ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 4, 2011

CLUB LIPS MWANZA UMESHAWAHI ZUKAaaaa?

ISAMILO LODGE MWANZA.KWA MALAZI NA CHAKULA CHA UHAKIKA WAKATI WA KAZI NA MAPUMZIKO, KUMBI ZA MIKUTANO ZA KISASA NA SHEREHE MBALIMBALI ZIKIWEMO HARUSI, BONGE LA DISCO CLUB LA KIMATAIFA LENYE KILA SIFA SEKTA ZOTE ZIMEKAMILIKA.

HAPO SHIMONI PANAITWA CLUB LIPS.

RATIBA NI HII:-
JUMATANO – USIKU WA MWAFRIKA
IJUMAA – FLASHBACK NA NGOMA ZOTE ZA KISASA
JUMAMOSI – NGOMA ZOTE ZA UKWELI KATIKA DJ MIX
JUMAPILI – CLUB LIPS ITAKUKUMBUSHA MANGOMA YA LONG TIME


SIKUTAKA KUAMBIWA Nimezuka mie LEO....

KWA WALE MABOB WANA CHEMBA YAO' MAALUM BILA KOKORO.

WAPENDA KANDANDA KUNA BIG SCREEN MAANDHARI YA KIFAHARI NA YENYE KULIWAZA.

KIINGILIO NI SHS 5,000/-
WANACHUO WAKIJA NA KITAMBULISHO NI SHS 3,000/-

TUKUTANE PALE.......

ISAMILO LODGE EXPLORE THE MAGIC OF ROCK CITY.

Thursday, March 3, 2011

XCLUSIVE TRACK "UMECHAKACHUWA" BY

POLENI KWA UJENZI WA TAIFA NA NAAMINI MU WAZIMA WA AFYA TELE

STUDIO MPYA YA SEDUCTIVE RECORDS INAPENDA KUWAPA NAFASI WADAU, MARAFIKI NA WAPENZI WOTE WA MUZIKI WA BONGO FLEVA KUSIKILIZAA SINGLE YA PILI YA MSANII OCHU EDDY SHEGGY AU KWA JINA LA KISANII OCHU

SINGLE HIYO INAITWA "UMECHAKACHUWA" IMEREKODIWA NA PRODUCER JILLY BABY WA SEDUCTIVE RECORDS NA PIA IMESHAFANYIWA MUSIC VIDEO YAKE CHINI YA KAMPUNI YA EMPTYSOULZ PRODUCTION AMBAYO IMESHAANZA SAMBAZWA KATIKA VITUO MBALIMBALI VYA TV.

NATUMAINI MTAENJOY KAZI HII NZURI NA PIA KUMPA SUPPORT MSANII HUYU AMBAYE ANAJARIBU KUENDEREZA SANAA HII ALIYOKUWA AKIIFANYA MAREHEMU BABA YAKE MSANII WA MUZIKI WA DANCE EDDY SHEGGY.

PIA USISITE KUANDIKA KUTOA USHAURI PALE UTAPOSIKILIZA SINGLE HII YA "UMECHAKACHUWA"

ASANTENI NA TUWE PAMOJA!

Regards:

Solomon Lamba

Bongo Flava meets Brooklyn Flava, featuring.....


For those who missed the concert on the 9th of february here is another chance to see a great collaboration of artists. Initially we were brought together through MDGFive.com and UNFPA's efforts to raise awareness about maternal health through music. This is an independent event organised by Caravan Records to challenge, renew and fuse two powerful youth cultures. Please spread the word. The concert will take place at Triniti on FRIDAY the 4th of March. 8PM-00AM
--
Kind Regards,

Caravan Records
MANAGEMENT
Tel: +255 763 822 022
E-mail: kichaamusic@gmail.com


www.myspace.com/mzungukichaa
www.reverbnation.com/mzungukichaa
www.youtube.com/nuttywhite
www.facebook.com/mzungukichaa
www.myspace.com/caravanrec
www.facebook.com/caravanrec
www.twitter.com/MzunguKichaa

MWILI WENYE SUMAKU.....

Kutana na mtoto mwenye umri wa miaka saba raia wa serbia anayefahamika kwa jina la Bogdan ambaye ameufanya ulimwengu kujiuliza kulikoni kutokana na uwezo wa mwili wake usio wa kawaida.

Kulingana na taarifa za Shirika la habari la nchi hiyo mwili wa Borgan unanasa vyombo vya chuma kama vile vijiko, visu, uma, nyembe, funguo, misumari vyote katika hali ya kushangaza kabisa.

Wanasayansi wanaumiza vichwa, wasipate jibu la haraka kuwa hali hii ya mwili wa binadaamu ya kujitengenezea sumaku inatoka wapi? ni kama kiroja hivi! Na cha kushangaza zaidi hata sahani, vyombo vya kioo na hata kiendesha mbali ‘remote control’ vinanaswa na mwili wake, mama yyangu!!...
Baadhi ya vitu anavyovinasa vingine wala si vya vyuma kama vile glasi, alisema mwanahabari mmoja wa Serbia.
Mmmmmh! Chunguza mjomba utabaini. Source: in.yfittopostblog

Wednesday, March 2, 2011

MKUU WA MKOA WA SHINYANGA AVUMISHIWA KIFO. BABA + MKUU WA WILAYA WAKANUSHA WASEMA YU HAI.

Siku ya jana hapa nchini zilizagaa Tetesi za kifo cha brigedia mstaafu dr Yohana Balele, vyombo vingi vya habari viliripoti juu ya taarifa hizo huku mitandao nayo ikitoa usaidizi wa kutosha kupenyeza kwa kasi ya ajabu taarifa hizo za majonzi.
Kupitia uvumi huo familia ya brigedia huyo mstaafu ambaye ni Mkuu wa mkoa wa Shinyanga siku nzima ya jana ilipata usumbufu kwa kupokea simu nyingi si kutoka kwa watu wa hapa nchini pekee bali hata watu kutoka mataifa ya mbali wakitaka kujua ukweli haswa na wengine kudiriki hata kutoa salamu za rambirambi kwa familia hiyo.

Taarifa za awali zilimtaja mkuu huyo kulazwa katika hospitali ya rufaa ya bugando ambako asubuhi ya leo blogu yako (gsengo) ilikwenda kuthibitisha ukweli na haikumkuta mkuu huyo. Lakini mara baada ya kufika hospitalini hapo mmoja wa wauguzi wa hospitali hiyo ambaye hakutaka jina lake litajwe akapenyeza taarifa kuwa mkuu huyo wiki takribani tatu zilizopita aliletwa hospitalini hapo kupatiwa matibabu ambapo alilazwa kwa siku mbili tu! na baadaye kuhamia nyumbani kwa mkewe Isamilo jijini Mwanza huko aliendelea kupatiwa matibabu.

NYUMBANI KWA MKE WA DR. BALELE, ISAMILO MWANZA.
Simon Mtemi Majola ambaye ni baba wa mkuu huyo wa mkoa ni moja kati ya watu niliowakuta nyumbani kwa mheshimiwa maeneo ya Isamilo, ambapo Mzee Majola amekanusha taarifa hizo za kifo na kusema kuwa Dr Yohana Balele yu hai akiendelea na matibabu nyumbani hapo ila kwa wakati huo siwezi kuonana nae kwani amepumzika chumbani kwake.

Nae kaimu mkuu wa mkoa wa Shinyanga Bi.Amina Masenza ambaye vilevile ni mkuu wa Wilaya ya shinyanga Mjini akiongea na Clouds fm amekanusha Uvumi huo. Ndugu wengi kutoka vijiji vya mbali na mikoa ya jirani wamefika nyumbani hapo mara baada ya kupata taarifa hizo za uvumi.

WAKATI HUO HUO chanzo cha 'UVUMI' huu unatajwa na vyanzo visivyo rasmi kuwa:- Umetokana na moja ya mikutano wa chadema kwenye vijiji vya mkoa wa Shinyanga ambapo Dr. Silaa alipokea ujumbe kutoka kwa mtu ambaye hakutajwa, ujumbe ukimtaja mkuu wa mkoa wa shinyanga Dr. Balele kufariki dunia hali iliyomlazimu kuvunja mkutano.

Blogu hii inamtakia matibabu mema na afya njema mkuu wa mkoa wa shinyanga Dr. Yohana Balele.

MASHETANI WEKUNDU WAFIA DARAJANI.

Frank Lampard.
Frank Lampard converted a penalty kick in the 80th minute, giving Chelsea a come-from-behind 2-1 victory over first-place Manchester United on Tuesday night that tightened the Premier League race.

Wayne Rooney scored in his third straight Premier League game for the first time in a year, putting United ahead in the 29th minute with a 25-yard shot that beat goalkeeper Petr Cech.


Sir Alex Ferguson was predictably livid after the controversial decision that ruined his night, but the simple fact is that Manchester United’s defeat to Chelsea on Tuesday was exactly what the English soccer season desperately needed.

Tuesday, March 1, 2011

NDOA BANDIA ZAONGEZEKA JP-POLISI...

Idadi ya ‘ ndoa bandia' zinazowahusisha raia wa kigeni ambazo zimefichuliwa na jeshi la Polisi kote nchini Japani kwa mwaka 2010 kuwa zilifikia 153 ikiwa ni ongezeko la asilimia 14.2 ikilinganishwa na mwaka uliopita. Takwimu hizi ni kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Shirika la Taifa la Polisi hapa Japani.


Polisi walichukua hatua malimbali ikiwa ni pamoja na kuuliza maswali, kukamata na kupeleka nyaraka kwa waendesha mashitaka dhidi ya watu 471 wakihusishwa na tuhuma hizo. Shirika hilo limesema kuwa Polisi wanafuatilia miendendo ya ndoa hizo ‘bandia ‘ zenye malengo mbalimbali kama vile kutengeneza mazingira ya kufanya uhalifu.Shirika hilo limesema kuwa baadhi ya raia wa kigeni walijihusisha na vitendo vya jinai baada ya kupata hati za vya ukaazi kwa hatua yao ya kufunga ndoa za raia wajapani huku vikundi vya kihalifu vikipata fedha kutokana nandoa hizi za kupanga.

MAANDAMANO YA CHADEMA YATINGA SHINYANGA.

Viongozi wa Chadema na wabunge wa chama hicho wakiwa wanaandamana mkoani Shinyanga huku akiwa ametanguliwa na vijana wa chama hicho Redbriged.

Wanafunzi wa shule ya msingi Jomu wakiwa katika maandamamo ya Chama cha Demokaria na Maendeleo yaliofanyika mjini Shinyanga jana huku wakiwa wameshikana na kuonesha alama ya Vidole viwili.

Mwenyekiti wa Chadema taifa Freeman Mbowe akisisitiza kuendelea na maandamano kumjibu Rais Jakaya Kikwete.

Aliyekuwa Mgombea ubunge jimbo la Shinyanga Mjini Shilembi Magadula Shilembi ambaye kutotangazwa kakwe mshindi kulisababisha vulugu kubwa katika mji wa Shinyanga na kuchomwa moto kwa ofisi za Halmashauri.

Mabango mbalimbali ya waandamanaji wa mkoa wa Shinyanga yakionekana kuwa na ujumbe mbalimbali kwa rais Kikwete.

(Picha zote na Frederick Katulanda)

WASANII WA MUZIKI NA FILAMU WACHANGIA MIL 76 WAATHIRIKA WA MABOMU GONGO LA MBOTO.

Waziri mkuu Mizengo Pinda akiwa katika picha ya pamoja na wasanii wa Filamu na wa Muziki wa kizazi kipya mara baada ya kupokea michango mbalimbali ya fedha na vitu vyenye thamani ya shilingi milioni 76 waliyoipata kutokana na tamasha walilolifanya mwishoni mwa wiki kuchangia waathirika wa mabomu wakatika eneo la Gongo la mboto jijini Dar es salaam. Kulia ni kaimu mkuu wa mkoa Mh. Sadik na kushoto ni Kamanda Kova, wa tatu kushoto ni mratibu mkuu wa tamasha hilo la soka kwa wasanii (GOLI) Bw. Ruge Mutahaba.

Picha ndogo msanii wa muziki wa kizazi kipya Mwana FA kwa niaba ya wasanii wote akiwasilisha hundi hiyo kwa mh. Waziri mkuu.

Monday, February 28, 2011

WAZIRI MKUU WA TUNISIA AJIUZULU.

Waziri mkuu wa Tunisia Mohammed Ghannouchi ametangaza kupitia televisheni ya taifa kuwa anajiuzulu- matakwa muhimu kutoka kwa waandamanaji.

Bw Ghannouchi mwenye umri wa miaka 69, anaonekana kuwa karibu sana na aliyekuwa Rais Zine al-Abidine Ben Ali tangu mwaka 1989, aliyeondoshwa madarakani mwezi uliopita.

Alisema, " Baada ya kutafakari kwa zaidi ya wiki moja, nikaanza kushawishika, na familia yangu iliniunga mkono, na hivyo kuamua kujiuzulu. Si kwamba nakimbia majukumu yangu; nimekuwa nikitimiza wajibu wangu tangu Januari 14." " Siko tayari kuwa mtu anayechukua uamuzi utakaoishia kusababisha vifo." "Kujiuzulu huku kutasaidia Tunisa, mapinduzi pamoja na maendeleo ya siku za usoni za Tunisia." Alisema.

Baada ya saa kadhaa mbadala wa Bw Ghannouchi alitajwa- Beji Caid Essebsi, mwenye umri wa miaka 84, ambaye aliwahi kuwa waziri wa mambo ya nje katika serikali ya marehemu Rais Habib Bourguiba.


Awali, polisi mjini Tunis walirusha mabomu ya kutoa machozi na risasi za onyo kutawanya maandamano ya hivi karibuni wakitoa wito wa kutaka serikali mpya na katiba mpya katika siku ya tatu ya ghasia.

WA HAPA HAPA...

Kirumba resort jiko maarufu la samaki choma.

Bei ya kiwese leo Rock city.

Kuna watu wawili katika picha hii Je! umewaona?

Barabara kuu kuelekea Musoma kwa akina muraa' hapa ni meneo ya Magu mbelembele, kwasasa daladala aina ya hiace zimepigwa bao na magari aina ya Noah.

KWAHERI RAFIKI..

Tangu 1975 hadi 2011 Ni siku za maisha yako na hatimaye siku ya jana (jumapili) ndugu jamaa na marafiki tulielekea katika kijiji cha Masanzakona wilayani Magu mkoani Mwanza, mahala ulipojenga nyumba yako kwa ajili ya mazishi. Namzungumzia Paul Kabara rafiki mcheshi aliyekuwa akisimamia jambo na kuhakikisha kuwa anapigana nalo mpaka mwisho wa matokeo. Mpendwa huyu alifariki siku ya ijumaa katika hospitali ya rufaa Bugando baada ya kuugua kwa muda.

Watoto wa marehemu wakiweka shada la maua kwenye kaburi la Baba yao.

Marafiki wa marehemu wakiongozwa na Mr. Bruno kulia wakiweka kwa pamoja wakiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu Paul Kabara.

Sehemu ya umati msibani nyumbani kwa marehemu. Shukurani kwa wote walioshiriki kwa hali na mali kufanikisha safari ya mwisho ya mpendwa wetu Paul Kabara, Mwenyezi mungu twakuomba ilaze mahala pema peponi roho ya marehemu.

Sunday, February 27, 2011

MAAFANDE WA MWANZA WAUAGA MWAKA NA KUUKARIBISHA 2011 NA BONGE LA SHEREHE LILILOFANYIKA KATIKA MOJA YA FUKWE ZA ZIWA VICTORIA

Polisi Jazz aka Wana Orch Vangavanga toka jijini Dar es salaam ndiyo walikuwa wamwaga burudani.

'Tukumbuke na kuzingatia viapo tulivyoapa' Kamanda S. Sirro ktk nasaha.

Makaribisho hayo ya mwaka mpya 2011 pia yalikwenda sambamba na utoaji wa Tunzo za shukurani kwa wadau walioshiriki kwa karibu katika kulisaidia jeshi la polisi Mwanza Pichani MNEC Mr Gachuma akipokea yake toka kwa mgeni rsmi mkuu wa mkoa wa Mwanza Abbas Kandoro.

Mambo ya maakuli yalikuwa si polepole 'full drafti'

Maafandez dadaz nao waling'ara!

Mc wa sherehe hiyo aliyeichangamsha ile kisawasawa Prince Baina Kamukulu akiikaribisha meza kuu kufungua muziki.

Flowers wakisebeneka na ile mipigo ya **Prakatatu-tantu-tantu, Prakatatu-tantu-tantu...***

Wau! maafisaa wa sheria nao Ndani'

Meza makini ya watu makini.

"Habari zenyu! mnakunywaa au mnatania, vipi vinywaji vimeishaa, tu-mi-ke-ni leo siku yetu" Kamanda Sirro alipita meza baada ya meza akikagua huduma kama zinasomeka.

Hapa ilikuwa ni kama ka-ligi hivi ka kushindana kucheza baina ya Kamanda Sirro na wafanyabiashara wawili maarufu jijini Mwanza Mr.Kihelya na Mr.Kitana. Basi wacha watu wajitume kukumbushia za enzi na enzi Dah!

ChiaaaaazZZz!

"Hebu njooni Tupige moja ya ukumbusho"

Ewaaa!!
Sherehe hii ya kufana ya Jeshi la polisi Mwanza kuuaga mwaka 2010 na kuukaribisha mwaka 2011 ilifanyika jana jumamosi katika fukwe za Yatch Club ikiwa na lengo la kukumbushana sera kuu ya umoja kwa jeshi hilo sambamba na umuhimu wa kushirikiana na wananchi katika kudhibiti na kuzuia uhalifu nchini.

'H BABA BURST BONGO MOVIES' BUBBLES'

Ali Kiba wa Bongo Fleva akitaka kumtoka beki wa Bongo Movie katika mechi iliyochezwa jana jioni katika uwanja wa Taifa jijini Dar.Bongo Fleva waibuka kidedea kwa ushindi wa mabao 2-0 yaliyotiwa kimyani na mshambuliaji H. Baba. Picha kwa hisani ya Othmani Michuzi.

Meya wa Manispaa ya Ilala Jelly Slaa akisalimiana na 'Muuaji' wa Bongo Movie H.Baba.

PICHA ZA VIKOSI KWA HISANI YA JIACHIE>Kikosi kamili cha Bongo Flava Fc.

Kikosi kamili cha Bongo Muvi Fc.

Katika matukio yaliyotengeneza historia kiwanjani hapo moja wapo ni mbwembwe za timu ya bongo Muvi wakiongozwa na kamati yao ya ufundi ikiongozwa na bi Mwenda, Mzee Chilo na wenzake. Dakika jinsi zilivyoendelea kusonga hali ilikuwa mbaya kwao kwani walionekana kukosa raha na kufadhaika mno kwa kichapo walichopokea, kama vile haitoshi mchezaji wao machachari Ben Kinyaiya ilikuwa ni kama kutia chumvi kwenye kidonda kibichi pale alipokosa penati. Dr. Mtitu wa Bongo Movie akikimbia na mpira huku beki wa Bongo Fleva akimfukuzia. Hadi mwisho Bongo Flava 2 Bongo Muvi 0. Mechi hii imefanyika kwa hisani ya kuwachangia watu waliopatwa na maafa/waathiriwa wa milipuko ya mabomu iliyotokea kambi ya Jeshi Gongo la mboto hivi majuzi.

HONGERA WASANII WA TANZANIA.