ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 14, 2012

KOFFI OLOMIDE ATUA JIJINI DAR TAYARI KWA MAONESHO YAKE DAR NA MWANZA

Mwanamuziki nyota wa dansi kutoka nchini DRC-Kongo, Koffi Olomide akiwasalimia baadhi ya mashabiki wake waliofika kumlaki usiku huu mara baada ya kuwasili akiwa sambamba na skwadi lake zima la Quartier Latin kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), tayari kwa maonesho yake, la kwanza litafanyika siku ya jumamosi ndani ya viwanja vya Lidaz Club, Kinondoni jijini Dar na jumapili jijini Mwanza ndani ya uwanja wa CCM-Kirumba, Maonesho yote mawili yamedhaminiwa na kampuni ya bia ya Afrika Masharikia (EABL) kupitia kinywaji chake cha Tusker kiingilio kimepangwa kuwa ni shilingi 10,000/= kwa kichwa kama tiketi jijini Dar ikinunuliwa mapema na shilingi 15,000/= getini na kwa jijini Mwanza ni shilingi 5,000/= tu kama zawadi.

Pichani kushoto ni Mwenyeji wake kutoka kampuni ya Prime Time Promotions Ltd, Godfrey Kusaga

Watangazaji wa Clouds FM na Clouds TV pichan shoto ni Millard Ayo na Ben Kinyaiya pichani kulia wakifanya mahojiano mafupi na Mwanamuziki Koffi Olomide mara baada ya kuwasili usiku huu  kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA),jijini Dar. Koffi Olomide alitanabaisha kuwa yeye amekuja nchini Tanzania kwa mara nyingine tena kuwaburudisha na kuwaonesha vipaji alivyo navyo sasa ndani ya kundi lake la Quartier Latin.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.