ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, September 3, 2011

MH. HIGHNESS, WENJE, VICENT, MAMA HEWA, WASHIRIKI NA MAELFU HESHIMA ZA MWISHO NA MAZISHI KWA DIWANI WA KIRUMBA MWANZA

Novatus Manoko Tangu 11/04/1969 hadi 31/08/2011.

"Si wakati wa kukata tamaa ni wakati wa kufarijiana kushikamana na kusema kurudi nyuma mwiko" Mbunge wa Musoma mjini Vicent Makongoro akihutubia wananchi waliokusanyika katika viwanja vya Magomeni kirumba jijini Mwanza kwaajili ya kutoa heshima zao za mwisho kwa marehemu.

"Ndugu zangu Leo tumesimama hapa hatupo katika kujali chama bali tupo kwa ajili ya kazi na mema aliyofanya ndugu yetu aliyelala ambaye namfahamu sana tangu nikiwa naibu meya wa jiji la Mwanza yeye akiwa mkusanyaji mzuri wa mapato ya Halmashauri na kwautendaji wake alikuwa rafiki yangu mzuri sana" Kauli ya Mbunge wa CCM Mama Maria Hewa ambaye aliyeshangiliwa na umati uliofurika viwanjani hapo mara baada ya kutoa salamu ya PEOPLE'S ......


Mbunge wa Ilemela Mh. Highness Samson akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa marehemu Diwani Novatus Manoko.

Mbunge wa Nyamagana Mh. Wenje akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu N. Manoko.

Kwaheri KIONGOZI ndivyo alisikika akisema mama huyu mwanachama wa CHADEMA.

Kulikuwa na misafara ya mistari minne kutoa fursa kuelekea kuaga mwili wa marehemu.

Akina mama wafanyabiashara wa soko la Mwaloni Kirumba katika sare ya pamoja.

Usimamizi ulidhibitiwa kumwezesha kila mwananchi kufika eneo la tukio.

"R.I.P Kamanda"

Sehemu ya wana ndugu na familia ya marehemu.

Umma

Hatimaye jioni ya leo marehemu amezikwa katika makaburi yaliyoko eneo la Kitangiri kata ya Kirumba wilayani Ilemela jijini hapa.

FIKIRIA NA WENGINE WALIO NA UHITAJI

Watu hukaa katika majumba ya kifahari meza zikisheheni kila aina ya tunda nayo kwa mafungu makubwa makubwa.

Wakichinja kila aina ya vitoweo, wapishi katika masufuria makubwa walipika vyakula kwaajili ya sherehe yenye nia moja tu nalo ni kupongezana.

Vyakula vya nafaka kwa shehena vikapikwa.

Nao hula na kunywa hata kusaza.

Mara baada ya sherehe chakula kingi kilichosalia humwagwa hata kisibakie kwani marufuku kula kiporo.

Kikimwagwa majalalani kama taka.

Chakula choote hutupwa.

Hayo yakifanyika hebu fikiria juu ya ndugu zetu wengine, wakiishi kama ndege kuokoteza.

Upande wa pili wa dunia unadhoofika kwa kukosa lishe.

Hali si hali kwa kukosa hata kipande cha chakula.

Mtizame mama yule anayenyonyesha.
DON'T WASTE FOODS ANY MORE, Kusanya peleka kwa wenye uhitaji.

Let this be remembered.. . each time we throw away Foods!
People who live in rich countries,, don't know this,, don't want to know
this,, never understand this!

but U,, please U,, understand this .........

MH. MABULA ASHUSHA TENA NEEMA KUVIWEZESHA VILABU VYA SOKA MWANZA

Diwani wa kata ya mkolani Stanslaus Mabula leo amekabidhi msaada wa vifaa vya michezo vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mbili kwa timu mbili tofauti za soka jijini Mwanza.Msaada wa kwanza ni Jezi seti moja na soksi pea 16 vyote vikiwa na thamani ya shilingi laki sita na nusu vilikabidhishwa kwa mkurugenzi wa jiji la Mwanza Wilson Kabwe (kushoto) ambaye pia ni mlezi wa timu ya Halmashauri ya jiji la Mwanza Fc MCC.

Akikabidhi msaada huo Mabula amesema kwamba yeye akiwa kama mdau wa michezo ametekeleza ahadi yake ya kuchangia timu hiyo baada ya kuombwa na uongozi wa timu hiyo kama sehemu ya chachu ya timu hiyo inayoshiriki ligi ya wilaya ya Ilemela na michuano ya kombe la ng’ombe inayoendelea kwenye uwanja wa michezo wa Jeshi Nyegezi ambapo timu hiyo imetinga hatua ya robo fainali.

Ameongeza kuwa akiwa kiongozi wa wananchi wa kata ya Mkolani na mdau mkubwa wa michezo ataendelea kutoa misaada mbalimbali ambayo italenga kukuza vipaji na kuendeleza michezo na amewaomba viongozi wengine wakiwemo na viongozi wenzake kuendelea kuzisaidia timu mbalimbali badala ya kuliachia jiji pekee ambalo huchukuwa muda mrefu kupitisha fedha za kuzisaidia timu na vifaa hali inayosababisha timu zetu kutofanya vizuri kwenye mashindano mbalimbali zinazoshiriki
.Naye mkurugenzi wa jiji la Mwanza Wilson kabwe amempongeza diwani huyo kwa kuguswa na kuhamasika kutoa msaada huo jambo ambalo limeonyesha kuwa ni kiongozi wa vitendo na anayependa maendeleo kwa wakazi wa jiji na katani kwake kwani si msaada wa kwanza toka kwa diwani huyo.

“Uongozi ni kuonyesha mfano na kuhakikisha unasimamia maendeleo kwa jamii ili kuleta manufaa ambayo yatasaidia vijana kukuza vipaji, kupata ajira na kuendeleza sekta ya michezo kwa kuzingatia ilani zilizo wekwa kuendeleza michezo nchini, jinsi zinavyotekelezwa kwa vitendo basi zinakuza kwa watu walio wachagua” Alisema Mkurugenzi kabwe wakati akitoa shukurani.


Pia diwani huyo amekabidhi jezi seti moja, mipira miwili vyenye thamani ya shilingi laki nne na kiasi cha shilingi laki tatu taslimu kwa timu ya Fc Shadia ya mtaa wa Shadia kata ya mkolani ikiwa ni kutekeleza ahadi wakati alipoalikwa kuwa mgeni rasmi wa hafla ya kumpongeza kuanzisha mashindano ya Kamanda Cup aliyoyaanzisha mwaka jana kabla ya kuwa diwani.

Wakati akikabidhi vifaa hivyo na fedha Diwani Mabula amesema kwamba mwaka huu mashindano hayo ya Kamanda Cup atayabadilisha jina na kuitwa Mkolani Cup na yatashirikisha timu kutoka mitaa yote ya kata hiyo, huku akiwa ameyaboresha zaidi kwa kutoa vifaa vya michezo vyenye ubora na kuongeza fungu kubwa kwa upande wa zawadi hivyo amezitaka timu kuanza maandalizi mapema ikiwemo Fc Shadia ambayo tayari imepata changamoto ya vifaa vitakavyoisaidia timu hiyo kwenye maandalizi.

Friday, September 2, 2011

MWILI WA ALIYEKUWA DIWANI WA KIRUMBA KUPITIA CHADEMA KUAGWA KESHO.

Mwili wa aliyekuwa diwani wa kata ya Kirumba (Mwanza)kupitia tiketi ya CHADEMA, Novatus Manoko aliyefariki jioni ya Aug,31,2011 utaagwa kesho katika viwanja vya wazi vya Magomeni Kirumba jijini Mwanza.

Siku meya mpya wa jiji la Mwanza kupitia CHADEMA Bw.Josephat Manyerere(kulia) aliposhinda na kupongezwa na mbunge wa Nyamagana Mh.Wenje, na kwa chati pembeni ndiye marehemu diwani wa Mwaloni Kirumba Bw.Novat Manoko....

Mwili wa diwani huyo leo ulichukuliwa toka hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza kwa maandamano makubwa ya vijana waliokuwa wakipeperusha bendera za chama hicho huku ummati wa waandmanaji ukiongezeka hatua kwa hatua kuelekea nyumbani kwa marehemu ambapo msiba utakesha pale kwaajili ya shughuli za heshima ya mwisho hapo kesho.

Moja kati ya kashikashi alizowahi kukutana nazo marehemu katika kipindi cha kuelekea uchaguzi wa mwaka jana uliompatia ushindi ni tukio lililotokea mnamo september 2010 kunusurika kufa baada ya kuvamiwa na kukatwa mapanga na watu wasiojulikana ambapo katika tukio hilo, Manoko alijeruhiwa sehemu za kichwani.

Marehemu pia alikuwa mkuu wa wafanyabiashara katika soko linaloshika Uchumi wa jiji la Mwanza, Mwaloni Kirumba.

BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LAKE LIHIMIDIWE.

MAONYESHO YA BIASHARA 8-8 MWANZA KUMALIZIKA TRH4 SEPT

Mwanadada Agatha akihudumia wateja wake ndani ya maonyesho ya 8-8 mkoani Mwanza yaliyoanza tarehe 26 mwezi August yakitazamiwa kumalizika tarehe 4 September 2011.

Nyuzi bin nyuzi.

nyuzi bin nyuzi pati two.

Banda la Barmedaz na mashamsham yake.

Mambo ya shoes hadi night.

Hapa napo panashine.

Thursday, September 1, 2011

TAARIFA YA MABADILIKO YA JINA NA LINK YA TONE INTERNET RADIO KWENDA TONE ONLINE RADIO

TAARIFA YA MABADILIKO YA JINA NA LINK YA TONE INTERNET RADIO KWENDA TONE ONLINE RADIO
Tone Multimedia Company Limited inapenda kuwapa taarifa wananchi wote popote Duniani kuwa tumefanya mabadiliko ya jina la Radio pia jina la Tovuti ambapo mala ya kwanza ilikuwa inaitwa Tone Internet radio na Jina la Tovuti lilikuwa ni www.toneinternetradio.blogspot.com, Kutokana na Sababu za kimsingi za kuingiliana kwa mtandao na Radio moja iliyopo USA inakwenda kwa jina la Tune Internet Radio ndio sababu iliyo tupelekea kubadilisha jina na kuzaliwa kwa jina jipya la Tone Online Radio ambapo tovuti yake sasa itakuwa ni www.toneonlineradio.blogspot.com na ikumbukwe pia Tone Online Radio ni Radio inayo tumia internet Pekee hatuna Frequency za aina yoyote. asanteni sana atakae pata link hii ampatie na mwenzake.pia kwa wanamuziki watume na maproducer watume kazi zao kupitia toneonlineradio@live.com Kwa pamoja tunaendelea kuleta maendeleo ya mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia. Tone Online Radio Tumekufikia popote Duniani.
Natanguliza Shukrani kwa niaba ya Uongozi,
Imetolewa na,
Joseph Mwaisango
Mkurugenzi wa Mawasiliano
Tone Multimedia Company Limited.


KUSIKILIZA TONE ONLINE RADIO BOFYA HAPA:
www.toneonlineradio.blogspot.com

BARAZA LA IDDI: JK ATUNISHA MISULI AONYA, MAHAKAMA YA KADHI HAITATEKELEZA SHARIA

RAIS Jakaya Kikwete amelikataa ombi la Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) la kuitaka serikali iwarejeshee shule ambazo walikuwa wakizimiliki kabla ya kutaifishwa miaka michache baada ya uhuru.Kikwete alitoa msimamo huo ambao alikiri kwamba unaweza ukawakera baadhi ya Waislamu wakati akihutubia kwenye Baraza Kuu la Iddi lililofanyika kitaifa katika Msikiti wa Gaddafi mjini Dodoma jana.

Badala yake, Rais Kikwete alizitaka taasisi za Kiislamu kuweka msisitizo katika kuzijenga shule mpya kwani maombi yao ya kutaka warejeshewe shule walizokuwa wakizimiliki yamekuja yakiwa yamechelewa.

Alisema uamuzi wowote wa kuzirejesha shule za Waislamu leo unaweza ukasababisha mgogoro mzito kutokana na ukweli kwamba wakati wa utaifishwaji serikali ilichukua shule zilizokuwa zikimilikiwa na taasisi tofauti za kidini na watu wa rangi tofauti.

Akifafanua, Rais Kikwete aliwalaumu Waislamu kwa kuwa mstari wa mbele kunung’unika kwamba wanaachwa nyuma katika masuala ya maendeleo kama yale ya elimu tangu mwaka 1992 pasipo kuchukua hatua zozote.

Kikwete aliyeonekana kuzungumza kwa namna iliyoonyesha kuchukua msimamo mkali na wa wazi dhidi ya maombi ya BAKWATA yaliyowasilishwa kupitia katika risala yao, iliyosomwa na Sheikh Mkuu wa Dodoma, alisema serikali kama si juhudi kubwa zilizofanywa na waasisi wa taifa hili hali ya ustawi wa elimu uliopo leo usingefikiwa.

“Tumeshirikiana vema na taasisi za dini, naamini bila ushirikiano huo baadhi ya maeneo wasingepata huduma za afya, elimu, maji na miundombinu…napenda kuwahakikishia kuwa hakuna kitu chochote ambacho serikali itatoa na kuwabagua wengine.

“Baada ya uhuru Mwalimu Nyerere alitaifisha shule hizo ili kuweka uwanja sawa kwa watoto wa rangi, dini na kabila zote kwa sababu zilikuwa za serikali.

“Ninyi kama mnataka jengeni shule na vyuo serikali itawasaidia kama inavyofanya kwenye shule na vyuo vya wenzetu Wakristo, shule za Azania na Kihindu…mfano ni mkopo unaotolewa na serikali kwa wanafunzi waliopo katika vyuo vya Wakristo.

Alisema wanaomcha Mungu ni watu wa upendo siku zote kwa sababu wanawahudumia vema wananchi wanaowahubiria amani na upendo, hali inayovipunguzia kazi ya kupambana na uhalifu vyombo vya dola.

Aidha, aliwataka Waislamu kuunda Mahakama ya Kadhi bila kuitegemea serikali huku akibainisha kwamba ushauri huo ulitolewa na Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria, Profesa Ibrahim Juma, ambaye ni mtaalamu wa Sharia na Sheria za Kiislamu.

Alisema mahakama hiyo ya kadhi itakayoundwa haitahusika na kesi za jinai na kwamba haitakuwa na utaratibu wa kutoa hukumu kama zile za kukatwa mikono kwa wezi na za watu kupigwa mawe hadi kufa ambazo zimekuwa zikitumika katika mataifa yanayofuata Sheria za Kiislamu (Sharia).

Hata hivyo, aliwaomba viongozi wa dini kuacha kukashifiana na kubainisha kwamba njia bora ya kufikia malengo ya mafanikio ni kupitia meza ya mazungumzo huku akiwataka kutimiza wajibu wao bila woga wala kuoneana.

Aliwataka viongozi wa dini zote kurejesha utaratibu wa mazungumzo katika meza moja na kubainisha kwamba nguvu ya dola inatumika pale amani inapotoweka.

Aliipongeza BAKWATA kwa utaratibu bora wa kila mwaka kuwapeleka Makka Mahujaji na kuwatia moyo waendeleze utaratibu huo ili ifike mahali baraza hilo liwe chaguo la hiyari la mahujaji.

Kuhusu mchakato wa kupata Katiba mpya, aliwataka viongozi wa dini zote kuwahamasisha waamini wao kushiriki bila kuwepo kwa ushabiki wa kidini na kusema suala hilo linawezekana iwapo viongozi hao wataamua na kuifanya Tanzania kuendelea kuwa kisiwa cha amani.

Alitumia fursa hiyo kuwaonya waumini wa Kikristo na Kiislamu kutougeuza mjadala wa mabadiliko ya Katiba kuwa mdahalo au malumbano ya kutaka kuingiza masilahi ya dini hizo mbili ndani ya katiba.

Akizungumzia tatizo la dawa za kulevya, Rais Kikwete alisema tatizo hilo lipo kila mahali, hivyo serikali imejipanga kukabiliana nalo huku akiomba ushirikiano kwa viongozi wa dini ambao miongoni mwao wanahusika.

Akionyesha namna tatizo hilo linavyokua, alisema wafanyabiashara hao wameshaanza kuwalenga vijana wa vijijini, ambapo iwapo hatua za kudhibiti hali hii hazitachukuliwa, hasa na viongozi wa dini, basi tatizo litazidi kuongezeka na kukithiri.

“Ni tatizo la kweli, hakuna mji ulionusurika, sasa hivi wanakwenda kuwauzia vijana wa vijijini…kazi iliyo mbele yetu ni ushirikiano mkubwa kati ya viongozi wa dini na waumini wao.

Alitumia fursa hiyo kuwajibu viongozi wa dini akiwamo Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Polycarp Kardinali Pengo, ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakimtaka awataje hadharani viongozi wa dini aliosema wamekuwa wakijihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Akirejea kauli alizopata kuzitoa katika maeneo mawili tofauti ya Kanisa Katoliki, Rais Kikwete alisema alifanya hivyo kama njia ya kutoa rai na tahadhari baada ya kupata taarifa ambazo zimekuwa zikiwataja viongozi wa dini kuwa miongoni mwa wafanyabiashara wa dawa za kulevya.

“Nilisema hili kama tahadhari, tumewakamata masheikh, wachungaji, maalhaji. Mmoja alikuwa anakwenda Brazil akakamatwa na kesi ipo mahakamani. Sikusema maaskofu bali watumishi wa Mungu…maaskofu na viongozi wa dini, niliwaomba tushirikiane..Nikaona wengine wanachukia,” alisema Kikwete pasipo kutaja jina la kiongozi yeyote wa dini.

Alisema wito wake huo kwa viongozi wa dini haukuwa na lengo la kuwakejeli au kuwashutumu bali alifanya hivyo kutokana na kutambua namna walivyo na uwezo wa kuvuta hisia za watu wengi wanaohudhuria mahubiri yao.

“Sikuwakejeli wala sina sababu ya kuwakejeli viongozi wa dini, sasa hili mkiliona baya wenzangu mnanikatisha tamaa na ninyi mnasikilizwa kwa sababu mna uwezo wa kukusanya watu wengi, mkawahubiria wakawaelewa,” alisema.


Hisani ya Tanzania Daima.

Tuesday, August 30, 2011

URBAN PULSE CREATIVE 2011

URBAN PULSE inawaletea video fupi ya Notting Hill carnival iliyofanyika jumapili 28.8.11
Asanteni,


URBAN PULSE CREATIVE wakishiriana Miss Jestina Blog


WELCOME 2THE NGORONGORO CONSERVATION AREA NA SERENGETI PIA.

The Ngorongoro Crater is often called ‘Africa’s Eden’ and the ’8th Natural Wonder of the World,’ a visit to the crater is a main drawcard for tourists coming to Tanzania and a definite world-class attraction. Within the crater rim, large herds of zebra and wildebeest graze nearby while sleeping lions laze in the sun.

G.Sengo looking at the Mbuga'z...
At dawn, the endangered black Nyumbu'z returns to the thick cover of the crater forests after grazing on dew-laden grass in the morning mist. Just outside the crater’s ridge, tall Masaai herd their cattle and goats over green pastures through the highland slopes, living alongside the wildlife as they have for centuries.

Tembo aka Elephant is the largest living land animals on Earth today. This male weighed about 11,000 kg.

Tembo na misafara yao.

Twiga (Girafe).

Kiboko na wenzie' basi tuwaite Viboko kwasababu wako wengi.

Swala.

Ukungu, umande yaaani ni full baridi humu mbugani.

Katika eneo hili la Hotel ya Serena iliyozungukwa na maadhari ya aina yake ya kuvutia, kila utakachokitizama kitakuwa na mvuto kwa macho yako, ardhi, nyasi, miti, utunzaji wa mazingira ololooo!

Kama Directory vile.

The Ngorongoro Crater and the Ngorongoro Conservation Area are without a doubt some of the most beautiful parts of Tanzania, steeped in history and teeming with wildlife.

Nikiwa Ngorongoro Serena Lodge.

Much respect kwa mwongoza huu msafara Dreva Abdul 'Masafari' aliyekuwa akinimwagia maifomesheni', mahistoria ya pori na makila kingafrengwa.

Lango kuu kuingia Hifadhi ya Taifa Serengeti National Park A Word heritage Site.