ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, March 12, 2012

BIDHAA FEKI ZINAVYOZIDI KUMWONGEZEA UMASIKINI MTANZANIA

SI KATIKA MADAWA, CHAKULA, VIFAA, BIDHAA MBALIMBALI WALA HUDUMA ZA USAFIRI NA UMEME TUSIPOKUWA MAKINI TUTAKWISHALeo Jijini Mwanza kwenye uwanja wa Makongoro kuna maonyesho ya Siku ya mtumiaji (mlaji)kujifunza jinsi ya kung'amua bidhaa feki ili kutumia bidhaa zenye ubora unaokidhi viwango.

Chunguza mjomba kabla hujaliwa... Bidhaa inayotambulishwa kwenye box jina lake ni tofauti na jina la bidhaa ndani ya box.

Kisha Soma kwa makini jina la bidhaa jeh linaandikwa hivi (SUMSNUG)?

"Ndiyo maana mbu hawafi..." says Katu, Wandishi wa habari wakishirikiana kung'amua bidhaa feki kwa dawa ya mbu ya Rungu, kutoka kushoto ni Emmanuel Chacha wa ITV, Fredrick Katulanda wa gazeti la Mwananchi na Mpiga picha wa ITV Steward Duguda.

Sambamba na mapungufu mengi katika bidhaa feki ikiwa ni pamoja na dawa kutokuwa na uwezo wa kuangamiza wadudu kama ilivyo kwa bidhaa halisi, bidhaa feki utaigundua kwa maandishi yake kupishana, baadhi ya maneno au herufi kuachwa au kuongezwa katika jina au nembo ya bidhaa. Fuatilia mfano ufuatao:-
a - hakuna jina la mzalishaji ktk bidhaa feki.
b - kuna jina la mzalishaji ktk bidhaa halali.


Kwa karibu zaidi.

Ufungashaji wa bidhaa huwa siyo bora ukilinganishwa na ule wa bidhaa halisi.

Haki na wajibu wa mlaji.

Maadhimisho haya ambayo kwa mwaka huu kitaifa yanafanyika mkoani Mwanza yanafanywa kwa harakati mbalimbali ikiwa ni pamoja na maonyesho na kauli mbiu yanataraji kufikia kilele chake tarehe 15/03/2012 chini ya kauli mbiu 'FEDHA ZETU HAKI YETU' ikiwa ni kampeni kuwasaidia wananchi katika kupata huduma bora za kifedha.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.