ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, January 14, 2012

SHAVU KWA WASANII LAKE ZONE.

AFYA RADIO -96.8 Mhz

Kwako Msanii wa Lake Zone kama unangoma unaiamini na unahitaji kutoka tuko kiHoME zaidi kama vp 'tUPIa' ngoma yako ktk email-iddjuma10@yahoo.com au weekendjumpoff@yahoo.com au fika mjengoni, capripoint MZA town uliza Anko Idd, Mr Credit au Bonge nafkiri utakuwa umenisomaaaa!!!!

@Idd Juma

BREAKING NEWS: AJALI YAPOTEZA MAISHA YA MBUNGE WA CHADEMA REGINA MTEMA

REGINA MTEMA ENZI ZA UHAI WAKE.
Habari tunazozipata hivi sasa kutoka vyanzo vya ndani ya CHADEMA zinamtaja aliyekuwa Mwanaharakati shupavu Mbunge wa viti maalum kupitia CHADEMA jimbo la Morogoro Regina Mtema kuwa amefariki dunia kupitia ajali mbaya ya gari iliyotokea leo katika eneo la daraja la Ruvu akiwa safarini kutokea jijini Dar es salaam kuelekea mkoani Morogoro. Bi. Mtema alikuwa na familia yake akiwemo mama yake mzazi. Majeruhi wote wamepelekwa kwenye Hospitali ya Tumbi, kibaha-Pwani.Habari hizi zinatukuta tukiwa kikaoni.
Katika kumuenzi mbunge huyo Wanachama wa chama cha wandishi wahabari mkoa wa Mwanza (MPC) walisimama kwa muda wa dakika moja.

BLOGU HII INAUNGANA NA WALE WOTE WAZALENDO WALIOGUSWA.
MWENYEZI MUNGU ILAZE ROHO YA MAREHEMU REGINA MTEMA MAHALI PEMA PEPONI AMEN.
Habari zaidi tutaendelea kupashana.

MDAHALO KUHUSU TASNIA YA HABARI NA MCHAKATO WA KATIBA MPYA TANZANIA

Mgeni rasmi mkuu wa Wilaya ya Ilemela Said Amanzi akitoa hotuba ya ufunguzi wa Mkutano mkuu maalum wa MPC aliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya jiji la Mwanza.

Mwezeshaji-Emanuel Bulendu kwa ufupi alizungumzia Mapungufu yaliyopo katika hali ya habari Zanzibar, Kinga za wabunge v/s wandishi wa habari, Maslahi ya wandishi wa habari Tanzania na Nguvu ya Vyama vya Habari katika kulinda maslahi ya wanahabari.

Mwezeshaji-Dennis Mpagaze kwa upande wake masuala yaliyochomoza ni pamoja na Tuhuma kwa wanahabari kujikita kuandika habari za watu wenye pesa na kuwatelekeza walalahoi wa taifa hili, Vyombo vya habari kutumika kuharibu maadili pia wanajamii wanachangia kiasi gani kuwezesha sekta ya habari kukabiliana na changamoto.

Mwezeshaji-Ray Naluyaga, Huwezi kuwa na jamii iliyo na demokrasia ya kweli bila kuwa na mabadiliko katika sheria, Wandishi wajikite kujiendeleza kielimu ili Media ifanye kazi yake vizuri kama inavyohitajika.

Mwakilishi wa taasisi za dini Christopher Kubeja
"Mswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba haujabainisha muda wa mtiririko mzima wa zoezi hili. Inapendekezwa ukomo wa muda uwekwe kwenye mtiririko wa mchakato wa kukusanya maoni ili kuepuka kuwa na mchakato kwa muda usiojulikana na kuleta uwajibikaji. Sambamba na hilo, kuna haja ya kuelekeza nguvu kazi pamoja na rasimali za kutosha kwenye hatua zote za mchakato ili Katiba inayoridhisha wananchi ipatikane". Maelezo zaidi tembelea
http://www.kas.de/wf/doc/kas_5088-1442-1-30.pdf?111114113050


Mwenyekiti Jimmy Luhende akitoa ufafanuzi kwa moja ya ajenda mkutanoni.

Pamoja na kujadili kuhusu "Katiba mpya na Habari" pia mkutano huo ulikaa na kujadili Mapitio ya Mkutano uliopita na marekebisho ya Katiba ya MPC.

Friday, January 13, 2012

GOR MAHIA YASAJILI 6WAPYA IVO MAPUNDA NDANI

Katika kujiandaa na msimu mpya wa ligi kuu nchini Kenya, timu ya soka ya Gor Mahia leo imetambulisha wachezaji wake sita wapya iliyosajili kwaajili ya msimu mpya unaotazamiwa kuanza wiki chache zijazo akiwemo golikipa wa zamani wa Tanzania (Taifa Stars) Ivo Mapunda.Mshambuliaji George Midenyo (pichani) amenyakuliwa na Gor Mahia toka timu ya Tusker ya nchini humo, Ivo Mapunda na mwenzake Rama Salim wamesajiliwa kutoka Congo United, wengine ni Yusuf Juma kutoka Thika United, Ali Hassan na Hugo Nzoka toka Sony Sugar.

Gor Mahia safari hii imejizatiti kufukuzia hatimaye kuyanyakuwa mataji yote matatu nchini humo likiwemo kombe la ligi kuu ya KPL, KFK Cup na KPL Top 8 trophy.

MWAMVITA'S CHARITY SALE KUFANYIKA KESHO

Bango
Kiki and Shamim....
Mwammy, Flavianna, Joselene, and Mange, sorting out cloths..
Mwammy pricing clothes....
Office wear....OMG yaaani..
Long dresses za ukweeee.....
Office wear...pencil skirts na mashati...
aaaawwww.... viwalo vya ukweeee....
Mwamvita anasema "Mmekuwa mkiuliza bei za nguo"
Bei za nguo ni kuanzia 10,000 – 100,000
Yaani bei ni poa sana…… lazima utakuta kitu ambacho u can afford…
Jamani nguo ni nzuri sanaaaa… yani mie ntawahii saa nne kamili niwahi viwalo nilivyovipenda leo maana tulinyimwa kununua leo…. Uwiiiii,nguo ni nzuriiiiiiii!!
Event itaanza 10am – 7pm, Jumamosi (kesho) pale Kikis Fashion. kama hupajui Kikis piga number hii kupewa directions +255714817102 Ila usije kuchelewa ukakuta the best stuff zishanunuliwa hivyo wahi mapema.
Kumbuka kwamba hii kitu yote ni kwa ajili ya kupata pesa kuweza kusomesha watoto yatima, so hata kama unajiona wewe ni mnene huwezi pata size, u can still come na ukamnunulia ndugu yako au rafiki yako chochote just to show ur support.....

Ahsanteni sana and see u tomorrow....
Zaidi tembelea http://u-turn.co.tz/

MRADI WA WANANCHI GEREZANI KIBASILA NI MFANO MZURI WA KUIGWA WAKUJIKOMBOA KIUCHUMI.

Picha inanoyoonesha mradi wa wananchi wazalendo utakavyokua.

Kibasila Estate Public limited company (KEPLC) ni kampuni inayomilikiwa na Wananchi wa kawaida wanaoishi kwenye nyumba 106 walizouziwa na Serikali kwa Mikataba Maalum ya mtu mmoja mmoja kupitia wakala wa majengo Tanzania (TBA), chini ya Wizara ya Miundombinu tokea mwaka 2004. Nyumba hizo zipo katika eneo maarufu liitwalo SHULE YA UHURU, katika makutano ya barabara ya Msimbazi/Lindi, Kata ya Gerezani, wilaya ya Ilala jijini Dar-Es-salaam.

Vikao vinavyoendelea kujadili maswala mbalimbali ya mradi huo.

Mara tu baada yakuuziwa na kupata mikataba yao, wananchi hawa waliamua kujiunga pamoja kwa mtindo wa kuhamasishana na kunadi wazo la kuunda Ushirika yaani Kibasila Housing Cooperative Society, waiombe serikali iwamilikishe eneo lao kwa pamoja, ili wapate urahisi wa kukopesheka na hatimaye kuzijenga upya nyumba zao, waweze kuishi katika nyumba bora zenye thamani wanayostahili na kukidhi viwango vya
mipango miji.


MALENGO YA MRADI

Wananchi wa Gerezani/Kibasila wamepania kuliendeleza eneo lao kibiashara kwa kujenga Vitega uchumi na kuvikodisha ili kupata gawio litakalo wawezesha kuinua hali zao kimaisha, kiuchumi na kijamii na sehemu ya fedha za faida zitumike kulipia gharama za Mradi utakaojengwa.

Kupandisha thamani ya ardhi yao kwa kujenga majengo ya kisasa na yenye kuvutia na hatimaye kubadilisha sura ya eneo la Gerezani na kuwa kitovu cha biashara na kuwa kivutio cha watalii.

Kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuinua maisha ya wananchi wake na kwa kupitia mradi huu maisha yao yataboreshwa.

Kutoa fursa kwa watanzania wengine kuajiriwa, kupata mahali bora pa kuishi na Serikali yao kunufaika kwa kodi kwa kupitia biashara mbalimbali zitakazofanyika katika eneo lao. Na kwa kuwepo na makazi ya kupangisha ya bei ya kati na ya juu.

Kumfanya Mkazi kumiliki na kuendesha uchumi wa nchi yake kivitendo na kuwa mfano wa watanzania wengine.

HASIRA ZA MPANGAJI

MPENZI WA RIWAYA:
BAADA ya kufanya utafiti wa kina juu ya uhusiano uliopo kati ya mwenye nyumba na mpangaji, nikianzia Songea 2005 na kumalizia Mwanza 2011, sasa nakuletea riwaya ya kisayansi(science fiction).
HASIRA ZA MPANGAJI ni riwaya iliyotungwa na mimi Gabriel Nombo. Inaelezea maisha ya watu kwenye sayari iliyo nje ya mfumo wa jua, extrasolar planet. Sayari yenye watu wanaopanga na wanaopangisha nyumba kama watu wa hapa duniani. Tofauti ni kwamba, wao wameendelea zaidi kisayansi na kiteknolojia ukilinganisha na sisi wa duniani.

Pia, kwa asili binadamu wa huko (aliens) wana hasira sana. Kwenye nyumba wanazoishi mifarakano ipo muda wote. Kitu kidogo tu, kwa wao, chaweza zua hasira kubwa.
Tafadhali usiikose riwaya hii ya aina yake. Ipo njiani kukutembelea.

Kwa maoni au maswali, tafadhali nitumie barua pepe hapo chini.
mapigaby@yahoo.com

Thursday, January 12, 2012

AIRTEL YASHEREHEKEA MAPINDUZI KWA KUKABIDHI MSAADA WA BAISKELI 10 VITUO VYA AFYA WILAYANI MISUNGWI

Katika kuadhimisha sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar, Kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi Airtel leo imekabidhi msaada wa baiskeli 10 kwa waganga wafawidhi kutoka vituo 10 vya Idara ya Afya wilayani Misungwi mkoani Mwanza. Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Bi. Mariam Lugaila (C) akimkabidhi baiskeli Mganga mfawidhi wa Kituo cha Afya Mwagiligi kilichopo wilayani humo huku akishuhudiwa na Meneja Biashara wa Kanda ya Ziwa Kampuni ya Airtel bw. Ally Maswanya (R).

Msaada huu wa Baiskeli utawasaidia waganga wakuu wa vituo vya tiba wa vijiji 10 kukabiliana na tatizo la usafiri.

Ally Maswanya
Airtel Tanzania sambamba na kutoa msaada huu wa baiskeli kwa wauguzi pia imeziwezesha shule mbalimbali nchini kwa misaada ya vitabu, madawati na vitendea kazi kadha wa kadha kwa lengo la kurejesha shukurani kwa wananchi na kuisaidia serikali katika harakati zake za maendeleo.

Sehemu ya wauguzi wa Hospitali Kuu Wilaya ya Misungi waliohudhuria makabidhiano hayo.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Bi. Mariam Lugaila (C) akimkabidhi baiskeli Mganga mfawidhi wa Kituo cha Afya Kijima, Dr. Marwa Mwita huku akishuhudiwa na Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Taknolojia, Mbunge wa wilaya ya Misungwi Mh. Charles Kitwanga almaarufu 'Mawe Matatu'.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Bi. Mariam Lugaila akimkabidhi baiskeli Mganga mfawidhi wa Kituo cha Afya Igongwa.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Bi. Mariam Lugaila (C) akimkabidhi baiskeli Mussa Shipemba ambaye alimwakilisha mganga mfawidhi Kituo cha Afya Nyamainza.

Msaada wa baiskeli kutoka Airtel kwa kituo cha Buhunda ukikabidhiwa.

Kaimu Mganga mfawidhi wa Idara ya Afya wilaya ya Misungwi Dr. Beichumila Saula akisoma lisala.
"Tunachangamoto mbalimbali zinazotukabili ikiwa ni pamoja na uhaba wa fedha kuendeshea shughuli mbalimbali, Uchache wa watumishi wa kada mbalimbali, Uhaba wa madawa na vifaa tiba, katika bohari ya dawa ya kanda (MSD), Uhaba wa usafiri katika vituo vya tiba, Asante Airtel".

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Bi. Mariam Lugaila
"Kwa niaba ya watu wangu wa Misungwi - Tunawashukuru sana Airtel tukiwasihi ushirikiano usiishie hapa, uendelee kwani bado kuna mahitaji mengi na makampuni mengine yaige mfano huu"

Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Tekinolojia ambaye ni Mbunge wa Misungwi Mh.Charles kitwanga nae akitoa shukurani.

Mh.Charles kitwanga akipata Picha ya pamoja na wauguzi wa Hospitali ya Wilaya Misungwi.

Misungwi Hospital.

Wednesday, January 11, 2012

KATUNI HII CHIBOKO.......!

Hii kwangu ni tafakuri ngumu na pengine ambayo pia ni nyepesi mno, chunguza mjomba utabaini...

TIMU YA TAIFA YA NGUMI YAENDELEA NA MAZOEZI

Kocha wa timu ya taifa ya mchezo wa ngumi, Edward Lyakwipa (kushoto) akimwelekeza bondia, Mohamed Abdul jinsi ya kuikwepa ngumi uku ukiwa kwenye gadi wakati wa mazaoezi ya kambi hiyo iliyopo uwanja wa ndani ya taifa Dar es salaam.

Baadhi ya mabondia wa timu ya taifa ya Masumbwi wakifanya Mazoezi ya pamoja katika kambi yao iliyopo Uwanja wa ndani wa Taifa Dar es salaam leo.
Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

MH. VICK KAMATA (MBUNGE) ATIMIZA AHADI AKABIDHI BAISKELI 30 KWA WALEMAVU GEITA

Hizi ni moja ya juhudi za mbunge huyo kwa wananchi wake katika kusaidia kuondoa matatizo yanayowakabili watu wenye ulemavu wa viungo ambao wamekuwa wakikabiliwa na matatizo mengi ukiwemo usafiri kama hizi baiskeli zitakazowasaidia kwenda hapa na pale na kuendelea na shughuli zao.Mwenyekiti wa Victoria Foundation Mh. Bi. Vick Kamata yuko Geita kwa wananchi wake kama anavyoonekana pichani akikabidhi baiskeli kwa walemavu 30 wa tarafa ya Bugando wilaya ya Geita mkoa mpya wa Geita.

Vick Kamata akimsaidia kusukuma baiskeli hiyo mmoja wa walemavu mara baada ya kumkabidhi baiskeli hiyo.

Baadhi ya baiskeli zilizokabidhiwa kwa walemavu huko Geita,

Baadhi ya walemavu wakiwa na baiskeli zao mara baada ya waliokabidhiwa.

Vick Kamata akifurahia jambo na mmoja wa wananchi hao wakati alipokabidhi baiskeli za walemavu huko Geita.

Baadhi ya walemavu wakisubiri kukabidhiwa baiskeli na mbunge Vick Kamata.

Mh. Vick Kamata akiteta jambo na mmoja wa wazee wa Geita.

Picha na www.fulshangwe.blogspot.com

Tuesday, January 10, 2012

THIERRY HENRY AIPAISHA ARSENAL FA

Goli pekee lililofungwa na mkongwe aliyerejea Arsenal, Thierry Henry limeipatia timu hiyo ushindi na tiketi ya kusonga mbele kwenye michuano ya Kombe la FA katika mchezo uliopigwa jana dhidi ya Leeds United.

Henry, 34, alifunga goli lake la 227 kwa Arsenal baada ya kurejea kuichezea klabu hiyo kwa mkopo wa miezi miwili.

Arsenal sasa itakutana na Aston Villa katika raundi ya nne ya kombe la FA katika mchezo utakaochezwa Januari 28.


Boss wa The Gunners Wenger anaronga kuwa: "Ndoto imekuwa kweli, ni hadithi ambayo mara zote nimekuwa nikiwaambia vijana kuhusu mchezo wa soka. "Tayari tulikwisha mtawaza kama Legend wa hapa lakini usiku wa leo kaongeza kitu zaidi katika historia yake yote."

"It didn't surprise me that he scored tonight but when he was through on goal I thought his angle was a bit too close. "But he didn't force his shot and still made it look easy. That was the special finishing of Thierry Henry that we all know."

Arsenal wamesonga mbele baada ya kupata ushindi wa bao 1-0.