ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 10, 2012

LOWASA AMPONGEZA KIDUNDA AKIWA DUBAI

KATIBU wa shirikisho la ngumi za Ridhaa nchini BFT Makore Mashaga pamoja na makocha na viongozi wa BFT kwa pamoja wamempongeza bondia Selemani kidunda kwa kuteuliwa kushiriki mashindano ya Olimpiki yanayotarajia kufanyika hivi karibuni akizungumza katika hafla hiyo ya kumpongeza na kumtia moyo kuendelea na mazoezi kwa ajili ya michunano ya olipiki inayokuja karibuni.

Aidha Makamu mwenyeki wa BFT Michael Changalawe amemshukuru Waziri Mkuu Mstaafu Eduward Lowasa kwa kumpatia Kidunda Dola 100 baada ya kukutana Dubai wakati wanarudi Tanzania kambi ya ngumi inaingia kambini leo hii tarehe 10 katika uwanja wa ndani wa taifa kwa ajili ya mazoezi zaidi.

Mbali na mashindano hayo timu hiyo imeomba wafadhili mbalimbali kujitokeza kwa ajili ya kuipa sapoti kampeni hiyo ambapo wanatarajia kwenda botswana kwa ajili ya kuweka kambi ya bondia Kidunda na wengine kupima Viwango vyao.

Timu hiyo inakabiliwa na uhaba wa fedha hivyo wametoa wito kwa watu binafsi, mashirika pamoja na makampuni kujitokeza kusaidia mchezo wa masumbwi ili uweze kusonga mbele.

Kwa sasa kambi hiyo itakuwa na mabondia kumi kila uzito.
Na:Super D Boxing Coach

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.