ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, September 24, 2011

VITU ADIMU......!!!!

Ni mchana majira ya saa saba na dakika 45 wanafunzi wa moja ya shule kata ya Isangijo Wilayani Meatu wakitoka kuteka maji umbali wa kilometa tano kwaajili ya matumizi kwa nyumba ya mwalimu.

Mawasiliano yakitafutwa eneo la mwinuko.

Mawasiliano yamepatikana.

Chakula mashuleni.

tathimini zinaonyesha kuwa ni ukweli usiofichika mradi wa chakula mashuleni umechangia kunyanyua kwa kiwango kikubwa mahudhurio ya watoto.

Usafiri.

Pozi la akina mama walojaa furaha.

Supu time katikati ya sherehe.

TASWIRA AJALI MBAYA YA LORI MJI MDOGO WA MBALIZI ILIYOUA WATU WA3 AKIWEMO MWANAFUNZI

Polisi wakiangalia gari aina ya roli lenye namba IT.9518, lililopata ajali baada ya kugongana na gari jingine na hivyo kupinduka na kusababisha vifo vya watu watatu watembea kwa miguu na kuvunja nyumba.

Gari lenye T.438 BRT aina ya Landover, mali ya mchungaji Nduka wa kanisa la Uinjilist Mbalizi. Ambalo liligongana na Lori hilo.

Taswira ya mbele ya Lori hilo lililosababisha hasara kumbwa.

Mwanafunzi wa chuo kikuu cha DIT kilichopo Dar es Salaam , Marehemu Dickson Nswila, ambaye alikuwa akielekea kwenye mazoezi ya vitendo TAZARA, jijini Mbeya.

Mfanyabiashara wa mitumba, mji mdogo wa Mbalizi Marehemu Charles Mwakanyuma.

Marehemu Mariam Side mwenye umri wa miaka 31.

Picha zote na www.latestnewstz.blogspot.com

Friday, September 23, 2011

NAPE AKIWA MWANZA AFUNGUKA KUHUSU CCM.

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye amesema kwamba licha ya madai kuwa chama hicho kimepoteza mvuto mbele ya jamii lakini takwimu zinaonyesha watashinda katika uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Igunga mkoani Tabora.Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Mwanza, Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi wa CCM amesema kwamba wanaodai kuwa Chama hicho kimepoteza mvuto wanatumia hoja za jumla badala ya takwimu. Amesema kwamba utafiti mdogo alioufanya katika mikoa 12 kwa kuangalia matokeo ya chaguzi ndogo za serikali za mitaa zilizofanyika kati ya mwaka 2009 hadi 2011, unaonyesha kuwa CCM bado ina mvuto mbele ya jamii na ana uhakika wanashinda katika uchaguzi mdogo wa ubunge huko Igunga.

Mikoa ambayo amefanya utafiti ni pamoja na Mara, Pwani, Dar es salaam, Shinyanga, Mbeya, Manyara, Singida, Morogoro, Mtwara, Arusha, Tabora na Tanga pia katika mikoa hiyo kwa kipindi cha kati ya mwaka 2009 na 2011 zimefanyika jumla ya chaguzi ndogo za viongozi wa vijiji 84, mitaa 22 na vitongoji 248.

Kwa mujibu wa Nape, kati ya viti 84 vya wenyeviti wa vijiji, CCM kimefanikiwa kunyakua viti 83 sawa na asilimia 98.8, kati ya mitaa 22, CCM kimeshinda viti 17 sawa na asilimia 77.3 na kati ya vitongoji 248, CCM kimeshinda vitongoji 186 sawa na asilimia 75.


Akizungumzia kuhusu ukali wa maisha Mh. Nape anasema suala hilo linahusiana na uchumi wa dunia na si kwa nchi ya Tanzania.

Akizungumzia hatua ya aliyekuwa Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz kuachia nyadhifa zake za ubunge na ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) akidai kuchoshwa na siasa uchwara lakini akarejea tena katika ulingo wa siasa kumnadi mgombea wa chama hicho Dk. Peter Kafumu, Nape amejitetea kwa kutoa mfano kwa kusema kuwa hata kanisani mtu akifanya kosa kuna adhabu maalum zilizo wekwa kama vile kutokushiriki meza ya bwana na kadhalika lakini siyo kwamba mtu huyo atakatazwa kuingia kanisani, ataingia kanisani kwa minajili ya kulishwa neno kuendana na utaratibu.


Amebainisha kubainisha kwamba Chama Cha Mapinduzi kinao mtaji wa wanachama ambapo katika kura za maoni kuwapata wagombea katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga, mgombea wa CCM alichaguliwa na wanachama 588 ilhali mgombea wa CHADEMA alichaguliwa wanachama 63.

Kupitia takwimu hizo Nape amejigamba kwa kusema kuwa CCM ina msingi mzuri iliyoujenga wa kushinda katika uchaguzi huo mdogo wa ubunge katika Jimbo la Igunga licha ya fitna zinazojitokeza kila kukicha toka kwa wapinzani wake, hivyo watu wasishangae siku chama hicho kitakapotangazwa kuwa mshindi.

BP YANYWEA KWA SERIKALI, KUPEWA LESENI KWA MASHARTI

KAMPUNI ya uuzaji wa mafuta ya BP imesalimu amri kwa Serikali, hivyo kuamua kuondoa mahakamani shauri la kupinga kufungiwa kwake na badala yake kurejea katika meza ya mazungumzo, hivyo kupewa masharti manne inayopaswa kuyatekeleza kabla ya kurejeshewa leseni kuendelea na biashara hiyo.

Masharti hayo yanatokana na kampuni hiyo kukaidi agizo la Serikali la kushusha bei ya mafuta iliyotolewa Agosti mwaka huu, na badala yake kufunga vituo vyake vyote, hali iliyochangia uhaba mkubwa wa mafuta nchini. Hatua hiyo ilisababisha Serikali kutoa amri ya kufunguliwa kwa vituo hivyo katika muda wa saa 24, amri ambayo BP iliendelea kuikaidi, hivyo kupokwa leseni yake.

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Nishati na Maji (Ewura), Haruna Masebu, alisema jijini Dar es Salaam jana kuwa, BP ilikuwa miongoni mwa kampuni zilizokuwa zikisambaza mafuta nchini, lakini baada ya kushushwa kwa bei ya bidhaa hiyo kampuni hiyo iligoma, badala yake ikakimbilia mahakamani.

Katika mkutano na waandishi wa habari, Masebu alisema kutokana na hasara waliyopata, BP wamelazimika kufuta kesi na kutaka kuingia kwenye kikao cha majadiliano kilichohitimisha malumbano yaliyokuwapo kwa kuwapa masharti manne kabla ya kuwarudishia leseni.

Chanzo cha mvutano
Mvutano baina ya Serikali na BP ulianza Agosti 3, mwaka huu baada ya Ewura kupitia kwa Masebu ilipotangaza kushusha bei ya mafuta mjini Dodoma ambapo petroli ilishuka kwa Sh202.37 kwa sawa na asilimia 9.17.

Katika tangazo hilo, dizeli ilishuka kwa Sh173.49 sawa na asilimia 8.32 na mafuta ya taa yalishuka bei kwa Sh181.37, sawa na asilimia 8.70. Masebu alisema kushuka kwa bei hizo kulitokana na kukamilika kwa mchakato wa kuandaa kanuni mpya ya ukokotoaji wa bei za bidhaa za mafuta hasa kutokana na maagizo ya Serikali na pia, kubadilika kwa viwango vya kodi katika bidhaa za mafuta.

Mkurugenzi huyo alifafanua kuwa, kodi za mafuta ya taa ziliongezwa na pia kupunguzwa kwa kodi za mafuta ya dizeli na tozo za mamlaka mbalimbali zimetazamwa na kupunguzwa.


CHANZO www.mwananchi.co.tz

Thursday, September 22, 2011

MATUKIO KATIKA PICHA SIMBA NA TOTO AFRICANS

Toto na Simba jumatano ya tarehe 21sept2011 CCM Kirumba Mwanza.

Wachezaji wa timu ya Toto Africans wakipongezana kwa moja ya magoli yao yaliyopatikana jana.

Toto v/s Simba.

Mchezo huo ulishuhudia matukio kadhaa katika dakika ya 15 mashabiki walivunja geti la uwanja na kuingia uwanjani, lakini polisi waliweza kuthibiti tukio hilo kabla ya mbwa wa polisi kumponyoka askari na kuingia uwanjani na kuanza kukimbiza wachezaji ambapo alimfukuza zaidi Haruna Moshi na kusababisha mpira kusimama kwa dakika tano katika dakika ya 29.

Mbwa mwenye mfunzo akitweta mara baada ya saka-saka za kumfukuza Boban (hayupo pichani)aliyetimka kwa spidi kama farasi kushindikana kukamatika.


Nje nako:- mguu hapa, mbwa hapa. Usimamizi mbovu wa ukataji tiketi kwani kulikuwa na Hiace moja tu iliyokuwa ikikatisha tiketi kiasi cha kusababisha baadhi ya wapenzi wa soka kuchelewa kuingia na wengine kuahirisha kabisa kutinga dimbani humo.

Mashabiki wa Simba wakishangilia bao la tatu la kusawazisha lililofungwa nae Patrick Mafisango katika dakika ya 69.

Wednesday, September 21, 2011

SIMBA YAKAMATWA MKIA NA TOTO LA MTAA WA KISHAMAPANDA

Ligi kuu ya soka Tanzania bara imeendelea tena leo kwa michezo mbalimbali mmojawapo ukipigwa katika dimba la CCM Kirumba jijini Mwanza ambapo timu za Simba ya Dar es salaam na Toto toka jijini hapa zimegawana pointi mara baada ya kutoka sare ya 3-3.

Mchezo ulianza kwa kasi ya ajabu pasi za nguvu, wachezaji wa timu zote wakionana mithili ya game za soka barani Uropa na haikuchukuwa muda ilikuwa ni dakika ya 8 tu kipindi cha kwanza mchezaji Felix Sunzu aliwanyanyuwa mashabiki wa timu ya wekundu wamsimbazi kwa kupachika bao la kuongoza.

Toto wakicheza nyumbani wakiwa na kibri cha kuwa na mashabiki lukuki huku wakionana walifanikiwa kuichanganya ngome ya simba kwa samba la hatari likiongozwa na vifaa vipya walivyosajili mwaka huu hali iliyopelekea ngome yake kupoteza mwelekeo hivyo kusababisha madhambi na Toto kuzawadiwa penati, bila ajizi mshambuliaji wa kimataifa aliyesajiliwa na timu hiyo Darlington Enyina aliutumbukiza kimiyani mpira huo kuandika bao la kusawazisha ikiwa ni dakika ya 15 ya mchezo.

Toto ilijipatia bao la pili dakika ya 26 kupitia Mohamed Sudi , Simba ikasawazisha dakika ya 59 mfungaji akiwa Felix Sunzu.

Bao la tatu la Toto lilipatikana katika dakika ya 65 kupitia Iddi Mudy nao Simba kusawazisha tena bao hilo dakika tatu baadaye kwa mkwaju wa kiufundi wake mshambuliaji mahiri wa wanamsimbazi Patrick Mafisango.

Mchezo uligeuka kuwa wa upande mmoja kwa Simba kulisakama kama nyuki lango la Wanakishamapanda waliopoteza uelekeo mara baada ya moja kati ya kifaa chake Filemon mwendafile kulimwa kadi nyekundu akimkanyaga mgongoni tena kwa maksudi mchezaji wa Simba Kago.

Hadi mwisho ngoma droo Simba 3, Toto 3.

Tuesday, September 20, 2011

MBUNGE WA CCM JIMBO LA KISESA MH. LUHAGA JOELSON MPINA APOKELEWA KWA SHANGWE NA WANANCHI WA JIMBO LAKE.

Mbunge wa Jimbo la Kisesa wilayani Meatu Luhaga Joelson Mpina (CCM) amepokelewa kwa shangwe za msisimko wa ajabu na wananchi wa jimboni kwake katika mkutano wake wa kwanza wa kuwashukuru wakazi wa jimbo lake kwa kuwa imani naye na kumchagua kuwa mbunge wao kwa awamu ya pili.

Moja kati ya matukio ya kusisimua ni ushirikiano alio nao Mh. Luhaga na vyama vingine ambapo Mwenyekiti huyu wa moja ya vijiji jimboni humo kupitia chama cha CHADEMA Sita Ngeniobuyu alijumuika kusikiliza shukurani za Mbunge wake na hakusita kumshika mkono kumpongeza kwa kazi nzuri aliyoifanya.

Mbunge wa Jimbo la Kisesa, Wilaya ya Meatu, Mkoa mpya wa Simiyu Mh. Luhaga Joelson Mpina akitunzwa kiasili na akinamama kupitia mila za kabila la Wasukuma jimboni humu.

Ujenzi wa barabara pamoja na madaraja ni moja ya changamoto kubwa za maendeleo Jimboni Kisesa.

Tangu kipindi cha Uchaguzi 2005 Jumla ya madaraja sita yenye thamani ya shilingi bilioni 1.5 yamejengwa yakipitika ambayo ni pamoja na daraja la mto Simiyu, Tingabuligi, Sakasaka, Lingeka, Lubiga na Longalonhiga.

Zaidi ya bilioni 1.6 zimetengwa kupitia bajeti ya serikali kuipatia umeme wilaya ya Meatu na vijiji vyake ambapo mpaka sasa miundombinu ya nguzo imekwisha simikwa huku mradi ukitegemewa kukamilika rasmi mwezi desemba 2011.

Sehemu ya wakazi wa Jimbo la Kisesa waliofurika kumlaki mbunge wao.

Akiwa kama moja ya waalikwa meza kuu kwenye kusanyiko hilo Mwenyekiti wa kijiji cha Lubiga kupitia CHADEMA Sita Ngeniobuyu alipata fursa ya kutoa shukurani zake kwa wananchi waliofurika kusikiliza shukurani na mipango ya maendeleo ya baadaye jimboni humo zake Mh. Mbunge Luhaga Joelson Mpina, pembeni yake ni Afisa Mahusiano Ofisi ya Mbunge Tito Paul Masele.

"Shauri zenu! jimboni humu sisi hatujali.. wewe ni wamashariki au magharibi tunapiga kazi pamoja kwani ni waajiriwa wa wananchi" Kauli ya katibu wa CCM wilaya ya Maswa Omary Kalolo (kushoto) aliyekuwa kivutio kwenye mkutano huo.

Wazee wa kijiji cha Mbugayabanyha wakimsikiliza kwa makini mbunge wao.

Kwa ajili ya kukuza michezo hapa Mratibu wa Elimu kata ya Lubiga bw. Emanuel Manyama akikabidhiwa vifaa vya michezo kwa kata yake.

Mwenyekiti wa kijiji cha Mbugayabanyha bw. Charles akikabidhiwa vifaa vya michezo kwaajili ya kijiji chake.


Ili kudumisha mahusiano na afya vilevile kukuza michezo nchini naye timu manager wa Lubiga Shooting bw. Misomung'ombe naye alikabidhiwa vifaa vya michezo ndani ya kusanyiko hilo.

Monday, September 19, 2011

SIYO KUTEMBEA TU.. NASAFIRI PIA!!

Kumekucha katika kijiji cha Mwandoya makao makuu ya jimbo la Kisesa wilayani Meatu mama akiwasha moto tupate kifungua kinywa.

Ndoo zitalala hapa shwaaaari bila mlinzi ni foleni kusubiri maji, Fanya hivi kwetu mujini uone!!!.

Vielekezi Jiografia.

Hicho kistuli mwanawane ni Sheli aka kituo cha mafuta kijijini hapa.

Nyumba bora na salama nilizokutana nazo njiani.

Yawezekana ulikuwa ukiyatafuta sana mawasiliano haya..au kama vipi kesho utayahitaji.

Sunday, September 18, 2011

BREAKING NUUZ: MOTO WATEKETEZA SOKO DOGO LA FOREST MAGHOLOFANI JIJINI MBEYA USIKU WA KUAMKIA LEO

Moto wateketeza soko hilo lililopo Forest ya zamani karibu na Chuo cha Mzumbe na Chuo Kikuu huria Jijini Mbeya

Moto ulianza majira ya saa 9:00 kamili usiku na Zimamoto walifika saa 9:10 na kufanikiwa kudhibiti moto huo ambao umeteketeza vibada kadhaa na kusababisha hasara kubwa.

Mtandao huu umefanikiwa kukuta baadhi ya masalia ya vibanda yakifuka moshi.

Mkuu wa wilaya Bwana Evans Balama asaidia kuzima Moto huo, lakini wadau wanajiuliza kunani katika masoko ya Mbeya na kwanini tahadhari hazichukuliwi

Picha zote na Latest News Tz