ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, April 14, 2012

HAYA HAYA.... NI WIKIENDI JAMANI....

Kama uko home jumamosi ya leo basi mida hii ya jioni kupitia TBC 1 umetoka kucheki mavituuuuZzz ya hawa majamaa katika kipindi chao 'Ben and mai' ila leo sijamwona kabisa kwenye chupa mwanadada Mai... Where is she bhana?

MKUU WA MKOA WA MWANZA AFUNGUA MKUTANO MKUU WA CHAMA CHA SOKA MKOA (MZFA)

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh. E Ndikilo akifungua mkutano MZFA.
Imetajwa kuwa kukosekana kwa uaminifu, matumizi mabaya ya madaraka sambamba na migogoro isiyoisha ndani ya vilabu na vyama vya michezo mkoani Mwanza ndiyo chanzo kikuu cha kuporomoka kwa michezo hususani soka kwa jiji la Mwanza.

Hayo yamebainishwa leo na mkuu wa mkoa wa Mwanza Injinia Ernest Ndikilo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Chama cha soka mkoa wa Mwanza (MZFA) unao kaa kila mwaka kuweka mikakati ya maendeleo na kujadili mstakabali mzima wa maendeleo ya soka.
Ongezeko la idadi ya watu na huduma mbalimbali za kijamii ile hali idadi ya viwanja inabaki palepale huku vingine vikibadilishwa matumizi imekuwa ni changamoto kubwa kwa mkoa wa Mwanza na wilaya zake.

Pia Mh Ndikilo hakuacha kuwapasha makocha wanaogeuza vyeti vyao mapambo ile hali walishiriki mafunzo ya Ukocha na fedha nyingi kutumika

Ili kurejesha heshima ya historia ya soka Mkoa wa Mwanza umeweka mikakati ya kuhakikisha unaingiza timu zaidi ya mbili katika ligi kuu zoezi ambalo litakwenda sambamba na uendelezaji wa vipaji vinavyochipukia.

Stori za ziada baina ya wajumbe wa MZFA na mkuu wa mkoa.

Picha ya pamoja.

Jumla ya wajumbe 33 kati ya 36 toka wilaya mbalimbali za jiji la Mwanza wamehudhuria mkutano huo wa mwaka uliofanyika katika ukumbi wa mikutano ukliopo ndani ya uwanja wa michezo CCM Kirumba Mwanza.

Friday, April 13, 2012

RAIS JAKAYA KIKWETE AWAAPISHA MWENYEKITI NA WAJUMBE WA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA MPYA IKULU LEO

Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Jaji Joseph Sinde Warioba, kuwa Mwenyekiti wa Tume ya mchakato wa kutafuta maoni ya Katiba Mpya, wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam leo.

Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Said Elmaamri, kuwa Mjumbe wa Tume ya mchakato wa kutafuta maoni ya Katiba Mpya, wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam leo.

Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria hafla hiyo katika Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam leo.

Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Jaji Agustini Ramadhan, kuwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya mchakato wa kutafuta maoni ya Katiba Mpya, wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Jaji Salim Ahmed Salim, kuwa Mjumbe wa Tume ya mchakato wa kutafuta maoni ya Katiba Mpya, wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam leo.

Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Mbunge wa Viti Maalum, Al-shymaa Kwegiyr, kuwa Mjumbe wa Tume ya mchakato wa kutafuta maoni ya Katiba Mpya, wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Said Elmaamri, kuwa Mjumbe wa Tume ya mchakato wa kutafuta maoni ya Katiba Mpya, wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam leo.

Rais Jakaya Kikwete na Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakiwapongeza wajumbe wa Tume hiyo baada ya kuapishwa rasmi katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Dar es Salaam leo.

Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Said Elmaamri, kuwa Mjumbe wa Tume ya mchakato wa kutafuta maoni ya Katiba Mpya, wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam leo. Picha na Muhidin Sufiani. OMR

Thursday, April 12, 2012

Tb JOSHUA ATABIRI KIFO CHA MUIGIZAJI NOLLYWOOD

Baada ya kutabiri kifo cha mmoja wa rais wa bara la Afrika, mtumishi wa Mungu Nabii na Mtume TB Joshua ametabiri kifo cha mwigizaji mwingine wa kiume wa Nollywood na ameomba ukiwa kama MwafriKa anaomba maombi yako kumwombea mungu amuepushie na kifo else basi mapenzi ya Mungu yatimizwe akasema muigizaji huyo ni wa kiume hivyo sala zaidi zinaombwa kwa waigizaji wafanye maombi ya kufunga na kuomba.

Fafanuzi toka kwa wadadisi wa mambo juu ya tabiri zinazotoka kwa kinywa cha mtumishi huyu wa Mungu zinasema.. Kitu ambacho wengi hawaelewi ni kuwa nabii siyo final say. Mungu ndiye final say. Kinachotokea ni kuwa Mungu anamwonesha nabii kitakachotokea mbeleni. Na wajibu wa nabii ni kuomba rehema za Mungu ili ikiwezekana Mungu aahirishe tukio tarajiwa. Mungu huonesha nabii kwa sababu mbili kwamba akae kwenye nafasi yake aombe au basi watu wajue kama halikuwa jambo linalotolewa unabii. Ndio utasikia anasema kwamba yeye anamwomba Mungu na anaomba watu waombe. Kuwa nabii siyo ujiko ila ni kazi maana utadaiwa. Ni mzigo mzito sana ndio maana tangu zamani hatuwi na manabii wengi kwa wakati moja. Yaani lazima kuna nabii na wana wa manabii kama enzi za Eliya.

MAREHEMU JENERALI MSTAAFU ERNEST MWITA KIARO AAGWA RASMI LEO JIJINI MWANZA

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh. Ernest Ndikilo leo ameongoza Umma aliojitokeza kutoa salamu za rambirambi kwa mwili wa aliyewahi kuwa mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama nchini Jenerali Mstaafu Ernest Mwita Kiaro aliyefariki dunia siku ya Jumanne wiki hii akiwa na umri wa miaka 87 ambaye ameagwa rasmi leo jijini Mwanza.

Jenerali Mstaafu Ernest Mwita Kiaro alizaliwa mnamo tarehe 1/01/1923 nakufariki dunia 10/04/2012.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Ernest Ndikiro akimfariji mke mdogo wa marehemu Zainab Kiaro.

Mmoja wa wanafamilia (Kushoto) akimfariji mke wa kwanza wa marehemu Jenerali Mstaafu Ernest Mwita Kiaro aitwaye Penina Kiaro (Kulia).

Makamanda wakijadiliana.

Makamanda wakizidi kufurika eneo la tukio kutoa salamu zao za mwisho kwa mwili wa marehemu.

Makamanda wakiwa eneo la juu katika kilima kidogo cha mawe ili kushuhudia ibada ya salamu za mwisho jijini Mwanza.

Safu ya Makamanda wengine.

Mwili huo ulitoka katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando mchana na hatimaye majira ya saa saba ukaagwa hapa katika nyumba yake ya kikazi maeneo ya Kapripoint kabla ya kusafirishwa kuelekea wilayani Tarime mkoani Mara kwaajili ya Mazishi.

Kwa mwendo wa pole mwili ulipelekwa eneo rasmi.

Moja kati ya wanajeshi akiongoza moja ya vifungu kwenye ibada hiyo.

Mapaparazi.

Wakati wa kutoa heshima za mwisho uliwadia.

Jeshi la polisi usalama barabarani nao walikuwepo kutoa heshima zao.

Heshima...

Heshima ziliendelea kutolewa.

Makamanda wakipanga mikakati.

Mzee Gachuma katikati akifanya majadiliano na baadhi ya maafisa wa Jeshi.

Msafara.

Mwili wa marehemu aliye kuwa mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama nchini Jenerali Mstaafu Ernest Mwita Kiaro umesafirishwa leo kuelekea wilayani Tarime mkoani Mara kwaajili ya Mazishi ambayo yatafanyika kesho.

Wednesday, April 11, 2012

WAKAZI WA PWANI YA DAR ES SALAAM WAONYWA JUU YA KUTOKEA TSUNAMI BAADA YA INDONESIA KUKUMBWA NA BALAA

Wakazi wa mkoa wa Dar es salaam nchini Tanzania kupitia Mamlaka ya hali ya hewa wamepewa taarifa ya tahadhari kukaa mbali na maeneo ya mwambao wa bahari kupitia tishio la Tsunami kulikumba eneo la pwani ya bahari ya Hindi.

Wavuvi na abiria wasafiriao mitumbwi na boti wametahadharishwa kuondoka kabisa maeneo ya pwani ili kuepuka balaa lolote linaloweza kujitokeza kwani 'heri ya kinga kuliko tiba'

Katika hatua nyingine safari zote katika bahari ya Hindi kutoka au kuelekea visiwani Zanzibar zimesitishwa kwa muda hadi kesho saa mbili asubuhi kwaajili ya sababu za kiusalama huku wananchi wakipewa taarifa ya kutopata hofu juu ya hatma yao.

Hofu nchini Indonesia
Mapema leo yametokea matetemeko makubwa mawili ya kipimo cha Ritchter 8.3 na 8.6 huko Aceh Indonesia ambapo tahadhari ya kutokea kwa Tsunami imeshatolewa na wakazi katika mwambao wa Bahari ya Hindi hasa majira ya saa 1 usiku hadi saa 3 usiku wa leo wametakiwa kuchukua tahadhari.

Experts said a tsunami wave had been produced, but there were no reports of damage and it remained unclear how big the wave would be.

Area prone to volcanic and seismic activity
Indonesia straddles a series of fault lines that makes the vast island nation prone to volcanic and seismic activity.According to the USGS, the 2004 quake struck about 155 south-southeast of Banda Aceh at a depth of 18.6 miles. Some 227,898 people were killed or missing presumed dead and about 1.7 million were forced out of their homes after the tsunami affected 14 countries in Asia and East Africa.

LULU’S SIDE OF THE STORY AS KANUMBA IS BURIED

Vice President Mohammed Gharib Bilal pays his last respects at Leaders Club grounds. Dressed in white in the background is First Lady Salma Kikwete. PH/SAID POWA
By Mkinga Mkinga
The Citizen Reporter
Dar es Salaam.

The prime suspect in the death on Saturday of local film star Steven Kanumba spoke out on the tragedy for the first time just a day before tens of thousands of people gathered for his funeral yesterday.Elizabeth Michael, alias Lulu, broke her silence on Monday—two days after she was arrested. Investigators at Oysterbay police station had to engage a crime psychologist to get her to open up on the events leading up to the death of the star who had just been invited to Hollywood in the United States.

Highly placed police sources told The Citizen in an exclusive interview yesterday that Lulu, girlfriend of the deceased, started narrating what had transpired on the night the 28-year-old died after meeting the psychologist.

“The suspect, who had refused to cooperate with police detectives from the Kinondoni regional police office, has now managed to speak for three hours with the psychologist,” the sources said on condition of anonymity since they are not official spokespersons of the Tanzania Police Force.

The psychologist from the Criminal Investigation Department (CID) headquarters in Dar es Salaam chatted candidly with the suspect for three hours on Monday, a day before Kanumba was buried.

Lulu reportedly told the investigators that Kanumba phoned her on the fateful night asking her to join him for an outing. She went to his home but told him she did not really want to go out and that she preferred to return home. Kanumba allegedly wanted Lulu to accompany him to a Mashujaa Band show at Vingunguti, and became furious when she refused to accompany him.

According to the sources, the misunderstanding between the two developed into a quarrel, with Kanumba demanding to know what it was that she had left at her home.“According to Lulu, the deceased locked the door to his room,” said the sources. “In a panic, she unlocked the door and fled.”

Lulu is quoted as saying that she managed to escape after he fell and had no idea what transpired after her departure.
The sources said police have also interrogated another suspect, a Bongo Flava musician (name withheld), who gave Lulu a lift when she left Kanumba’s Sinza residence. “I am sorry, brother, I cannot comment on that issue,” he told The Citizen before he hang up.

According to detectives, other suspects have also been lined up for questioning. The sources could not say how long the interrogations would take.

In another development, the sources said heavyweight politicians related to Lulu have been sending her consolation text messages pledging to assist her. “Their involvement with the suspect could complicate our investigations,” said the sources.
Yesterday, this paper reported that Kanumba died of a brain injury caused by a sudden blow to the head.

One of the doctors who examined Kanumba’s body at Muhimbili National Hospital hinted that the actor died on the spot after suffering such severe brain damage that he collapsed and stopped breathing.

His sudden death sent shockwaves across the country, East Africa and West Africa—particularly Ghana and Nigeria—where he had achieved prominence in the continent’s leading film industry, Nollywood. He had returned home from a trip to Ghana just a few days before his death.

President Jakaya Kikwete joined mourners on Sunday, calling the fallen star a brilliant ambassador who sold Tanzania far and wide through the screen.

NAIWEKA HAPA ILI KILA MTU AISOME
Source: The Citizen

JENERALI KIARO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama nchini, Jenerali mstaafu Ernest Mwita Kiaro (Pichani), amefariki dunia jana asubuhi akiwa na umri wa miaka 87.

Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Job Masima, Jenerali Kiaro amefariki dunia saa 4.20 asubuhi kwa ugonjwa akiwa katika Hospitali ya Bugando Mwanza.

Masima alisema mipango ya mazishi inafanywa kwa pamoja kati ya Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na familia ya Marehemu. Aidha, alisema ratiba ya mazishi itatolewa baadaye.

Jenerali Kiaro alikuwa ni Mkuu wa Nne wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania kati ya mwaka 1988-1994.

Katika hatua nyingine, Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jakaya Kikwete amemtumia Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange salamu za rambirambi kuomboleza kifo cha Jenerali Mstaafu Kiaro.

Katika salamu zake kwa Jenerali Mwamunyange, Rais Kikwete amemwomba Mkuu huyo wa Majeshi ya Ulinzi kumfikishia salamu za rambirambi za dhati ya moyo wake kwa familia ya Jenerali Mstaafu Kiaro na kwa makamanda na wapiganaji wote wa Majeshi ya Ulinzi kwa kumpoteza mdau, mwenzi wao na kiongozi wao.

Rais Kikwete amesema katika salamu zake, “Nimepokea kwa huzuni nyingi na majonzi mkubwa taarifa ya kifo cha Jenerali mstaafu Ernest Mwita Kiaro ambaye ameaga dunia asubuhi ya leo (jana) katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Mwanza, ambako alikuwa amelazwa.

“Nilimfahamu vizuri na nilifanya kazi na Jenerali Kiaro wakati wa enzi ya uhai wake. Alikuwa Mtanzania mzalendo wa kuigwa, mwadilifu na mwaminifu kwa taifa lake, mchapakazi hodari na mpiganaji na Kamanda wa mfano kabisa kwa waliokuwa chini yake,” alisema Rais Kikwete na kuongeza:

“Alithibitisha sifa zake hizo katika kipindi chote cha miaka 50 na miezi 11 alipokuwa katika ulinzi wa nchi yetu, tokea alipokuwa mpiganaji hadi alipopanda na kuwa Kamanda na hatimaye Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi kwa kipindi cha miaka minne kati ya 1988 hadi Februari 25, 1992, alipostaafu utumishi wa Jeshi. Tutaendelea kumkumbuka na kumuenzi kwa utumishi wake uliotukuka kwa taifa letu.”

Tuesday, April 10, 2012

KILIMANJARO PREMIUM LAGER EASTER BONANZA AT CCM KIRUMBA STADIUM ILIVYOKUWA.

Mgeni rasmi Afisa Usalama wa Mkoa Bwana Mutash akiongea na wachezaji wa mpira wa pete kabla ya ufunguzi wa bonanza. Bonanza hili lilifanyika katika viwanja vya CCM Kirumba na baadae sherehe fupi ndani ya Shooter’s Pub ambayo ilidhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania.

Maveteran wa Mwanza na Dodoma wakilisakata kabumbu katika mchezo wa kwanza wa mpira wa miguu, timu hizo zilitoka sare ya bao 2-2.

Haya ndo mambo yalivyokua katika bonanza la sikukuu ya Pasaka, hapa ilikua mechi kati ya Mwanza na Isaka ambayo pia matokeo yalikua sare ya 1-1.

Baadhi ya mashabiki wakifuatilia kwa umakini bonanza la maveterani huku wakichati kwa nafasi.

Wadau wakiwa ndani ya Shooter’s Pub wakisherehekea baada ya bonanza la Pasaka kuisha majira ya jioni hivi.
PICHA NA ERICK TBL MZA