ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 22, 2011

ARUSHA KIDEDEA KATIKA VODACOM MWANZA CYCLE CHALLENGE 2011.

Picha kulia ni mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Kanda ya ziwa Steven Kingu sambamba na mkuu wa udhamini Vodacom Tanzania George Rwehumbiza wakimkabidhi Mshindi wa kwanza wanaume Richard Laizer kutoka Arusha zawadi ya kitita cha shilingi milioni 1.5 baada ya kuwashinda washiriki wengine 400 kwenye mbio za baiskeli za Vodacom Mwanza Cycle challenge iliyomalizika leo jijini Mwanza na kudhaminiwa na Vodacom sambamba na SBL kupitia Malta Guinness na Redio Clouds.

Mshindi wa pili Mindi Mwangi kutoka mkoani Shinyanga aliyekuwa akitumia baiskeli ya kawaida tu hapa akipokea kitita chake.

Mshindi wa kwanza mbio za baiskeli wanawake kilomita 80 Sophia Husein akipokea kitita cha shilingi milioni moja toka kwa wadhamini.

Mkurugenzi wa Masoko Kampuni ya Bia ya Serengeti SBL bw. Ephraim Mafuru akikabidhi zawadi kwa Zavalina Abel aliyeshiriki mbio za kilomita 10 zilizomalizikia katika vilima vya Bugando na hafla ya kukabidhi zawadi kufanyika uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.

Si mnaona jamaniiii!!

Washiriki katika pozi.

Mkurugenzi wa Masoko Kampuni ya Bia ya Serengeti SBL bw. Ephraim Mafuru kwa upande wake ametoa pongezi kwa chama cha baiskeli kanda ya ziwa kwa kazi kubwa ya kufanya mapinduzi kwenye mashindano hayo ya sita, kuyapendezesha na kuwa na mwonekano wa kitaifa zaidi.

Washiriki mbio tofauti katika pozi wakisikiliza yanayojiri.

Mashindano yalikuwa na kila sifa za kuvutia, vuta hisia kilomita 196 kwa baiskeli...Duh!!

Haaooo darajani...

Ajali nazo zimo hapa ziligongana kama baiskeli saba hivi....kisa utelezi wa ganda la ndizi.

Mtu kule baiskeli kule...!!

Pamoja na walume hawa kutumia baiskeli hizi za teknolojia hawakufua dafu... mbele ya washosha ng'ombe wazee wa shy.

Akitumia baiskeli isiyo na teknolojia (mfupa) mzeiya wa Shy akiovateki tena kwenye kilima...

Balaaa mwanawane, mzee mzima huyoooo....

Kulia mtu, kushoto mtu hapa ni kazi tu..

Hapa jeh!!

Kote tambarare, shughuli ilikuwa ni kukimaliza kilele cha Bugando...

"Isiwe tabu sheria si zinaruhusu, kwenye kilima to finito ... naikokota"


Kutoka kushoto ni Bukuku wa blogu maarufu ya Full Shangwe, Brand Manager wa Malta Guinness bw. Maurice Njowoka, Butunga wa TBC, Blogger maarufu Michuzi Jr na G.Sengo.

CHADEMA


Friday, October 21, 2011

MZOZO JUU YA MAZISHI YA GADDAFI.

Mazishi ya Kanali Gaddafi yamesitishwa kutokana na tofauti zilizozuka baina ya maafisa wa Libya kuhusu jinsi ya kufanya maziko hayo.
Chini ya utamaduni wa Kiislam, maziko hutakiwa kufanyika haraka iwezekanavyo. Lakini waziri wa mafuta wa Libya amesema mwili wa Gaddafi huenda ukahifadhiwa "kwa siku kadhaa".

Haifahamiki kama kiongozi huyo wa zamani atazikwa Sirte, mji aliouawa siku ya Alhamis, au Misrata, mji aliopelekwa baada ya kufa, au mahala pengine.

Rais wa Ufaransa Nicolas Sarkozy amesema kifo cha Muammar Gaddafi kinamaanisha shughuli za Nato nchini Libya zimefikia kikomo.

Awali kulikuwa na taarifa kuwa mamlaka nchini Libya zinafanya mipango ya kufanya mazishi ya siri kwa kiongozi huyo. Hata hivyo, inaonekana huenda kukawa na kuchelewa kufanyika kwa mazishi hayo, ambayo chini ya utamaduni wa Kiislam mazishi hufanyika haraka iwezekanavyo.

Waziri wa mafuta Ali Tarhouni aliliambia shirika la habari la Reuters kuwa mwili wa Kanali Gaddafi huenda ukahifhadhiwa "kwa siku kadhaa".

WAZIRI MEMBE ALIPOTEMBELEA CLOUDS MEDIA GROUP LEO ASUBUHI

Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe akifafanua jambo wakati wa mahojiano katika redio Clouds Fm iliyopo jijini Dar es Salaam. Pembeni yake yupo mtangazaji wa Clouds Fm Wasiwasi Mwabulambo.

Mkurugenzi wa Utafiti wa Clouds Media Group Bw. Ruge Mutahaba (kulia) akimfafanulia jambo Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe wakati alipotembelea Clouds Media Group.

Tanzania ni nchi ya kuigwa- Waziri Membe
Watanzania wametakiwa kuuenzi Umoja, Upendo na Mshikamano ulipo Tanzania maana ndiyo sifa inayoiweka nchi katika historia.

Hayo ameyasema Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe wakati akifanya mahojiano katika redio Clouds iliyopo jijini Dar es Salaam.

Alisema kuwa nchi za jirani wanatamani sana amani iliyopo mchini Tanzania, maana nchi nyingine huwa mpaka wapigane ndiyo amani ipatikane.

"Tanzania tunaonewa wivu kuhusu huu utaratibu wa kupeana vijiti vya uongozi, kijiti cha Mzee Nyerere akamkabidhi Mwinyi kwa amani na kura...kijiti cha Mzee Mwinyi akamkabidhi Mkapa na vile vile kijiti cha Mkapa akamkabidhi Kikwete hivi ndivyo inavyopaswa kufanyika siku zote," aliongezea Waziri Membe.

"Tunaposherehea miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania ni vyema tukatambua kuwa Tanzania ni nchi ya pekee na ni mfano wa kuigwa kwa mataifa mengine.


PICHA ZAIDI BONYEZA www.kajunason.blogspot.com

SWAHILI FASHION WEEK IN ANGOLA ON 15/10/2011

Designer Gabriel Mollel from Tanzania during the Fashion Bussiness in Angola on 15th-oct-2011

Designer Manju Msita from Tanzania during the Fashion Bussiness in Angola on 15th-oct-2011

Mustafa Hassanali from Tanzania during the Fashion Bussiness in Angola on 15th-oct-2011

Tanzanian Consul in Luanda HE Mziray Mbwana with Team Tanzania at Fashion Business Angola on 15 Oct 2011

"HAKUNAGA USIKU KAMA HUU MWANZA"

oYAaaaa! kArIbU kWEnYe pAtI lA kIkUbWa jUMaMosI hII!!!

TWANGA KUSUGUA VISIGINO NCHINI UINGEREZA

Mkurugenzi Wa Twanga Pepeta Katikati Asha Baraka Akiongea na waandishi wa Habari Kuhusu Uzinduzi na Ziara UK.
Baada ya kufanya na Kumaliza uzinduzi wa albamu yao kabambe tarehe 6 Novemba 2011 ASET wakishirikiana na URBAN PULSE CREATIVE Wanatarajia kuwaburudisha wapenzi wa Bendi Maarufu ya Twanga Pepeta Nchini Uingereza mwishoni mwa Mwezi wa Novemba.

Show Hii Maalum ni kwa ajili ya kuazimisha Miaka 50 ya uhuru wa Tanzania. Tarehe pamoja na maelezo ya Ukumbi yatafuatia mda sio mrefu. Hivyo wadau kaeni mkao wa Kula.

DC ILEMELA AOMBA MSAAADA WA CHAKULA NA MAHEMA KWA WALIOATHIRI NA KIMBUNGA MWANZA.

Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wilaya ya Ilemela na Kaimu Mkuu wa Wilaya hiyo, Said Amanzi ameyaomba mashirika, watu binafsi na wasamaria wema kujitokeza kutoa msaada wa vyakula kwa watu walioathiriwa na kimbunga cha upepo katika Kata ya Bugogwa wilayani Ilemela. Said Amanzi.

Amanzi ameyasema hayo jana jijini Mwanza wakati akitoa tathimini ya uharibifu uliosababishwa na mvua hiyo kwa waandishi wa habari na kuleta athari kubwa miongoni mwa wakazi wa Kata hiyo.

Miongoni mwa sehemu zilizoharibiwa vibaya na mvua hiyo ni pamoja na vyumba vinne vya madarasa na Ofisi ya Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Igombe, Jengo la Ofisi ya CCM na lile la Kanisa la Roman Katholiki.

Katika tukio hilo lililotokea usiku wa Oktoba 18 mwaka huu lililosababishwa na mvua iliyoambatana na upepo mkali jumla ya kaya 322 zimeathirika kutokana na athari hiyo ya mvua na kimbunga na Inakadiriwa pia kaya zipatazo 45 hazina chakula kabisa, zinahitaji msaada wa haraka ikiwa ni pamoja na mahema na chakula hii ni kutokana na vyakula vyao kuharibiwa na mvua.

Jumla ya watu 14 wamjeruhiwa na wote wamekwishatibiwa katika Hosipitali ya Rufaa ya Bugando na wamekwisharuhusiwa.

Tayari hatua mbalimbali zimekwishachukuliwa kuwanusuru wakazi hao ikiwa ni pamoja na kuundwa kwa Kamati ya Ulinzi na Usalama kufanya tathimini ya kina ya athari hizo kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza.

Thursday, October 20, 2011

KANALI GADDAFI AUAWA KIKATILI

Kiongozi wa Zamani wa Libya, Muammar Gaddafi amekufa katika mateso ya majeraha baada ya kukamatwa karibu na Mji wake wa Sirte Juu imethibishwa na Afisa Mwandamizi wa Kijeshi wa Baraza la Taifa Mpito NTC leo.Taarifa kupitia vyombo vya habari.

Afisa huyo wa Baraza la Taifa Mpito, Abdel Majid Mlegta aliiambia Reuters awali kwamba Gaddafi alikamatwa na kujeruhiwa katika miguu yote kabla ya alfajiri leo wakati akijaribu kukimbia baada ya msafara wake kushambuliwa na ndege za kivita za NATO. 'Pia alipigwa risasi kichwani ,`alisema kiongozi huyo.

Majeshi ya upinzani nchini humo yakishangilia kifo cha Gaddafi.

AJALI NYINGINE MBAYA MKOANI MBEYA YAZIDISHA MASWALI

MWILI WA MAREHEMU YUDA AMBOKILE UKIWA UMENASA KWENYE GARI.

MAJERUHI WA AJALI HIYO MBAYA ILIYOTOKEA MBEYA JANA.

MAJERUHI MWENGINE ALIYE NUSURIKA KIFO

STORY
Na Ezekiel Kamanga-Mbeya yetu.
Jinamizi la ajali mbaya limeendelea kuusakama mkoa wa Mbeya ambapo usiku wa kuamkia jana imetokea eneo la Mlima Nyoka Uyole Jijini humo na kuua watu watatu akiwemo dereva wa gari hilo dogo Yuda Ambokile Jeshi la Polisi limethibitisha.

Kaimu kamanda wa polisi Anacletus Malindisa anesema Marehemu wengine ni Peter Kishimba mwenye umri wa miaka 47 mkazi wa Tazara Iyunga na Joshua Sanga mwenye umri wa miaka 2 mkazi wa Uyole jijini Mbeya na ajali hiyo ilitokea majira ya saa Moja na nusu kwa kuhusisha gari Nne ambazo zote zilijeruhi watu waliokuwemo ndani yake.

Wakizungumza na waandishi wa habari eneo la tukio, mashuhuda wa ajali hiyo walisema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni kuharibika kwa gari aina ya Toyota Dyana yenye namba za usajili T 660 AUX ambayo ilikuwa imeegeshwa katika mlima huo.

Walisema kuwa kutokana na kuharibika kwa gari hiyo ndipo gari dogo aina ya Suzuki Escudo yenye namba za usajili T 425 BAZ , iliyokuwa ikitokea barabara ya Mbarali kwenda Mbeya mjini ambayo ilikuwa na abiria watano iliigonga gari hiyo na kusababisha kifo cha Dereva wake Yuda Ambokile na wengine kujeruhiwa vibaya na magari mengine Toyota Cheser T 512 BCT na Nissan T 991 BAK.

Baada ya gari hiyo kugonga gari iliyokuwa imeegeshwa na kusababisha madhara hayo ndipo gari nyingine aina ya Baloon ikagongwa na gari hiyo aina ya Escudo kisha Baloon hiyo ikatumbukia korongoni na kusababisha majeruhi wawili waliokuwemo ndani ya gari hiyo ambao wote walikimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya na Mmoja wao akaruhusiwa baada ya hali yake Kiafya kuimarika.

Ajali hiyo haikuishia hapo bali gari nyingine aina ya Pickup yenye namba za usajili T 991 BAK nayo ikakumbwa na dhahama hiyo ambapo iliharibika vibaya bila kusababisha majeruhi kwa watu waliokuwemo ndani yake.

Majeruhi wa ajali hiyo waliolazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya na kutembelewa na waandishi wa habari leo, wengi wao walikutwa wakiwa na hali mbaya na kushindwa kuzungumza chochote bali baadhi yao waliokuwa na nafuu walisema kuwa walikuwa hawakumbuki chochote juu ya ajali hiyo zaidi ya kujikuta wamelazwa wakiwa na majeraha katika miili yao.

Majeruhi hao ambao baadhi yao waliweza kuzungumza na waandishi wa habari ni pamoja na Denis Untwa (24) ambaye ni dereva wa Baloon, Laina John Sanga (35), Michael Mteve (20), Anania Simbeye(35) ambaye ni dereva wa Escudo, Emmanuel Tambikeni na mmoja aliyejitaja kwa shida jina moja la Boniface..

Habari na (http://www.mbeyayetu.blogspot.com/)

Wednesday, October 19, 2011

KAMBI YA MAFUNZO YA MPIRA WA KIKAPU KWA VIJANA WALIO NA UMRI CHINI YA MIAKA 18 KUMALIZIKA LEO MWANZA.

Kocha Twalib Puzo akitoa maelezo kwa washiriki (hawako pichani) kuanzia kushoto ni Iddy Zuberi, Sosho Kizito, Twalib Puzo, Vicent Shinde katika mafunzo ya mpira wa kikapu kwa vijana walio chini ya umri wa miaka 18 kutoka katika shule mbalimbali za sekondari jijini mwanza, yakiendelea kufanyika katika uwanja wa CCM Kirumba na yanatarajiwa kumalizika leo saa 10 jioni katika uwanja huu.

Mafunzo hayo yameandaliwa na kusimamiwa na Shirika la kijamii la Planet Social development (PSD) la jijini Mwanza pamoja na Mambo Basketball kutoka Dar es Salaam yamejumuisha jumla ya vijana 81 ikiwa wavulana ni 68 na wasichana ni 13.

Mafunzo hayo yalikuwa na malengo yafuatayo:
1.Kuangalia vipaji na jinsi ya kuviendeleza katika kusaidia maendeleo ya mchezo huu hapa Tanzania ambao ni wito wa shirikisho la mpira wa kikapu Tanzania (TBF).
2.Kupata na kutoa picha halisi kwa wachezaji ikiwa ni sehemu ya mafunzo tutakayoyafanya mwakani kwa kushirikiana na kocha wa Basketball program ya Memorial Newfound University kutoka Canada. Hii ni baada ya mafunzo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam mwezi wa saba mwaka huu ambapo kijana wa ki Tanzania Alphaeus Kisusi alifanikiwa kupata “Partial Scholarship” kwenda kusoma katika chuo hicho.
3.Kubadilishana uzoefu na makocha wa mchezo huu hapa mwanza katika kuendesha mafunzo kama haya kwa siku zijazo.
4.Kuendeleza ushirikiano wa vikundi vyetu (Mambo Basketball na PSD) katika kutekeleza malengo tuliyojiwekea kama US Sports program Alumni baada ya safari yetu ya mafunzo nchini Marekani mwaka 2009 iliyogharamiwa na Ubalozi wa Marekani – Tanzania.

Washiriki kwenye training.

Mafunzo haya yanatarajiwa kufungwa na Rais wa shirikisho la mpira wa kikapu Tanzania ndg. Mussa Mziya akiambatana na mlezi wa vijana katika chama cha mpira wa kikapu Mkoa wa Mwanza ndg Altaf H. Mansoor “Dogo”

DAKTARI MTANZANIA JULIE MAKANI APOKEA TUZO KUTOKA ROYAL SOCIETY PFIZER LONDON

Dr Julie Makani Akipokea Tuzo yake.

Wageni waalikwa kwenye Royal Society Pfizer Awards London

Dr Julie Makani. akiwa na Cleo, Paul na Frank baada ya kupokea Tuzo.

Parliamentary Under Secretary of State, International Development Stephen O'Brien. akimpongeza Dr Julie Makani PG

Dr Julie Makani akiwa na familia yake

Kutoka Kulia Balozi Kallaghe, Mama Makani, Dr Makani, MP O'Brien, Naibu Balozi Chabaka na Mr Simba

Dr Julie Makani kutoka Tanzania amepokea Tuzo jumanne tarehe 18 octoba 2011 ya Royal Society Pfizer nchini Uingereza. Dr Makani amepokea tuzo hii ya utafiti alioufanya katika gonjwa hatari la Sickle Cell (SCD) ambaye makazi yake ya kazi ni kwenye Chuo Kikuu Cha Afya na Sayansi cha Muhimbili katika idara ya Haematology. Kutokana na utafiti wake kumeonekana ushahidi kuwa, chanzo kukuu cha magonjwa na vifo vitokanavyo na sickle Cell nchini Tanzania husababishwa na Arnemia (upungufu wa damu)

Dr Makani pia amefanya mchakato wa matibabu katika majaribio ya Hydroxyure chemotherapy agent inayo gusa Bone marrow katika matibabu ya Anaemia kwenye ugonjwa Sickle Cell

Ni matumaini yake kuwa utafiti huu utapelekea kuboresha uchunguzi na matibabu ya ugonjwa huu ili kuweza kuimarisha afya za watu, mfumo mzima wa afya na jamii kwa ujumla.
Kwa niaba ya Watanzania wote blogu ya G. Sengo inatoa pongezi kwa DR Makani kwa mafanikio hayo.


Asanteni.
Urban Pulse.

Tuesday, October 18, 2011

MASHITAKA 8 KATI YA 9 'TUPA KULE' KESI YA KUPINGA MATOKEO ILEMELA, KESI YAHAIRISHWA WALALAMIKAJI WAINGIA MITINI

Wakili Tundu Lisu akitoa maelezo ya mwenendo wa kesi hiyo huku mteja wake Mbunge Highness Samson (wapili kuia) akimsikiliza kwa makini.
Kesi namba 12/2010 yakupinga matokeo ya uchaguzi mkuu jimbo la ilemela mkoani Mwanza iliyompatia ushindi mbunge kupitia tiketi ya CHADEMA bw. Highness Samson imeahirishwa tena leo jioni katika mahakama ya rufaa jijini humo.

Wakili T. Lisu (kulia) akiwa ameambatana na mteja wake mbunge H. Samson wakitoka kwenye ukumbi wa mahakama.
Kati ya mashitaka tisa yaliyofunguliwa dhidi ya mbunge wa sasa wa Ilemela mashitaka nane yametupiliwa mbali na kubaki shitaka moja tu ambalo ni dai la watu wapatao laki moja na elfu kumi na nne kudaiwa kuzuiwa kupiga kura.

Shitaka hilo lililosalia linaonekana kukosa nguvu kwani linafananishwa na kesi ya uchaguzi ya mwaka 1995 ya bw. Silvester Masinde na Pius Msekwa, ambapo Mahakama ya Rufaa Tanzania iliamuru kuwa kura ambazo hazikupigwa au hazikuhesabiwa kugawanywa kwa uwiano wa asilimia walizopata wagombea kwenye uchaguzi.

Mashitaka nane yaliyofutwa ni pamoja na kufanyika kampeni kwenye vituo vya kupigia kura na makanisani siku ya kupiga kura, wafuasi wa chadema kuzuia watu wasipige kura, mgombea wa chadema na mawakala wake kutoa rushwa kwa kujenga visima kwa wapiga kura na kutoa vinywaji na vyakula kwenye misiba, mahela yalitolewa kwenye eneo la Manguruwe, mshtakiwa mbunge pamoja na mawakala wake walinunua shahada za wapiga kura, kulikuwa na mabadiliko ya vituo vya wapigia kura vituo vya soko la Kirumba na kwenye viwanja vya Furahisha, jingine ni kuwa kuna mawakala wa Sangabuye na Buhongwa hawakula kiapo cha kutunza siri.

Mfanyabiashara maarufu jijini Mwanza Jack Fish' akiteta jambo na mh. mbunge na wakili wake mara baada ya kuahirishwa kwa kesi hiyo ambapo inategemewa kusomwa tena Ijumaa hii 21oct2011.

Matokeo ya uchaguzi huo yanayopingwa ni kuwa Highness Samson aliweza kutangazwa kuwa mshindi wa kiti cha ubunge wa jimbo la Ilemela kwa kumshinda Anthony Diallo wa CCM kwa kura 31,269 dhidi ya kura 26,270 hii ikiwa ni tofauti ya kura 4,999.