ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 22, 2012

NAMTAMBULISHA LADY ZHENA…..AWAPA SOMO WANAMUZIKI WA KIKE!!

Wapo wanamuziki wachache wa kike wanaopiga muziki wa kizazi kipya, kwa sasa, lakini kadri siku zinavyokwenda, wanaendelea kuibuka wanamuziki kadhaa wa kike ambao kwa hakika wanajitahidi kuziteka nyoyo za wapenzi wa muziki wa kizazi Kipya.

Mmoja wa wanamuziki hao ambaye ameamua kufunguka na kueleza ya moyoni mara baada ya kuingia rasmi katika tasnia hii ya muziki wa kizazi Kipya ni manamuziki Lady Zhena.

Lady Zhena anaeleza kinagaubaga kuwa ni vyema wanamuziki wa kike nchini kutambua kuwa wanapaswa kuwa na moyo wa uvumilivu nakutokata tamaa mapema kwani hakuna maendeleo ya ghafla na ya haraka.

Wanamuziki wa Kike wanapaswa kutilia maanani mazoezi na kujifunza mbini za muziki zitakazo wawezesha kutunga na kuimba kwa sauti tamu kama wanavyofanya wenzao wanong'ara hapa Afrika.

Anasema Inafaa pia kwa wanamuziki wetu wa kike Kuithamini kazi hiyo kwa kuiona kuwa sawa na zingine, tena isiyopaswa kuchezewa.

Isiwe tu wanapotoka stejini, basi wanajiona na kazi ndiyo imekwisha. Ni vyema pia kwa wanamuziki wa kike kujiheshimu wakati wote.

 Iwapo watajiheshimu wawapo kwenye muziki, ni rahisi pia kwao kuheshimika kwa mashabiki.

Lady Zhena amefunguka na kusema kuwa maendeleo ya wanamuziki wa kike na kung'ara kwao kimuziki kutaamsha hamasa kwa wanawake wengi wenye vipaji kujitokeza badala ya ilivyo hivi sasa ambapo wengi wanasita kwa kuiona fani hiyo ni ya kihuni.






Mwisho Lady Zhena, anaomba
Suport kwa watanzania waipokee kazi yake mpya na kuomba baraka za Watanzaniakuipokea kazi yake mpya na kuomba baraka zao, kwani bila wao yeye si mali kitu.

Single yake mpya aliyoitoa hivi karibuni katika Audio na Video amemshirikisha B-Baros imeanza kufanya vizuri kwenye radio na televisheni nyingi hapa nchini ikienda kwa jina 'Niliteleza' chini ya usimamizi wa Brabe Entertainment.




Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.