ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, May 12, 2012

MWANZA KWANZA YAMTEKA KALA JEREMIAH

Kala Jeremiah(L) katika flash na mwenyekiti wa Mwanza kwanza Philbert Kabago(R).
Katika hatua nyingine Umoja wa wasanii na watu wa Mwanza (Mwanza kwanza) umefanikiwa kuziteka hisia na hatimaye kumwingiza kundini msanii wa hip hop nchini kinara aliyetikisa BSS, Kala Jeremiah.

Akizungumza na blogu hii Kala Jeremiah amzitaja kwa kifupi sababu za kujiunga na Umoja huo kuwa kwanza ni sifa yakuwa mzawa wa moja ya vitaa vya jiji hilo la miamba, pili akiamini kuwa Umoja ni nguvu amefurahishwa na kuvutiwa na misingi iliyopo ndani ya umoja huo sanjari na msimamo pamoja na mshikamano uliopo.

Mwanza kwanza imeendelea kuteka fani mbalimbali kama vile Waigiza filamu, Watayarishaji wa muziki, Ma-Dj, Watangazaji, Waimbaji Muziki wa injili na Muziki wa kizazi kipya akiwemo Dudu Baya, Sajna, Sisar Madini na wengine wengi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.