ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, February 16, 2012

TOTO YACHARAZWA 2-0 DIMBA LA NYUMBANI

Timu ya soka ya Toto ya jijini Mwanza leo hii ikiwa nyumbani katika dimba lake la CCM Kirumba imezididi kujichimbia kaburi mara baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-0 dhidi ya Mtibwa Sugar.Choki Abeid ambaye ni Kocha wa timu hiyo inayoshiriki ligi kuu Tanzania bara kwa kusuasua kutokana na ukata unaoiandama kiasi cha wachezaji wake kucheza kwa kujitolea yaani bila mishahara amesema kuwa sababu za timu yake kupoteza mchezo huo muhimu ni wachezaji wake kukosa umakini na maandalizi mabovu lakini hata hivyo kocha huyo ana matumaini kuwa iwapo wadau watasikiliza kilio chao mambo yatabadilika na kujitengenezea mazingira mazuri kubaki ligi kuu.

Kwa upande wa Mtibwa Sugar timu ambayo ilianza msimu wa pili ligi kuu kwa kichapo kocha wake msaidizi Patrick Mwangata anapinga timu yake kupata ushindi kwa kutegemea timu vibonde akisema kuwa Mtibwa ni moja kati ya timu zenye ushindani ligi kuu na hata matokeo katika msimamo wa ligi kuu zilizopita timu hiyo imekuwa ndani ya top four.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.