ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, May 12, 2012

TANZANIA DMV KUCHUANA NA ETHIOPIA KUNDI (B)

Na Abou Shatry
Katika mchezo wa lingi ya 2011 Diaspora World Cup zinazoendelea katika viwanja vya Hyattsville na Germantown jijini Maryland Nchini Marekani, timu ya Tanzania DMV watachuwana vikali na timu ya Ethiopia Leo hii Jumamosi May 12, 2012 mida ya 12:PM (Mchana wa saa sita) katika kiwanja cha Greencastle, kiliopo Burtonsville, Maryland
TANZANIA DVN

ETHIOPIA
Kundi (B) Timu ya wa Ethiopia katika mchezo wa awali walifungwa bao 3-0 na timu ya Malawi ndani ya uwanja cha Greencastle, Burtonsville, Maryland, ambao leo watajianda vikali ili kutaka kurudisha nguvu zao kwa mchezo waliopoteza dhiti ya timu hiyo ya Malawi, ambao leo hii timu ya Malawi watapambana vikali na timu ya Armenia mida ya saa 1:PM Mchana wa leo, kwa mechi ya kwanza timu ya Armenia waliwabamiza Nigeria bao 4-1 katika mchezo wa awali.

Pia timu ya waTanzania DMV katika mchezo wa kwanza siku ya Jumapili ya April 29,2012 walifanikiwa kuwabamiza timu ya Ghana bao 3-2 ndani ya uwanja wa SoccerPlex Stadium uliopo Ager Road Hyattsville Maryland.

Kama kawaida yao timu ya waTanzania DMV inawaomba Watanzania wote ushirikiano wenu wa kila hali ili kuipa changamoto timu ya Watanzania DMV, mnaombwa pia kufika mapema mida ya saa 11:AM kuzowea mazingira kabla ya mchezo huo kuanza. 
Adress ya mchezo utakaochezwa leo hii ni Fairland Field 3928 Greencastle Rd. Burtonsville, Maryland 20866 Habari na http://swahilivilla.blogspot.com/

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.