima ya ajari.

 Hofu kubwa ni uendeshaji usiozingatia sheria na taratibu ikiwa na leseni na umakini kazini. Taasis watu binafsi mnashiriki vipi kuwezesha ajira35% isiyo lasmi iweze kuwa rasmi na kupunguza 60% ya vijana ambao hawana ajira? Japo kama umakini ktk uendeshaji wa boda boda unahitajika ili kuepusha ajari

Wahenga waronga:- mtaji wa masikini ni nguvu zake. Na dunia ya leo inasema ili uwe mfanya biashara uliyefanikiwa na unayetaka kufanikiwa kwa haraka na kwa wepesi basi 
1. nilazima ufanye biashara ya mtandao tofauti na kuchukua mzigo na kukaa na kusubiri mteja akufuate hapo ulipo.

2 Ujue mshindani wako katika biashara. 

3. Uatambue mteja wako. 

4. Uwe mbunifu na kutambua fursailiyopo inayoweza kupelekea ukawa tofauti na wafanya biashara wanaokuzunguka. Wewe unaonaje katika bisahara yako?    

Camera inaweza kutumiwa kama chombo cha kuchukua kumbukumbu lakini kwa Alex Nyoni Enhard kijana mwenye umri wa miaka 25 mwenyeji kutoka mkoa wa Mbeya ni ajira inayomuwezesha kumudu maisha yake kila siku na kumsaidia kupata 8000 kwa siku mpaka 150000 mara 3 kwa mwezi. Kwakua yeye ni mtoto wa kwanza ktk familia yake basi biashara hii isiyokuwa na bima au mkopo ameweza kuimudu kwa miaka mitatu na kumwezesha kuwa na familia ya watu watatu na kusomesha wadogo zake wawilili.

 Japo kama ana account bank kipato chote anachokipata kinaishia kinywani na kwenye mzunguko wa mahitaji ya familia. Mafanikio makuu ambayo ameyapata katika biashara hii ni pamoja na kuimarisha mahusiano na watu na kufanhamika.
   

HABARI ZA USIKU HUU NDANI YA LIDAZ CLUB

Hapo kwa  Benny Kinyaiya na Shadee.......?

Hapa ndipo shughuli itapigwa....

Mchaina wa Clouds Tv akiwa na brozee wa Club 10.

Engo....

Wakali kutoka himaya yetu wote wamemiminika hapa kwaajili ya kufanya majaribio.

Mmmmmh...!

Ni Shilole, Inspector Haroon na Baby Madaha... Chege yuleeeeee!!!

Ni Baby Madaha, Mchaina na Keysher.

Pamoja na kuwa dekoresheni za jukwaa zinaendelea viwanjani hapa vilevile sound ya mtikisiko ambayo imeongezwa nyenzo zaidi inajaribiwa hapa. 

Safu ya wahapa hapa ni Ben Kinyaiya, Dj Venture, Peter Moo na Kelvin Twissa

Ze stage usiku huu..

Bado tupo.....

MWANAMUZIKI WAKIMATAIFA RICK ROSS ATUA DAR USIKU HUU

Meneja wa Bia ya Serengeti ambao ndio wadhamini wakuu wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012,Allan Chonjo akisalimiana na Mwanamuziki wa Kimataifa kutoka nchini Marekani Rick Ross mara baada ya kuwasili usiku huu ndani ya uwanija wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,akiwa na baadhi ya wanamuziki wenzake pichani nyuma,kati ni Oparesheni Meneja wa Prime Time Promotions Ltd,Balozi Kindamba ambao ndio waratibu wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012 linalotarajiwa kufanyika hapo kesho.Picha nyingine baadae kidoogo wadau. 

 Rick Ross akitoa salamu ya salut kwa washabiki wake waliojitokeza usiku huu (hawapo pichani) kumlaki

 Operesheni Meneja wa Prime Time Promotions,Balozi Kindamba akiwaongoza wageni wake kuelekea kwenye gari tayari kuondoka kuolekea kwenye hoteli waliopangiwa kufikia usiku huu,Shoto ni Rick Ross na akiwa na baadhi wanamuziki wenzake aliombatana nao .

 Rick Ross akiingia ndani ya mchuma.

Rick Ross akiondoka na mchuma wake kuelekea hotelini usiku huu.

Mmoja wa mashabiki wa Rick Ross aliyezua tafrani kiaina akijifananisha na Rick Ross akizungumza na na baadhi ya watu waliojitokeza kumlaki The Big Boss mwenye Rick Ross.

Friday, October 5, 2012

AIRTEL NA MWENDELEZO WA WIKI YA HUDMA KWA WATEJA.

Mkurungezi wa spanco Tanzania bw Chandrashekhar Narayanan akizungumza na waandishi wa habari wakati wa maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja ambapo Airtel imesherehekea na wateja wake kwa kuwashukuru kwa kutumia huduma Zake, Kushoto ni Mkuu wa kitengo cha huduma kwa wateja Airtel bi Adrianna Lyamba  na  kulia ni Meneja uendeshaji Amit Arora.


Mkurugenzi wa Airtel Sam Elangallor akiongea na waandishi wa habari wakati wa maathimisho ya wiki ya ya wiki ya huduma kwa wateja ambapo Airtel imesherehekea na wateja wake kwa kuwashukuru kwa kutumia huduma Zake

Airtel yaadhimisha wiki ya Huduma kwa wateja, yaahidi kuendelea kutoa huduma za kisasa
·         Kauli mbiu “Ni mimi wa kukupa huduma bora “ Airtel inadhihirisha mteja ni muhimu
·         Airtel yawaahidi wateja huduma bora na za kisasa nchini

Dar es salaam, 4 Oktoba 2012 Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Imeshiriki katika maadhimisho ya wiki ya huduma kwa mteja duniani kwa kutoa na kuahidi kuendelea kutoa  huduma bora na za kisasa kwa wateja wake hapa nchini.

Ahadi hiyo imetolewa na Mkurugenzi mkuu wa Airtel Tanzania Bw. Sam Elangalloor leo Jijini dar ikiwa ni katikati ya maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja wa kampuni hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania bw Sam Elangalloor alisema “Airtel imejipanga kutoa huduma bora na za kimataifa kwa kuwa tumewekeza kikamilifu katika vitendea kazi vya kisasa na pia tunashirikiana kikamilifu na wadau wetu wataalam wa huduma kwa wateja SPANCO RAPS –Tanzania Limited ili kumpatia mteja huduma yenye ubora zaidi kila wakati, tunawatoa huduma zaidi ya 650 wakitoa huduma masaa 24 siku 7 za wiki. Airtel tutaendelea na dhamira yetu hii ya kutoa huduma bora na ya kisasa ili kuendelea kuvutia wateja wengi kutumia mtandao wa Airtel pamoja na kutimiza malengo yao mbalimbali.”

Sam aliendelea kwa kusema” tumewekeza kwa kiasi kikubwa kupanua wigo wa mawasiliano hasa vijijini na hivyo tumekuwa na ongezeko kubwa la wateja  wanaojiunga kwenye huduma zetu. Leo asilimia 97 za simu zinazopigwa kwenye kituo chetu cha huduma kwa wateja ni zakutaka ufafanuzi wa namna ya kutumia huduma zetu za Internet, meseji, namna ya kutumia simu, Airtel money na nyingine zinazofanana na hizo

Vileviele Airtel tumewekeza kikamilifu katika mfumo wetu wa ndani na nje wa mawasiliano kwa kuweka miundombinu ya kisasa kwa lengo la kuwahudumia wateja kwa haraka na urahisi zaidi. Airtel tunaushirikiano mkubwa na IBM wataalam wakubwa katika teknolojia ya mwasiliano duniani ikiwa ni muendelezo wa  kutimiza dhamira yetu kuhakikisha tunatoa mawasiliano bora na nafuu kwa kumfaidisha mteja wetu wakati wote atumiapo huduma za Airtel” aliongeza bw Elangalloor

Kwa upande wake mkuu wa kitengo cha huduma kwa wateja Adriana Lyamba alisema” tunao wafanyakazi waliopata mafunzo na wanaoendelea kupewa mafunzo mbalimbali ili kwenda na mabadiliko mbalimbali ya technologia za kisasa. Hivi karibuni tulizindua Mafunzo ya muda mrefu yajulikanayo kama Airtel Service Academy ili kuwawezesha wafanyakazi wetu kuongeza ufanisi kwa kupitia mafunzo haya”.

Sambamba na hilo tumewekeza kwenye technolojia za kisasa ili kuwawezesha wateja wetu kutufikia kirahisi kupitia call center zetu. Leo tunayofuraha kuweza kuwasiliana na  wateja wetu nchi nzima kupitia mawakala au kwa kupiga namba 0784001001 bila malipo na kuweza kupata taarifa mbalimbali zikiwemo ofa kabambe, huduma za internet, kupiga na kutuma ujumbe mfupi na nyingine nyingi”

Airtel call center inapatikana masaa 24 siku 7 za wiki, na tunapokea simu zaidi ya laki moja kwa siku hii ni kutokana na wateja wetu wengi kutumia huduma za simu na internet  mara ya kwanza,

Maduka yetu yanafunguliwa kuanzia saa 2 hadi saa moja usiku, ili kuweza mteja wetu ili kuwasiliana nasi tafadhali piga namba 100 bure au piga +255 78 4105 400+255 78 4104 800 ikiwa unatumia namba ya mtando mwengine na utatozwa gharama ya kupiga simu ya kawaida,  vilevile unaweza kutupata kwa kupitia barua pepe Email info@tz.airtel.com.” aliongeza Lyamba

Nae Mkurugenzi wa Spanco Tanzania Chandrashekhar Narayanan alisema” tunayofuraha kushirikiana na Airtel katika kutoa huduma bora kwa wateja Tanzania. Tunaamini huduma bora tunayoitoa inafanikisha lengo la Airtel la kuwa mtandao unaopendwa na watanzania nchini. Tunauzoefu wa kutoa huduma kwa wateja katika nchi mbalimbali duniani ikiwa ni pamoja na kupokea simu za wateja zaidi ya 400000 kwa siku”

Wiki ya huduma kwa wateja huadhimishwa tarehe mosi hadi tano ya mwezi October Duniani kote na hapa nchini kampuni ya Airtel yenye wateja zaidi ya milioni 8 inafanya maadhimisho hayo kwa shughuli mbalimbali huku kauli mbiu yao ikiwa ni “ Ni mimi wa kukupa huduma bora “ Airtel inadhihirisha mteja ni muhimu

Airtel ni mtandao wenye gharama nafuu na wenye mtandao mpana ulioenea zaidi kwa utoa huduma kama vile Airtel money ambayo imewezesha upatikanaji wa huduma za kifedha kirahisa kwa gharama mahali popote nchini.

NYUMBANI 88.4



Kutoka kushoto ni Anthonio Nugaz, Suka, Ally, Mlope na G. Sengo.


Salum Mwinyi, G. Sengo na Faraja Kyarenda.


Mablogers Michuzi Jr, G.Sengo na Dj Fetty.


Sports Xtra kijiweni zaidi.


Ndani ya kipindi cha Jahazi Michapo ya Michezo. 


18:00 wakati wa kupata habari ya Phillip Muyava.


Presenter Lodge:- Ni Millard Ayo wa Amplifaya, Vanessa Mdee na Shadee. 

Tukikamilisha Jahazi kupisha Amplifaya.


Bhaaaaaassss.