ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 30, 2011

TAQWA SEC MABINGWA AIRTEL RISING STAR KITUO CHA MWANZA

Kipa wa timu mabingwa Taqwa Sekondari Damian Paul(16) na makeke yake langoni.

Fainali ya Airtel Rising Star imefanyika leo jioni kwenye kituo cha mwanza viwanja vya Buswelu Sekondari ambapo leo kulikuwa na michezo miwili, mchezo wa kwanza umeshuhudia Mwanza Sekondari wakiibuka nafasi ya tatu mara baada ya ushindi wa bao 1 dhidi ya Buswelu sekondari goli likipatikana kwa njia ya penati (pichani) mfungaji akiwa ni Selemani Ibrahimu aliyefanikiwa kumhadaa kwa ufundi kipa wa timu pinzani.

Mabingwa Taqwa Sekondari.

Aka Chicharito mchezaji wa Taqwa aliyekuwa mwiba kwa Nsumba.

Nsumba Sekondari.

Mchezo wa pili wa fainali ulikuwa ni kati ya Nsumba Sekondari na Taqwa kipute kilichoanza kwa kasi ya ajabu na ushindani mkubwa lakini hadi dakika za kawaida za mchezo zinamalizika ngoma droo 0-0 ndipo ikaamuliwa njia ya matuta iliipa ushindi Taqwa kwa penati 4-3, penati zilipigwa nane, nane.

SHERIA YA KUDHIBITI MAANDAMANO YAJA

Kauli za kuendelea na maandamamo mpaka kieleweke ambazo zimekuwa zikitolewa na baadhi ya viongozi wa Chadema zinaonekana kuikera Serikali na sasa inakusudia kuifanyia marekebisho sheria husika ili kuyadhibiti.Fredrick Werema
Akichangia hotuba hiyo juzi kabla ya kuahirishwa kwa Bunge kwa ajili ya mapumziko, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema alisema mabadiliko hayo ya sheria yatalenga kuzuia bughudha katika maeneo ambayo watu hawashiriki maandamano husika.

Maandamano ni miongoni mwa mambo ambayo yalitawala mjadala wa siku mbili bungeni wa hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, iliyowasilishwa hivi majuzi na Waziri Shamsi Vuai Nahodha

"Tunadhani kuna haja ya kurekebisha sheria ili kuregulate (kudhibiti) maandamano katika maeneo ambayo watu si washiriki wa maandamano hayo, hili linawezekana maana nchi kama Ujerumani wamefanya hili," alisema Werema na kuongeza:

"Nimesikia hapa kauli mbalimbali zinazohamasisha maandamano na wengine wanasema tutaandamana mpaka kieleweke na wengine wanasema kutoka Mwanza mpaka Dar es Salaam, tunasema ndiyo ni haki ya kisheria, lakini lazima tuzingatie kwamba wapo wasiopenda maandamano haya."

Kadhalika, Werema alitumia nafasi hiyo kutoa somo kwa wabunge kuhusu mivutano iliyotokea bungeni siku chache zilizopita: “Peaneni nafasi kwa kila mtu na mwenzake na muwe na ushirikiano kama ambavyo mikono ya kushoto na kulia inakuwa na ushirikiano mzuri.”

Jaji Werema aliwaambia wabunge kuwa kazi ya kuwakilisha wananchi inahitaji uvumilivu kuliko kazi nyingine na akawataka wabunge wa pande zote kutumia lugha za kistaarabu wanapo kuwa ndani ya ukumbi wa bunge.

Hata hivyo, alikemea tabia za baadhi ya wabunge kutumia lugha za maneno makali akitolea mfano wa hotuba ya Msemaji wa Kambi ya Upinzani Bungeni kuhusu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi... “Ni kweli Mheshimiwa Lema (Godbless) alitumia lugha kali kidogo.

Hapa naomba ifahamike hivyo, lakini yote mimi ambaye ni Mwanasheria wa Serikali nasema muendelee kuvumiliana na kuangalia lugha za kutumia. Namshukuru sana Mheshimiwa Lukuvi (William), katika hotuba ile alitaka kusimama amzuie Lema, lakini nikamwabia muache aendelee kwani kuna njia nyingi za kuzungumzia hivyo akimaliza utaomba mwongozo.’’

Alisema kuwa katika suala lile yeye (Werema) akiwa Mwanasheria Mkuu, ndiye mwenye dhamana ya kulisemea jambo hilo.


Habari zaidi tembelea:
www.mwananchi.co.tz

Friday, July 29, 2011

AIRTEL RISING STARS KITUO CHA DAR

Mshambuliaji wa timu ya soka ya Shule ya Sekondari Msongola, Hamisi Juma, akichanja mbuga kuelekea goli la wapinzani wao, wakati wa mchezo wa nusu fainali wa ligi ya soka ya vijana chini ya miaka 17 kwa shule za sekondari ya Airtel Rising Stars, uliofanyika uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

Mshambuliaji wa timu ya soka ya Shule ya Sekondari Msongola, Ally Shaaban akiwatoka walinzi wa Alphonce Mathias (kulia) na Shukuru Mbaraka.

Mshambuliaji wa timu ya soka ya Shule ya Sekondari Msongola, Amos Juma (kushoto), akikabiliana na beki wa Jitegemee, Alphonce Mathias wakati wa mchezo wa nusu fainali wa ligi ya soka ya vijana chini ya miaka 17 kwa shule za sekondari ya Airtel Rising Stars, uliofanyika uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

Mshambuliaji wa timu ya soka ya Shule ya Sekondari Msongola, Amos Juma akizuiwa na kipa wa Jitegemee.

INTER ZEPHA TANZANIA LIMITED JIJINI MWANZA YATOA ZAWADI KWA MSHINDI.

Afisa mauzo na masoko wa Inter zepha Tanzania Limited Mr.Hamisi S. Fupi akitoa zawadi kwa mshindi.

Sehemu ya wanafunzi wa shule ya Pamba Sekondari ya jijini Mwanza walioshuhudia tukio hilo.

Washindi walioshinda katika Essay writing competition, kutoka kulia ni Renatus Hemed (head prefect) mshindi wa 3 ,Mayala P Mapinda mshindi wa 1 na Samwel J Mtiba mshindi wa 2.

Wanafunzi wakijumuika katika picha ya pamoja kumpongenza mshindi Mayala P Mapinda.

Inter zepha Tanzania Limited ya jijini la Mwanza imetoa zawadi kwa mshindi wa shindano la essay writing competition lililofanyika katika shule ya sekondari pamba ya jijini mwanza. Shindalo hilo lililo jumuisha wanafunzi wa kidato cha 5 na 6 baada ya kampuni kufanya Semina kuhusu ICT Aweaness iliyofanyika tar 15 july na kutoa zoezi la kuandika essay juu ya umuhimu wa tekinolojiya ya habari na mawasiliano katika elimu ambapo kampuni hiyoilitoa ahadi kutoa zawadi ya lap top kwa mshindi.

Interzepha inatoa pongezi kwa Mayala P mapinda wa kidato ya 5 CBG kwa kuwa mshindi la shindalo hilo.pia tunatoa shukurani za dhat kwa wanafunzi wote walioshiriki.

BIASHARA NI MATANGAZO

Kutangaza na blogu hii Tuwasiliane kupitia email ifuatayo:
albertgsengo@yahoo.com

KAMANDA WA WAASI AUAWA LIBYA

Kiongozi wa kijeshi wa waasi nchini Libya wanaokabiliana wakitaka kumpindua Kanali Muammar Gaddafi ameuawa, baraza la mpito la Libya limesema.Kiongozi wa baraza hilo Mustafa Abdul-Jalil amesema Jenerali Abdel Fattah Younes ameuawa na watu wanaomuunga mkono Gaddafi, na kiongozi wa watu hao tayari amekamatwa.

Amesema Jenerali Younes aliitwa kwenye mkutano ambapo alitakiwa aeleze kuhusu harakati za kijeshi, lakini aliuawa kabla ya kufika kwenye kikao hicho.

Taarifa zinasema kuwa Jenerali Younes alishukiwa kuwa na uhusiano na majeshi yanayomuunga mkono Gaddafi. Jenerali Younes ni waziri wa zamani wa mambo ya ndani ambaye alikimbia na kujiunga na upande wa upinzani mwezi Februari.

Wasaidizi wawili wa Jenerali Younes, Kanali Muhammad Khamis na Nasir al-Madhkur, pia waliuawa kwenye shambulio hilo, Bwana Jalil alisema.

Taarifa ambazo hazikuweza kuthibitishwa zilisema kuwa Jenerali Younes na wasaidizi wake wawili walikamatwa mapema siku ya Alhamisi katika eneo la kaskazini mwa Libya. Mapema siku ya Alhamisi, waasi walisema kuwa wameteka mji muhimu wa Ghazaya karibu na mpaka wa Tunisia, baada ya makabiliano makali na vikosi vya Kanali Gaddafi.
Abdel Fattah Younes alimuasi Gaddafi na kujiunga na waasi.


kwa hisani ya bbc swahili

NDUI NA UTANZANIA

NO. 1

NO. 2

NO. 3

NO. 4

Thursday, July 28, 2011

MRISHO NGASA v MANCHESTER UNITED (pt 2)


Mtanzania Mrisho Ngassa siku aliposakata kabumbu dhidi ya Manchester United wakati akifanya majaribio na timu ya Seattle Sounders ya Marekani.

Wednesday, July 27, 2011

AIRTEL YAENDELEA KUGAWA ZAWADI YA JIVUNIE PROMO

Meneja Uhusiano wa kampuni ya simu za mkononi ua Airtel Tanzania, Jackson Mmbando (katikati) akikabidhi funguo za gari mpya aina Corolla kwa Yohana Athumani Ntile wa Igunga Tabora aliyeibuka mmoja wa washindi wa promosheni ya Jivunie iliyomalizika hivi karibuni. Hafla ya makabidhiano ilifanyika jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni mmoja wa maofisa wa Kitengo cha Masoko cha Airtel, Alice Paulsen. Airtel kwa sasa inaendelea na promosheni yake kabambe ya Kwanjuka ambayo mteja hutuma neno kwanjuka kwenda namba 15656 ambapo mteja anaweza kushinda shs milioni moja kila siku, tano mwisho wa wiki na shs milioni 50 mwisho wa promosheni.

Mshindi wa promosheni ya Jivunie iliyokuwa ikiendeshwa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel mkazi wa Igunga Tabora, Yohana Athumani Ntile akipunga mikono mara baada ya kukabidhiwa gari lake jipya aina ya Corolla na Meneja Uhusiano wa kampuni hiyo, Jackson Mmbando (kushoto) jijini Dar es Salaam jana. Airtel kwa sasa inaendelea na promosheni yake kabambe ya Kwanjuka ambayo mteja hutuma neno kwanjuka kwenda namba 15656 ambapo huweza kujishindia shs milioni moja kila siku, tano mwisho wa wiki na shs milioni 50 mwisho wa promosheni.

Mshindi wa promosheni ya Jivunie iliyokuwa ikiendeshwa na Airtel, mkazi wa Igunga Tabora, Yohana Athumani Ntile akijaribu gari lake baada ya kukabidhiwa na Meneja Uhusiano wa kampuni hiyo, Jackson Mmbando (hayupo pichani) jijini Dar es Salaam jana. Airtel kwa sasa inaendelea na promosheni yake kabambe ya Kwanjuka ambayo mteja hutuma neno kwanjuka kwenda namba 15656 ambapo huweza kujishindia shs milioni moja kila siku, tano mwisho wa wiki na shs milioni 50 mwisho wa promosheni.

AIRTEL RISING STAR MWANZA YAANZA RASMI LEO

Michuano ya Airtel Rising star kwa mkoa wa Mwanza imeanza rasmi leo viwanja vinavyotumika ni uwanja wa Buswelu Sekondari, Michuno ikifunguliwa nae mkuu wa mkoa wa Mwanza Abbas Kandoro ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi hapa akiikagua timu ya Taqwa Sekondari.


Mgeni rasmi akikikagua kikosi cha Buswelu Sekondari.

Katika mchezo huo wa pili Taqwa waliondoka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji Buswelu (pichani).


"Mcheze mpira mzuri, uliojaa ushindani pamoja na ufundi mkiwa na nidhamu ndani yake, kumbukeni kuwa siyo wote mtaenda ngazi ya taifa bali ni vijana sita hivyo itumieni vyema nafasi hii kuiwakilisha Mwanza na sehemu yake ya ajira kwa zama zijazo. Kila mmoja acheze akiweka nadhiri moyoni mwake kuwa MIMI LAZIMA NIWE KATI YA WALE SITA" @Mkuu wa mkoa wa Mwanza Abbas Kandoro.

Kwenye mchezo wa awali leo nayo Nsumba Sekondari imeibamiza timu yenye majigambo mengi vijana wa mjini Mwanza Sekondari 1-0


Taqwa Sekondari ( red) wakipeleka mashambulizi langoni mwa Buswelu Sekondari hekaheka zilizozaa bao la ushindi.

Ni soka na NIDHAMU yake.

Kwa mujibu wa mratibu wa mashindano hayo mkoa wa Mwanza Job Mushumba amesema kuwa michezo ya ligi hiyo katika hatua inayofuata itachezwa kwa njia ya mtoano yaani Fist looser kucheza na Second looser kupata mshindi wa tatu na First winner kucheza na Second winner kumpata bingwa wa kituo cha Mwanza,

Michezo yote hiyo inataraji kuchezwa jumamosi ya wiki hii kiwanja nitakwambia papahapa.

Tuesday, July 26, 2011

WEZI WA MAFUTA YA MELI WANASWA MWANZA

Wafanyabiashara wa vyombo vya usafiri majini kupitia ulinzi shirikishi kwakushirikiana na jeshi la polisi Mwanza hivi majuzi katika eneo la Mwanza South wamefanikiwa kukamata watu wanaojihusisha na biashara haramu ya wizi wa mafuta kwa meli zinazopaki mara baada ya kutoka safari.

Chini ya ulinzi: Kulia ni mfanyakazi wa meli hiyo

Mchezo huo mchafu ulistukiwa na mfanyabiashara maarufu jijini Mwanza bwana Kitana, ambaye pia ana miliki vyombo vya usafirishaji na uvuvi ziwani Victoria, mara baada ya kuona mazingira yasiyoeleweka alito taarifa kwa wamiliki wa meli ya Mv. Allez ambao kwa haraka walipanga mchakato wa mtego na siku iliyofuata walifanikiwa kushuhudia wizi huo mwanzo mwisho live bila chenga jinsi unavyochezwa.


Mpira wa kufyunzea mafuta hupita njia hii hadi chini kwenye injini.

Watuhumiwa hao katika mahojiano wamesema kuwa wamekuwa wakijihusisha na mchezo huo kwa kipindi kirefu wakishirikiana na wafanyakazi wa meli hiyo nao hufanya zoezi hilo nyakati za usiku pindi meli zinapotoka safari, kwa kufyonza mafuta yaliyosalia mara baada ya meli kutoka safarini na hili hufanyika kabla meli haijaandikiwa mafuta kwa safari inayofuata.


Mpira wa kufyonzea ukiwa kwenye chanzo (matanki ya mafuta) melini.

Wezi hao wakiwa na boti yao maarufu yenye jina la upako ‘ASANTE MUNGU’ waliokutwa wakifyonza mafuta hayo kiulaini, huku jumla ya madumu 140 yakinaswa mengine yakiwa tayari yameshibishwa mafuta huku mengine yakiwa kwenye foleni.


Watuhumiwa wakiwa sambamba na mtuhumiwa namba moja mfanyakazi wa meli hiyo (wa tatu kutoka kushoto)

Wizi wa mafuta umekuwa kero kubwa nao ukilalamikiwa sana na wamiliki wa vyombo mbalimbali vya usafirishaji ziwani Victoria hasa wamiliki wa TRC, Kampuni ya Marine Services.

Monday, July 25, 2011

NKOME FC MABINGWA WA MANSOOR JIMBO CUP

Timu ya soka ya Nkome fc kutoka kata ya Hungumalwa wilayani Kwimba mkoani Mwanza imekuwa timu ya kwanza kutawazwa kuwa mabingwa wa kwanza kwenye michuano ya kwanza ya Mansoor Jimbo Cup iliyoanzishwa rasmi mwaka huu.

Pamoja na kukabidhiwa kombe la ubingwa pia timu hiyo imejizolea kitita cha shilingi 500,000/= seti moja ya jezi na mpira mmoja..

Kwaniaba ya timu yake kapteni wa Ngano fc toka kata ya Ngudu akipokea zawadi ya mshindi wa pili ambayo ni Jezi seti moja na kitita cha shilingi 300,000/= toka kwa mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya Kwimba bw. Christopher Kangoye, kutoka kushoto ni katibu wa CCM wilaya ya Kwimba Petronila Kichele, Mkuu wa wilaya, katibu Mwenezi Ledenta Majigwa na Mwenyekiti wa chama cha mpira wa miguu wilayani Kwimba (KWIDEFA) Michael Matola.

Tuzo rahaaaa.... Hapa ni kocha wa timu ya Mwahobha Fc akichekelea tuzo iliyozawadiwa timu yake kama Timu yenye nidhamu mashindanoni.

Washindi wa tatu ni Polisi Ngudu ambao walipata zawadi ya shilingi 150,000/= Lengo la kuanzishwa kwa Mashindano haya ni kuibua na kukuza vipaji jimbo la Kwimba, Kukutanisha wananchi katika suala zima la Umoja na kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kuhusu ukuzaji wa Michezo.