ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, April 2, 2012

CHEZEA TWANGA WEYE....!!!!

Ziara ya Twanga Pepeta kanda ya ziwa imedhihirisha kuwa bendi hiyo bado ni mahiri linapokuja suala la kuwa na mashabiki wengi. Kwa mujibu ya wakuu wa kumbi mbalimbali za burudani ambao hutumiwa na www.gsengo.blogspot.com kwa shughuli mbalimbali za burudani kila mmoja amekiri kupata faida kupitia ziara ya Bendi hiyo. Ukianzia Villa Park Mwanza ambapo kamera yetu ilikuwa pale, Musoma mkoani Mara na hata katika wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga kwa show iliyofanyika jana Club Dimpoz.
Dogo Rama akisalimia watu wake wa nyumbani.

Mmoja kati ya mashabiki aliyejitambulisha kwa jina moja tu Selemani, amesema kuwa hata fitina gani ziwaandame hawa jamaa watabaki kuwa juu kwani kama Uongozi wanao, jina wanalo, mashabiki wanao vizazi hadi vizazi kuanzia watu wazima, wazee, wanaume kwa wanawake vijana hadi watoto.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.