ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, August 6, 2011

2'PRE SEASSON YA TOTO KUELEKEA LIGI KUU.

Timu ya toto ya jijini Mwanza leo tena imeendeleza wimbi lake la ushindi kwenye mechi zake za Pre' season ya Tz Premium League mara baada ya kutandaza kichapo kingine cha mabao 5-0 kwa timu ya TSC ya jijini Mwanza.

Magoli ya Toto Africans yamefungwa na Chika Chukwu, Salum Kamana na Ariwodo Darlington aliyepiga 3.

HAYA USAFI NA AFYA ZETU JEH!

Mfanyakaizi wa moja ya makampuni ya uzibuaji maji taka Mwanza akiwa na vifaa vyake vya uzibuliaji begani na mikono chukuchuku.

Wakusanyaji taka katika dampo la furahisha jijini Mwanza.

Upungufu wa usafi wa mazingira ni sababu kuu ya maradhi duniani kote. Uboreshaji wa mazingira una manufaa kubwa kwa athari za afya ya wote katika kaya na katika jamii. Ila tujiulize jeh wakusanyaji taka wetu (wafanya usafi) pamoja na wenzao wote wa mlengo huo wa kufanikisha hatua za usafi jeh! wanavitendea kazi vinavyozilinda afya zao?

NAPE ATEMBELEA CLOUDS MEDIA GROUP

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akizungumza na baadhi ya viongozi na waandishi wa Clouds Media Group alipotembelea ofisi za kampuni hiyo Mikocheni Dar es Salaam, leo. Wapili kushoto ni Mkurugenzi Mwendeshaji wa Kampuni hiyo, Ruge Mtahaba akimsikiliza kwa makini.

Nape akionyeshwa na Ruge Studio za Clouds Tv zilivyo za kisasa.

Cathbert Kajuna mtayarishaji wa jarida la Kitangoma linaloandaliwa na kampuni hiyo, na pia ni mmiliki wa blog ya KAJUNA (HABARI NA MATUKIO) akimkabidhi Nape nakala ya jarida hilo alipoingia katika ofisi za utayarishaji wa jarida hilo ambalo ni miongoni mwa majarida yanayosisimua sana hapa nchini. Katikati ni Ruge Mutahaba.

Mkurugenzi Mtendaji wa Cloud Media Group, Joseph Kusaga (kushoto) akisalimiana na Nape wakati wa ziara hiyo. Katikati ni Ruge.

Ruge akiagana na Nape mwishoni mwa ziara hiyo.

Picha na habari kwa hisani ya KAJUNA

RAMADHANI KAREEM

Baadhi ya wafanyakazi wa Villa park wakishiriki futari iliyoandaliwa maalum kwao na wadau wao wa karibu. Blogu hii inawatakia kheri na fanaka waislamu wote katika kipindi chote hiki cha mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Friday, August 5, 2011

PRE SEASSON YA TOTO KUELEKEA LIGI KUU.

Casto Mumbala wa Toto (11) akijaribu kumtoka Maxwel Anthony wa Tinsela.
Katika kujiandaa na mikikimikiki ya ligi kuu soka Tanzania bara Wanakisha Mapanda wa jijini Mwanza Toto Africans katika mechi yake ya kirafiki jioni ya leo wameikandamiza bila ya huruma timu ya Tinsela toka wilayani magu bao 4-0.

Katika mchezo huo huo wa nguvu na wakuvutia uliosheheni kosakosa nyingi magoli ya Toto yalifungwa na Casto Mumbala, Emma swita (bao la pili na la tatu) na bao la nne lilitupiwa nyavuni nae Salum Kamana.

Magoli ya Tinsela yamefungwa na Amani kipanya pamoja naye Maxwel Anthony. Kesho jumamosi timu ya Toto itashuka dimbani katika mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya Tanzania Soocer Academy ya jijini Mwanza.

Thursday, August 4, 2011

NCHI IMEINGIWA GIZA AU TUNAIGIZA?

Aaaaaah-Kumbe!!

Mwananchi wa kawaida alikuwa akisikiliza yanayojiri mjengoni lakini mwisho wa siku baada ya tathimini zake aliamua kuongeza neno kwenye bango la mgenjo kisha akasepa zake!!

Mhhh tutaona mengi awamu hii nchi imekuwa kama familia ya kambale kila mmoja ana sharubu!!

Wafanyabiashara kuwa na sauti kuliko serikali.

AIRTEL YATOA MSAADA WA VYEREHANI 10 KWA VIKUNDI 3 VYA WATOTO YATIMA DAR ES SALAAM

Meneja Huduma za Jamii wa Airtel, Tunu Kavishe (kulia) akishikana mikono na motto yatima, Zena Mohamekatika hafla ambayo Airtel ilikanodhi msaada wa vyerahani 10 kwa vikundi vitatu vya wanawake vya kulelea watoto yatima vya Msasani, Kawe na Kinondoni, Jijini Dar es Salaam jana.

Meneja Huduma za Jamii wa Airtel, Tunu Kavishe (kushoto) akikabidhi moja ya mashine za kushonea, cherahani, kwa mwakilishi wa kikundi cha wanawake cha kulelea watoto yatima cha Kawe Huruma Group , Hilda Rwebangira.

Meneja Huduma za Jamii wa Airtel, Tunu Kavishe (kushoto) akikabidhi moja ya mashine za kushonea, cherahani, kwa mwakilishi wa kikundi cha wanawake cha kulelea watoto yatima cha Msasani Womens and Orphans Centre, Yonnes Kihiyo katika hafla hiyo.

KAMPUNI ya simu za mikononi ya AIRTEL imetoa msaada wa vyerehani kumi kwa vikundi vitatu vya wanawake vinavyolea watoto yatima jijini Dar Es Salaam ili kuviongezea uwezo wa kulea watoto wanaolelewa katika vituo hivyo. Msaada huo umekabidhiwa na meneja huduma za jamii wa airtel Tunu kavishe kwa vikundi hivyo. Vikundi vilivyofaidika na msaada huo ni kikundi cha wanawake cha kulea watoto yatima cha Msasani, kikundi cha Huruma cha Kawe pamoja na kile cha kulea watoto yatima cha Kinondoni.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Bi.Kavishe alisema "AIRTEL itaendelea kugawa misaada kwa vikundi vya wasiojiweza ikiwa ni sehemu ya kampeni yake ya kusaidia jamii katika kutatua baadhi ya matatizo ambayo inayakabili hususani katika sekta ya elimu". Akipokea msaada huo wa mashine za kushonea, mwakilishi wa kikundi cha wanawake cha kulelea watoto yatima cha Msasani Womens and Orphans Centre, Prudencia Kibatara alisema " Msaada huu utatusaidia katika kuboresha utoaji wa huduma kwa watoto hawa ambao tunawahudumia katika vituo vyetu. Tunachangamoto nyingi ikiwemo idadi kubwa ya watoto na kipato kidogo cha uendeshaji vikundi hivi, hivyo tunawapongeza sana Airtel kwa kushirikiana nasi katika kusaidia jamii. Kupitia cherehani hizi tutaanzisha madarasa ya ushonaji na ada zitakazolipwa zitatumika kusaidia watoto hawa, vilevile chereharani hizi zitatumika kushona vitambaa na mashuka ambayo yataleta pato katika vikundi na tutaweza hata kuendelea kuwasomesha watoto hawa vizuri" aliendelea kusema Bi Kibatara

Aidha Afisa mtendaji wa kata ya msasani .. Swai aliiipongeza kampuni ya simu ya Airtel kwa kujitokeza na kusaidia vikundi hivyo na kutoa angalizo kwa walezi wa vikundi hivyo kutumia msaada huo kwa manufaa ya watoto na si yao binafsi.

"Jamani wakina mama naomba huruma zetu za dhati ziendelee hakikisheni mnaendelea kutumia msaada huu mlioupata kama nyenzo ya kuendelea kuwatunza na kusaidia watoto hawa na sio kujifaidisha sisi wenyewe" alisema Afisa mtendaji wa Msasani .

..Leo Airtel wameonyesha jinsi wanavyojali jamii wanayoihudumia hivyo naomba tuwaunge mkono ili dhamira yao itimie" alimaliza kwa kusema afisa mtendaji...

Vituo vilivyopata msaada huo viko jijini Dar es salaam ambavyo kwa ujumla vyote vinalea watoto wasiopungua 40 kila kimoja. Watoto wanaolelewa katika vituo hivyo bado wanamahitaji mengi japo kampuni ya simu za mkononi airtel imeweza kujitolea msaada huo wa vyerehani bado pia wanahitaji vifaa vya shule, vifaa vya kujifunzia, chakula pamoja na malazi ya kila siku.

Airtel imekuwa mstari katika kusaidia uboreshaji wa maisha ya jamii kwa kutoa misaada ya aina mbalimbali na kudhamini shughuli za miradi ya maendeleo.bado Airtel inampango wa kutoa msaada wa cherehani pia katika mikoa ya mwezi huu kwa dhumuni la kuendelea kupunguza tatizo la kipato kwa vituo vya wananchi wanaoishi katika mazingira magumu.
Mwisho

Wednesday, August 3, 2011

MUBARAK WA MISRI AKANA MASHTAKA

Aliyekuwa Rais wa Misri Hosni Mubarak amekana mashtaka ya rushwa na kuamuru kuuliwa kwa waandamanaji, siku ya mwanzo ya kesi yake iliyofanyika mjini Cairo.Bw Hosni Mubarak

Waandishi walisema, alipelekwa akiwa kwenye kitanda cha hospitali na kuwekwa ndani ya kizimba mahakamani humo, jambo lililowashtusha wengi waliokuwa nje.

Bw Mubarak mwenye umri wa miaka 83 anashtakiwa na watoto wake wawili wa kiume, ambao pia walikana mashtaka yanayowakabili, na pia aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani Habib al-Adly na waliokuwa maafisa wengine sita.

Hukumu ya kuamuru mauaji ya waandamanaji ni adhabu ya kifo.

Takriban askari na polisi 3,000 wamezambazwa kuhakikisha kuna utulivu katika chuo cha mafunzo cha polisi ambapo kesi hiyo inasikilizwa.

Awali ilikuwa isikilizwe kwenye kituo cha mkutano cha Cairo lakini mamlaka husika zikahamisha eneo na kuunda mahakama ya muda ndani ya chuo hicho kutokana na suala la usalama.

Inakadiriwa watu 600 walitazama kesi hiyo ndani na nje ya mahakama, na mamilioni ya wengine wengi wakitazama kupitia televisheni.

MAGEREZA MABINGWA WA NDONDI TAIFA

Mara baada ya kuahirishwa mara kadhaa hatimaye mashindano ya wazi ya Ubingwa wa Taifa kwa mchezo wa ngumi yaliyoanza jumatatu jijini Mwanza yamemalizika jana nao timu ya Magereza Dar es salaam kuibuka washindi wa jumla.Kaimu rais wa BFT mstaafu Meja Changarawe akikabidhi kombe la Ubingwa wa jumla kwa timu ya ndondi ya Magereza.

Jofray Timoth wa Temeke akipeleka sumbwi kwa Osward Chaula wa Magereza, ambaye alishinda kwa pointi 3 kwa 0 michezo yote ikichezwa kwa round mbili kila mmoja.

Ndondi za uzito wa kilogramu 56 Wigoro Katuba toka Nyamagana (kushoto) alimtandika kwa pointi 2-1 Undule Langsoni wa Magereza


Ndondi za Uzito wa kilogramu 49, Yahya Maliki wa Temeke aliibuka mshindi dhidi ya Antony Idoa wa Magereza kwa kumkunyuga kwa pointi 3-0


Hili ndilo dimba la ndondi Taifa 2011 Uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza.


Yona Segu v Nasser Mafuru

Ndondi za uzito wa kilogramu 60 kipute baina ya Nasser Mafuru wa Magereza na Yona Segu wa Temeke kiliisha kwa Yona kushinda kwa pointi.

Kaimu rais wa BFT mstaafu Meja Changarawe akikabidhi kombe la Ushindi nafasi ya pili kwa timu ya Nyamagana.

Kaimu rais wa BFT mstaafu Meja Changarawe akikabidhi kombe la ushindi ndondi nafasi ya tatu kwa Temeke.

Tuesday, August 2, 2011

FRIDAY NIGHT FREESTYLE SPECIAL SEASON 1(URBAN PULSE)

URBAN PULSE CREATIVE ikishirikiana na True Talk Records Company inapenda kuwaletea program mpya ya tv inayoitwa Friday Night Freestyle special. Hii ni Reality Programme yenye mchanganyiko wa ucheshi, ubunifu wa kushika Mic mtaani mbele ya kamera na kuonesha vipaji kutoka kwa wasanii waliopo hapa UK. Programme hii itarushwa kwenye TV Hapa UK na baadhi ya Nchi jirani za Ulaya. Vilevile kutakuwepo na zawadi mbalimbali kwa washindi na recording deal mwishoni mwa series

Asanteni

URBAN PULSE CREATIVE

HAMIA AIRTEL NGWASUMA YATIKISA SONGEA

Kiongozi wa bendi ya muziki wa dansi ya FM Academia 'Wazee wa Ngwasuma' Nyoshi El Sadat (wa pili kushoto) akiwaongoza wasanii wenzake katika kulishambulia jukwaa katika onyesho la 'Hamia Airtel Ngwasuma' lililofanyika mjini Songea na kudhaminiwa na Airtel mwishoni mwa wiki.

Msanii wa bendi ya muziki wa dansi ya FM Academia 'Wazee wa Ngwasuma' Pablo Masai akikonga nyoyo za wakazi wa mji wa Songea katika onyesho la 'Hamia Airtel Ngwasuma' lililofanyika mjini Songea na kudhaminiwa na Airtel mwishoni mwa wiki.

Wanenguaji wa bendi ya muziki wa dansi ya FM Academia 'Wazee wa Ngwasuma' wakifanya vitu vyao katika onyesho la 'Hamia Airtel Ngwasuma' lililofanyika mjini Songea na kudhaminiwa na Airtel mwishoni mwa wiki.

Baadhi ya wapenzi wa muziki mjini Songea wakiselebuka katika onyesho la 'Hamia Airtel Ngwasuma' lililofanyika mjini Songea na kudhaminiwa na Airtel mwishoni mwa wiki.

CELEB COUPLE HEIGHT MISMATCHES

Shaquille Neal & Nicole Alexander

Kim Kardashian & Kris Humphrey

Kylie minogue & Andres Velencoso

Will Smith & Jada Pinkett Smith

Jessica Simpson $ Eric Johnson

Khloe Kardashian & Lamar Bodom

Holmes Band & Frorida

Sacha Baron & Cohen Isla Fisher

Monday, August 1, 2011

WENGI TUNAJUWA UMUHIMU WA MATUNDA KIAFYA LAKINI..


Matunda mazuri ni yale yaliyoivia mtini na matunda ni vyema yakaliwa na kambakamba zake na siyo kuchujwa kama wengi tufanyavyo.
Matunda na mbogamboga ni muhimu sana kwa afya, haya-haya sasa tununue na tule!! KWANI TUNAJUA UMUHIMU WAKE. Kwani wewe hujui umuhimu wa matunda na mbogamboga kwa afya yako?

WOW!!! ....SERENGETI FIESTA 2011 DAR ES SALAAM


PICHA ZOTE KWA HISANI YA AHMAD MICHUZI WA JIACHIE BLOG NA CUTHBERT ANGELO WA HABARI NA MATUKIO BLOG

IMETENGENEZWA NA
FREDY TONY NJEJE-MBEYA YETU BLOG