ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, March 7, 2012

SAYANSI NA TEKNOLOJIA YA KESHO ?

MAAJABU YA ULIMWENGU!
*Fahamu mikasa na vituko mbalimbali wanavyofanya baadhi ya wenye nyumba na wapangaji wa hapa Tanzania kwenye nyumba za kupanga, kwa kusoma hadithi yenye vituko vilivyotokea kwenye baadhi ya nyumba: HASIRA ZA MPANGAJI(HM).

*Fahamu pia jitihada mbalimbali wanazofanya wanasayansi wa nchi za magharibi katika kutafiti viumbe hai nje ya dunia (extraterrestrial life). NASA (National Aeronautics and Space Administration) yenye makao makuu yake Marekani, kwa kupitia projekti yao ya SETI, wanatafiti uwezekano wa kuwa na viumbe wenye akili na utashi kama binadamu wa hapa duniani. Viumbe vinavyosadikiwa kuishi kwenye sayari zilizo nje ya mfumo wa jua, kama vile sayari za Kepler-22b, GJ 1214b na Gliese 581d. (Mwanga {300,000km/s} huchukua miaka 20, kusafiri toka duniani hadi sayari ya Gliese 581d).

Utafiti huo hautaleta uhalisia kama utafanyika huku watafiti wakiwa duniani tu. Hivyo, wamejenga maabara yao huko nje ya dunia(International Space Station au ISS). Ipo kwenye kiwanja kinachoelea hewani!.

Wazo la kujenga maabara hiyo ya aina yake liliibuliwa mwaka 1869, baada ya mwandishi wa ki Amerika(Edward Everett Hale) wa hadithi ya kisayansi iitwayo “Brick Moon”, kuchapisha hadithi hiyo. Malighafi ya kwanza ya kujengea ISS ilipelekwa kwenye kiwanja hicho novemba 1998.Roketi ya Kirusi ilifanya kazi hiyo.Malighafi nyingi zaidi ziliongezwa kwa miaka miwili iliyofuata. Mpaka kufikia mwaka 2000, tayari jengo hilo lilifaa kwa watu kuishi ndani yake. Hivyo kikosi cha kwanza cha wana utafiti kilitua (docking) kwenye jengo hilo mwezi octoba, 2000.

Mwezi Julai mwaka jana (2011), NASA walikwenda ISS kwa kutumia usafiri maalumu,ATLANTIS. Mwishoni mwa mwaka jana, Warusi nao wakajitosa huko kwa kutumia SOYUZ.Na hivyo, kuhitimisha ukarabati wa nyumba hiyo inayoizunguka dunia kila baada ya dakika 90. ISS ina mabafu mawili na sehemu ya michezo(GYM). Jengo hilo la kiunajimu, ni kubwa kama nyumba ya vyumba vitano.

Ni changamoto gani wanakutana nazo?. Kwa nini jengo hilo linaelea?. Wanazigunduaje sayari mpya?. Kwa nini wanahatarisha maisha yao na kuteketeza mabilioni ya fedha ili kuwekeza kwenye utafiti huo?.Wataalamu mbali mbali duniani,wanasemaje juu ya utafiti huo?. Usiachwe nyuma, kimbia pamoja na maendeleo ya sayansi na teknolojia kwa kusoma riwaya ya HASIRA ZA MPANGAJI, uhabarike, uburudike na kujiongezea maarifa ya mtindo huo.

*Waandalie watoto mazingira mazuri ya kuipenda sayansi na teknolojia kwa kuwazawadia riwaya ya kisayansi: HASIRA ZA MPANGAJI.
*Kwa wapenzi wa kutalii,usikubali kutalii ndani ya dunia tu, ungana na mwandishi wa HASIRA ZA MPANGAJI usafiri kwenda nje ya dunia, uitalii jiografia, sayansi na maisha ya watu wa huko.
Kwa kanda ya ziwa, HASIRA ZA MPANGAJI inapatikana kwa Tshs 3500/= tu kwa wauza magazeti na vitabu walio maeneo yafuatayo;
<>MWANZA MJINI(PPF PLAZA,MAKOROBOI,SOKONI,TANESC O,KAMANGA FERRY,0764331568,0755734574)-Pia inapatikana kwenye VICTORIA BOOKSHOP. (BURUDIKA!: BAADA YA MIAKA 1200 TOKA SASA, TEKNOLOJIA YAWEZA KUFIKIA WAPI?,JIBU=HM)

<>KAKOLA (0764361519), KAHAMA (0753574124), MUSOMA- KAMISA(0755004410), BUKOBA (0713918505, 0754552485), BUNDA(0655282034), TARIME(0765649612), SHINYANGA (0755873500),GEITA(0759419303) , SENGEREMA(0753982040, 0769359373).
NA HIVI KARIBUNI, ITATUA DAR ES SALAAM.

Tujadiliane kupitia riwaya za kisayansi na kiteknolojia!.

Tupe maoni yako

2 comments:

Note: Only a member of this blog may post a comment.