ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 16, 2012

MPC WACHAGUA SURA MPYA 2012

Akitangaza matokeo  Mwenyekiti wa uchaguzi huo bw. Robert Mkosamali (aliyesimama pichani) nafasi ya za Wajumbe watano wa kamati ya Utendaji zimekwenda kwa Rose Jackob na Grace Chilongola waliopita bila kupigiwa kura, wengine ni George Ramadhani, Atley Kuni na Kelvin Jilala.


Hivi ndivyo ilivyokuwa wakati wa zoezi la uhesabu kura.

Nafasi ya Mweka hazina imekwenda kwa Fred Katulanda aliyepata kura 28 aliyewaangusha Paulina David aliyepata kura 25 na Clara Matimo aliyeambulia kura 1.

Makamu Katibu mkuu imetwaliwa na bi Sheila Sezy aliyepita kwa kura za NDIYO 39 na HAPANA 14.

Nafasi ya Katibu Mkuu imekwenda kwa Jimmy Luhende aliyepata kura 27 akiwashinda Felista Kulijila kura 22 na Nashon Kenedy aliyeambulia kura 7.

Nafasi ya Makamu Mwenyekiti imeenda kwa Flora Magabe aliyepata 29 dhidi ya wapinzani wake Rahabu Fred kwa kupata kura 27, ambaye hata hivyo hakuwepo uchaguzini kwenye mkutano huo  kutokana na kuwa na udhuru.


Mwisho nafasi nyeti ya Uwenyekiti ilinyakuliwa kwa kishindo naye Deus Bugaiwa aliyetikisa kwa ushindi wa kishindo kwa kuzoa kura 41  dhidi ya Osoro Nyawangah aliyepata kura 15 za wanachama walioshiriki uchaguzi huo. 


 Wadau wa habari katika moja ya meza za majukumu mkutanoni humo.

 Wanachama mkutanoni.

 Hapa wanachama walikuwa wakijinadi kupata ridhaa ya wadau kuwania nafasi tano za Ujumbe.
  

Wanachama wakifuatilia mkutano wa mwaka 2012.

Tupe maoni yako

1 comments:

  1. Kuna sura mpya hapa? Ni kubadilishana viti ili kuweka sawa ulaji!

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.