ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, December 12, 2012

MBIO ZA SERENGETI MARATHON 2012 ZAFANA MKOANI SIMIYU

Mshindi wa kwanza wa Serengeti marathon 2012 Dickson Marwa kutoka mkoani Mara, akihitimisha ukimbiaji mbio za nyika mita 21 zilizofanyika jana kwenye mbuga za Serengeti mkoani Simiyu.

Mashindano hato ya kwanza yamevuka malengo kutoka washiriki 80 waliojiandikisha awali hadi kufikia washiriki 207 waliojitokeza mapema asubuhi kabla ya mbio hizo kuanza kutimua vumbi.

Big up sana kwa Mshiriki mwenye ulemavu wa mkono mmoja Edward Joseph aliyemaliza mbio hizo kwa upande wa wanaume akiwa nafasi ya 14.

Mshindi wa kwanza wa Serengeti marathon 2012 Dickson Marwa kutoka mkoani Mara akiwa ameshikilia medali yake ya dhahabu na fedha kiasi cha shilingi laki 5 alichonyakuwa kwenye mbio za kwanza za nyika za Serengeti Marathon.

Hawa ndiyo washindi kumi wa kumi bora upande wa wanaume ukimbiaji mbio za nyika mita 21 zilizofanyika jana kwenye mbuga za Serengeti mkoani Simiyu, mbele ni mshindi wa kumi akifuatia wa tisa hadi wa kwanza nyuma, wakiwa kwenye mstari kwaajili ya kutunukishwa zawadi zao.

Wakuu mbalimbali waliohudhuria michuano ya kwanza ya Serengeti Marathon.

Mshindi wa kwanza wanawake katika Serengeti marathon 2012 Failuna Mohamed kutoka mkoani Arumeru akiwa ameshikilia medali yake ya dhahabu na fedha kiasi cha shilingi laki 5 alichonyakuwa kwenye mbio za kwanza za nyika za Serengeti Marathon.

Maafisa wanyamapori kutoka mbuga ya hifadhi ya taifa ya Serengeti wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri wakati wa utoaji wa zawadi kwa watimua vumbi wa mbio hizo, hawa ndio waliosimamia zoezi la kuhakikisha barabara ni salama kwa wakimbiaji  ili wasishambuliwe na wanyama wakali.

Dr. Mtiro akitoa Huduma ya Kwanza kwa moja ya washiriki wa mbio hizo mara baada ya kumalizika kwa mashindano. 

Vitita na Medali mezani kabla ya kumilikishwa kwa washindi....

Serebuka ya wafukuza upepo.

Mkuu wa wilaya ya Busega Paul Mzindakaya (katikati) akipata picha ya pamoja na washindi watatu watatu kutoka kwa kila pande, Kutoka kushoto ni Ndege Stephen (Nyamagana Mwanza) aliyeshika No. 3, Said Makula (Arumeru ) aliyeshika No. 2 na Dickson Marwa (Mara) mshindi nafasi ya kwanza, Upande wa pili baada ya mweshimiwa ni mwanadada Failuna Mohamed (Arumeru) aliyeshika nafasi ya kwanza wanawake, Grace Jackson (Bariadi mkoani Simiyu) No. 2 na Neema Mathius (Magu mkoani Mwanza) No. 3. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.