ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, May 16, 2012

RC MWANZA AWATAKA MA DC KUPAMBANA NA UFISADI WA FEDHA ZA UMMA KWENYE HALMASHAURI ZAO

Mkuu mpya wa wilaya ya Magu Jaqueline Liana akila kiapo mbele ya mkuu wa Mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo leo katika viwanja vya ofisi ya mkuu wa Mkoa.

Mkuu wa wilaya wa Kwimba Selemani Mzee Selemani akila kiapo cha utumishi mbele ya mkuu wa Mkoa wa Mwanza huku akishuhudiwa na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa.

Mkuu wa wilaya ya Ilemela Amina Masenza akila kiapo cha utumishi kwa mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo huku akishuhudiwa na Katibu Tawala mkoa Doroth Mwanyika.

Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga akila kiapo cha utumishi mbele ya mkuu wa mkoa wa Mwanza katika hafla fupi ya kuwaapisha wakuu wapya saba wa wilaya za mkoa wa Mwanza uliofanyika leo.

Mkuu wa wilaya ya Misungwi wa zamani Mariam Lugaila akila kiapo mbele ya mkuu wa mkoa wa Mwanza baada ya kuteuliwa tena kuwa mkuu wa wilaya hiyo.

Mkuu wa wilaya ya Ukerewe Mary Tesha akila kiapo mbele ya mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo.

Mkuu wa wilaya ya Sengerema Karen Yunus akila kiapo cha utumishi wa umma.

Wanahabari nao hawakuwa nyuma kuwajibika katika tukio zima la kuapishwa wakuu wapya wa wilaya saba za mkoa wa Mwanza walioteuliwa hivi karibuni ambapo leo wameapishwa rasmi.
Picha ya pamoja ya wakuu wa wapya wilaya walioapishwa na viongozi waalikwa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.