ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 9, 2012

UWF YAMTWAA MAMA MJASIRIAMALI ANAYEFUATA NYAYO ZA MWANAMAKUKA 2012

Pichani shoto ni Meneja matukio na Udhamini wa benki ya NBC,Rachel Remona akimkabidhi Mwanamke Mjasiliamali aliyeibuka na tuzo ya Mwanakuka,Bi.Tatu Mwenda mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni sita. Pichani kati kulia ni Mwenyekiti wa UWF (waandaji wa tuzo hiyo ya Mwanamakuka),Bi.Mwate Madinda sambamba na Mtangazaji wa kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM, Dina Marios wakishuhudia tukio hilo adhimu kabisa, katika kuadhimisha siku ya Mwanamke Duniani, iliyofanyika leo,Hafla hiyo imefanyika usiku huu ndani ya hotel ya Serena, jijini Dar na kuhudhuriwa na watu mbalimbali.

Pichani kushoto ni Meneja matukio na Udhamini wa benki ya NBC, Rachel Remona akimkabidhi mshindi wa pili wa tuzo ya Mwanamakuka, Bi. Mwanne Msekalile mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni mbili. Pichani kati kulia ni Mwenyekiti wa UWF (waandaji wa tuzo hiyo ya Mwanamakuka), Bi. Mwate Madinda sambamba na Mtangazaji wa kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM, Dina Marios wakishuhudia tukio hilo adhimu kabisa, katika kuadhimisha siku ya Mwanamke Duniani, iliyofanyika leo, Hafla hiyo imefanyika usiku huu ndani ya hotel ya Serena, jijini Dar na kuhudhuriwa na watu mbalimbali.

Meneja matukio na Udhamini wa benki ya NBC, Rachel Remona akimkabidhi mshindi wa tatu wa tuzo ya Mwanamakuka, Dada Sikudhani Daudi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni moja na laki tano.

Mshindi wa tuzo ya mwanamke mjasiriamali ya Mwanamakuka, Bi. Tatu Mwenda akiwa katika picha ya pamoja na wanachama wa UWF huku akiwapungia mkono wageni waalikwa mbalimbali (hawapo pichani) waliofika kwenye hafla hiyo iliyofana kwa kiasi kikubwa.

BIG UP WADAU.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.