ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 22, 2012

MKUU WA MKOA WA MWANZA AWAKABIDHI BENDERA YA TANZANIA KILIMANJARO STARS USIKU HUU

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo (R) akimkabidhi bendera ya Taifa Nahodha wa timu ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars Juma Kaseja kwenye hafla fupi iliyofanyika usiku huu ndani ya Hotel Lakairo jijini Mwanza tayari kwa safari kuelekea nchini Uganda michuano ya Chalenji inakayoanza kutimua vumbi 24 nov 2012 nchini humo, huku ikiwakosa wachezaji wake, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu, Hata hivyo licha ya wachezaji hao kutowasili hadi jana, viongozi wa timu hiyo wanaamini kuwa wataungana na wachezaji hao. Katikati anaonekana kocha mkuu wa timu hiyo  Kim Poulsen.


Mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo akiwaasa wachezaji wa timu ya taifa Tanzania Bara Kilimanjaro Stars, ambapo kubwa zaidi kutoka kwake amewasisitiza  wachezaji hao kuweka fikra zote kwenye kila mchezo kwa dakika 90 pamoja na nidhamu ndani na nje ya uwanja.


Kilimanjaro Stars, inayonolewa na kocha wake Kim Poulsen, iliweka kambi jijini Mwanza kwa siku kadhaa, kabla ya kesho alfajiri kuondoka Mwanza na kuunganisha ndege katika Uwanja wa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam.


Licha ya kocha mkuu wa timu hiyo Kim Poulsen kuahidi mazuri kwa watanzania pia amesema kuwa morari itaongezeka kwenye timu yake iwapo Watanzania watajitokeza kwa wingi kuisapoti timu yao ya Taifa, katika michezo yake yote na kustaajabisha wenyeji kwa ubunifu namna ya ushangiliaji.


Meza kuu...


 Meya wa jiji la Mwanza (Nyamagana) Stanslaus Mabula (R) akiteta na Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela Henry Matata (L) kwenye hafla fupi iliyofanyika usiku huu ndani ya Hotel Lakairo jijini Mwanza tayari kwa safari kuelekea nchini Uganda michuano ya Chalenji inakayoanza kutimua vumbi 24 nov 2012 mjini Kampala.


Mkuu wa wilaya ya ilemela Bi. Amina Masenza (L) akiteta jambo na Katibu tawala wa Mkoa wa Mwanza (RAS) Bi. Doroth Mwanyika, kwenye hafla fupi iliyofanyika usiku huu ndani ya Hotel Lakairo jijini Mwanza tayari kwa safari kuelekea nchini Uganda michuano ya Chalenji inakayoanza kutimua vumbi 24 nov 2012 mjini Kampala.


Afisa habari wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mr. Kuni Atley (R) akiwa na kocha mkuu wa Kilimanjaro Stars,  Kim Poulsen (L).


M-blogishaji maarufu wa The big top ten Muhksin Mambo (R) akiwa na kocha mkuu wa Kilimanjaro Stars,  Kim Poulsen (L).


CEO wa Blogu hii Albert G. Sengo (R) akiwa na kocha mkuu wa Kilimanjaro Stars,  Kim Poulsen (L).


Kila la kheri Kilimanjaro Stars. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.