ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 8, 2012

BREAKING NEWS: DALADALA YAUWA WANAFUNZI WAWILI ENEO LA BUGANDO MWANZA

Leo majira ya saa nne asubuhi katika barabara ya kuelekea Hospitali ya Bugando imetokea ajali mbaya ya basi dogo la abiria (daladala) iliyokosa uelekeo na kusababisha vifo vya watoto wawili.Askari wa jeshi la polisi wakiondoa vizui vya mawe njiani barabara ya keuelekea Huspitali ya Bugando jijini Mwanza.

Mchoro wa ajali.
"Hii gari ilikuwa inatiokea Bugarika inashuka kuelekea mjini, kwa spidi aliyokuwa nayo dereva kwa kweli ilikuwa hairidhishi kwani gari liliyumba kabla ya kufika eneo la Bar ya Bugando Hill, imagine sisi tulikuwa pembeni ya barabara lakini kwa hofu tukalipisha tukakaa pembeni kabisaa. Lilipofika karibu na Shule ya msingi Bugando dereva wa gari kona ikawa kama imemshinda akakwepa akaenda kugonga nguzo ya umeme akawa anahangaika kurudi barabarani eneo ambako kuna kama kivuko kwa wanafunzi ikamshinda na kupitia watoto wawili waliokuwa wakisubiri kuvuka barabara kisha akagota kwenye mawe yaliyopangwa pembezoni" alisema Joseph Nyanda Karumbeti almaarufu kwa jina Baba Teresa, shuhuda wa ajali hiyo.

Mtoto Elizabeth Kamsoka mwanafunzi wa darasa la 7 shule ya Msingi Sahara alifariki dunia papo hapo katika eneo la ajali mara baada ya kupasuka kichwa mazingira yanayotisha, nae Baraka Revocatus mwanafunzi wa darasa la 4 shule ya msingi Bugando amefariki dunia akiwa Hospitali ya Rufaa Bugando wakati juhudi za madaktari kuokoa maisha yake zilipogonga mwamba.

Licha ya gari hili kuwa na mgonjwa aliyekuwa amezidiwa wananchi hawakutoa nafasi lipate pita.

Askari usalama barabarani akihusika na mchoro wa ajali hiyo iliyosababishwa na daladala ambapo dereva wake mara baada ya ajali alikimbia kusikojulikana.

TUNAOMBA RADHI KWA PICHA ZIFUATAZO
Haya ni mabaki ya vipande vya fuvu la mtoto Elizabeth, blogu hii inaomba radhi kwa picha hii.

Ilikuwa ni hali ya kutisha blogu hii inaomba radhi kwa picha hii ya masalia ya ubongo wa marehemu eneo la ajali.

Kwa muda wa takribani saa nzima barabara hiyo haikupitika kwani mara baada ya ajali hiyo kutokea kundi la watu wanaoishi maeneo hayo walijitokeza na kufunga barabara kwa kuweka mawe makubwa hali iliyosababisa ugumu wa huduma za usariri kwa magari ya wagonjwa na abiria wanao toka au kuelekea Hospitali ya Bugando kupata huduma.

Nguzo iliyogongwa.
Baadhi ya abiria waliopata majeraha kwenye daladala iliyosababisha ajali wamepelekwa hospitali ya Bugando kupatiwa matibabu.

Mwenyezi Mungu zilaze pema peponi roho za marehemu.
Amen.

Tupe maoni yako

5 comments:

  1. inasikitisha sana kwa madereva wetu kukosa umakini nani alaumiwe ni jeshi la polisi kutowajibika ipaswavyo wao wamegeuza magari hayo mabovu kuwa mtaji kuyaacha yafanye kazi.

    ReplyDelete
  2. Magari ya Bugarika yote vimeo tunategemea nini sasa?

    ReplyDelete
  3. Nimeiona kupitia star tv jana usiku nimeogopa kweli hata kutumia usafiri wangu leo kazini nimmeamuakupanda tax.

    ReplyDelete
  4. Kuhusu suala la dereva abanwe mwajiri wake atapatikana tu.
    Ewe Mola tunusuru waja wako zilaze pema roho za marehemu.

    ReplyDelete
  5. Sasa ao waliweka mawe huku ambulance yenye mgonjwa ikipaswa kupita kuwahisha mgonjwa ni akili au matope busara ni kuzuia magari ya huduma za hawaida na si magari yenye wagonjwa hata ivo nimeumia sana kwa tukio la ajali pole kwa familia zilizopoteza watoto wao ongera jisengo kwa habari.

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.