ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 14, 2012

DIWANI KATA YA KIPAWA AANZISHA MRADI WA KUWASAIDIA WANAWAKE WA KATA YAKE.

Diwani wa Kata ya Kipawa,Bonnah Kaluwa akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kutangaza Uzinduzi wa Mradi wa Kuwaendeleza Wanawake na Wasichana wa Kata ya Kipawa kuwa Wajasiliamali na wanaoelewa biashara na Taaluma zao,unaofahamika kama WANAMA (Wamama na Maendeleo).Kulia ni Afisa Mtendaji wa Kata ya Kipawa,Said Fundi.
Meneja Mauzo wa Kampuni ya Dalring Hair,Edward Shilla (kulia) ambao ni wadhamini wa Mafunzo ya Mradi huo wa WANAMA akizungumzia namna walivyoweza kujitokeza kudhamini Mradi huo utakaowawezesha Wanawake na Wasichana wa Kata ya Kipawa kuwa Wajasiliamali na wanaoelewa biashara na Taaluma zao.Kushoto ni Diwani wa Kata ya Kipawa,Bonnah Kaluwa ambaye ndie Mratibu mkuu wa Mradi.
Afisa Mtendaji wa Kata ya Kipawa,Said Fundi (kushoto) akitoa shukrani kwa wadhamini wa Mradi wa Kuwaendeleza Wanawake na Wasichana wa Kata ya Kipawa kuwa Wajasiliamali na wanaoelewa biashara na Taaluma zao,unaofahamika kama WANAMA (Wamama na Maendeleo) ambao ni Kampuni ya Dalring Hair.Katikati ni Diwani wa Kata ya Kipawa,Bonnah Kaluwa na kulia ni Meneja Mauzo wa Kampuni ya Dalring Hair,Edward Shilla.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.