ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, August 10, 2012

AIRTEL TANZANIA YAPELEKA NYOTA WAKE MICHUANO YA AIRTEL RISING STARS AFRICA.

Afisa Habari wa Kampuni ya Airtel Tanzania Jane Matinde(kulia)akizungumza na waadishi wa habari wakati wa kutangaza kikosi cha timu ya soka cha Airtel Rising Stars kitakachoshiriki michuano ya Inter-continental yatakayofanyika Nairobi, Kenya mwezi  huu. Amefuatana na Meneja Uhusiano wa kampuni hiyo Jackson Mmbando(kulia)

Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Airtel Tanzania Jackson Mmbando(kulia) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kutangaza kikosi cha timu ya Airtel Rising Stars kinachokwenda kushiriki michuano ya Inter-continental itakayofanyika Nairobi, Kenya baadaye mwezi huu. KAtikati ni Afisa Habari wa kampuni hiyo Jane Matinde na Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam(DRFA).


Taarifa kwa Vyombo vya Habari 
Airtel yapeleka Kikosi cha wachezaji nyota wa Airtel Rising Stars Nairobi Timu ya Yoso bora 16 kuwakilisha Tanzania kwenye michuano ya Airtel Rising Stars  Afrika, Airtel Tanzania kupitia mpango wake maalum wakuvumbua na kukuza vipaji vya soka nchini ujulikanao kama Airtel Rising Stars leo wametangaza kikosi cha wachezaji 16 watakaoiwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya kimataifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel yatakayofanyika Nairobi kuanzia Agosti 19 hadi 25, 2012.

Wachezaji hao walichaguliwa na jopo la makocha kwa kushirikiana na shirikisho la mpira TFF na chama cha mpira cha Dar es Saalam DRFA wakati wa fainali za Taifa za Airtel Rising Stars zilizofanyika kwenye uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam mwezi Juni na kushirikisha timu kutoka mikoa ya Lindi, Mbeya, Arusha, Ilala, Temeke na Kinondoni.


Akiongea na waandishi wa habari katika ofisi za TFF leo, Afisa Maendeleo wa mpira wa miguu nchini Salum Madadi aliwataja vijana watakaowakilisha Tanzania kuwa ni Denis Richard, Juma Hamza, Abdul Selemani, Ishaka Shekolowa na Bakari Ally kutoka mkoa wa kisoka wa Temeke.


Wengine ni Abdulatif Mohamed, George Joseph na Badilu Said (Lindi), Said Kassim, Amos Ikungula, Paul Balama na Goodluck Mabiku (Ilala), Joel Kasimula na Ibrahim Mtenga (Mbeya), Sntkony Angelo na Suleiman Yunus (Arusha).


Mashindano hayo yanayotarajiwa kuwa na ushindani mkali yatashirikisha wachezaji wengine nyota wa ARS kutoka nchi za Kenya, Uganda, Malawi, DRC, Congo Brazzaville, Nigeria, Ghana, Zambia, Niger, Gabon, Burkina Fasso, Sierra Leone, Chad, Madagascar na Tanzania.


Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano Mallya amesema kuwa lengo la mashindano hayo ya kimataifa ni kuwapa vijana fursa zaidi ya kuendeleza vipaji vyao na kupata uzoefu. "Vile vile Airtel Rising Stars inatoa nafasi kwa wanasoka hawa chipukizi kuweza kupanua jiografia yao na kujenga urafiki na vijana wenzao kutoka nchi mbali mbali", alisema Singano.


Michuano hiyo itafuatiwa na kliniki ya soka ya kimataifa ambayo pia itafanyika Nairobi chini ya walimu wa soka la vijana kutoka klabu maarufu duniani ya Manchester United ya Uingereza. Kliniki kama hii ilifanyika mwaka jana kwenye uwanja wa kisasa wa soka jijini Dar es Salaam na kushirikisha vijana kutoka Kenya, Malawi, Sierra Leone na wenyeji Tanzania.


Katika kliniki ya mwaka huu, Tanzania itawakilishwa na wachezaji sita miongoni mwao ni wavulana watatu na wasichana watatu ambao walioibuka kuwa wachezaji bora wakati wa fainali za Taifa jijini Dar es Salaam mwezi Juni.


Airtel Rising Stars ni mpango kabambe wa kuibua na kukuza vipaji vya wanasoka wanaochipukia barani Afrika. Walengwa ni wavulana na wasichana wenye umri chini ya miaka kumi na saba ambao watapata fursa ya pekee ya kuonyesha vipaji vyao mbele ya waatalum wa mpira wa miguu wa kitaifa na kimataifa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.