ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, March 6, 2012

KAZI YA POLISI TABORA

Hassani akikanyagwa na askari wa jeshi la polisi Tabora.
From DEBORAH MPAGAMA,
Urambo Tabora.

Hivi karibuni nilikuwa katika wilaya ya urambo mkoani Tabora ambapo kijana mmoja aitwae Hassan Mgalu akiwa katika soko la wilaya hiyo aligongwa na baiskeli na aliye mgonga alikuwa askari aliyevaa nguo za kiraia baada ya Hassani kugongwa na askari huyo hali ilikuwa hivi:-

Hassani; kwanini umenigonga ?
Askari ; kwanini unataka nini?
Hassani; yani unanigonga na baiskeli na unasema nataka nini?

Hassani akampiga kibao askari huyo ambaye alikuwa amevaa nguo za kiraia, kufatia hali hiyo askari huyo aliondoka na kuwafata wenzie ambao walikuwa na nguo za kirai na walimkuta Hassani akicheza pull katika eneo la standi ya zamani wilayani humo, mmmmh, wamshushia kipigo cha hali ya juu na kumvuta kwa moja kushika mguu wa kulia na mwingine mguu wa kushoto kichwa kikijibuluza chini umbali wa mita 2000 mpaka karibu na ofisi ya ushirika ya urambo na benki ya NMB ambapo walimtupia katika bajaji hiyo ambayo unaiyona hapo katika picha mmoja akiwa amemkanyaga kichwa chake.

Kutokana na mateso makali aliyoyapata hassani alipoteza maisha , katika jalada lililofunguliwa kwenye kituo cha polisi urambo maelezo yaliandikwa amepigwa na wananchi wenye hasira jambo ambalo si kweli na lilileta utata kati ya wanafamila na wananchi wa eneo hilo ,ni meeandika haya ili upate picha.

Je askari anahaki ya kumpiga raia, manyanyaso haya ya raia kwa kutofahamu sheria mpaka lini, umegongwa na baiskeli, unapigwa na hata kutolewa uhai wako tutafika?

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.