ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, January 14, 2011

FLY540 YAZINDUA SAFARI ZAKE MWANZA.

Mkuu wa wilaya ya Ilemela Said Amanzi akizindua rasmi safari za ndege ya shirika la FLY540 leo katika uwanja wa ndege wa Mwanza.

FLY540Tanzania itaanza rasmi safari zake kati ya Dar es Malaam na Mwanza siku ya jumatatu tarehe 24.jan.2011 ambapo itatoa huduma zake kila siku kasoro siku ya jumamosi tu.

FLY540Tanzania aim to play a leading role in the expansion of air travel service in Tanzania and the Eastern and Central African Region as a whole. The company's objective is to deliver value for money without compromising on safety and quality. It provide cheaper fares so that travel becomes affordable for more people.

Time for Kata fumua pilipili and test tube masala.

FLY540Tanzania, yenye ofisi zake kuu jijini Dar es Salaam zinapatikana Samora Avenue na matawi yake Arusha ni India Street jengo la Blue Plaza ile hali Mwanza Posta Road.

Suka wa jidege hilo lenye kutumia muda wa saa moja na dakika kumi kwa safari ya Dar-Mwanza, uwezo wa kubeba abiria 50 ni Kapteni Richard Shivogo(32).

Burudani ya ngoma asili kabila la wasukuma kutoka Bujora.

This flight operated on the CRJ- jet aircraft which comprises of 50 seats.

Godwin Gondwe mc wa shughuli alikuja na mwewe huo mpya na kurejea nao.

Meneja wa uwanja wa ndege wa Mwanza bi.Ester Madale akizungumza na vyombo vya habari.

FLY540Tanzania kuanzia jumatatu 24jan2011. itafanya safari zake kama ifuatavyo:- ASUBUHU-ndege itaondoka Dar at 0630hrs, na kuwasili Mwanza at 0745hrs, itaonndoka Mwanza 0815hrs na kufika Dar 0930hrs. Kwa JIONI-ndege itaondoka Dar at 1630hrs, na kuwasili Mwanza at 1745hrs, itaondoka Mwanza at 1815hrs na kufika Dar 1930hrs.

Thursday, January 13, 2011

HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA YATOA SIKU 5 KWA WAMACHINGA KUONDOKA KATIKATI YA JIJI.

Halmashauri ya Jiji la Mwanza limetoa siku tano kwa wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama wamachinga na mama lishe kuondoka katika maeneo ya katikaki ya jiji kwa vile wamekuwa wakivunja sheria ndongo ya mazingira na usafi namba 312 ya mwaka 2010 na sheria ya Mipango miji na Ujenzi Mijini.Tamko hilo limetolewa juzi na Meya wa Jiji la Mwanza Bw.Josephat Manyerere (Diwani wa Kata ya Nyakato Wilayani Ilemela) kwamba Halmashauri ya Jiji kwa kushirikiana na wakuu wa vilaya za Nyamagana na Ilemela, kikosi cha polisi na vyombo vingine Dola vitaendesha oporesheni kabambe ya kuwaondoa wamachinga hao waliotapakaa kila kona ya jiji wakifanya biashara holela.
Tamko hilo linaonekana kukinzana na lile la ruksa ya kuendelea kufanya biashara toka kwa Mbunge wa Nyamagana Ezekia Wenje (Chadema) alilolitoa siku chache zilizopita wakati akihutubia mkutano wa hadhara wa kulaani tukio la polisi kutumia nguvu kuwatawanya wafuasi wa Chadema Arusha katika mkutano uliofanyika viwanja vya Ngoko’s vilivyopo Kata ya Milongo jijini mwanza.
Meya Manyerere amefafanua kuwa kutokana na hadhi ya Jiji la Mwanza na kusifika kushika nafasi ya kwanza ya usafi kwa miaka mitano mfululizo, likitembelewa na wageni mbalimbali wa kitaifa na kimataifa ili kuilinda hadhi hiyo uongozi hawana budi kuwaondoa wamachinga na mama ntilie ambao wamekuwa kero na kusababisha kuziba barabara za watembea kwa miguu sambamba na kuacha uchafu kila maeneo.
Meya Amewataka wabunge na madiwani wa Jiji la Mwanza kuacha tabia ya kuwapotosha wananchi na badala yake wawe mstari wa mbele kuwaeleza ukweli na kuwaweka tayari kufuata taratibu na sheria zilizopo ili jiji la mwanza liendelee kuwa kioo katika suala la usafi na utunzaji mazingira.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza bw. Wilson Kabwe amewataka wafanyabiashara hao kuzingatia kanuni na sheria kwa kuondoka maeneo yasiyoruhusiwa kufanya biashara na kuelekea kwenye maeneo waliyopangiwa toka awali.

Maeneo yaliyotengwa kwaajili ya wafanyabiashara hao ni Kiloleli, Buzuruga, Kitangili, Nyegezi, Mlango mmoja, Mabatini na kwenye magulio katika maeneo ya Mkuyuni, Igombe, Sabasaba, Nyakato National, Kayenze, Kitangiri, Buhongwa, Mkolani, Igogo, Magomeni Kirumba na Igoma hii ni kwa kufuata siku kama ilivyopangwa na si vinginevyo.

Mdau ... UMESOMEKA!!..!!

Hi Sengo
hongera sana kwa kutufanya hata sisi tulio mbali na tanzania hususani mwanza kuelewa nini kinaendelea, nilikuwa na maombi yafuatayo nikiwa kama mfuatiliaji wa blog yako kila siku hata kama sicommet chochote lakini huwa lazima nifungue mara nyingi huwa najulikana kama bm.

1. kuna habari huwa unazianzisha lakini baadaye unatuacha kwenye mataa, mfano uliwahi kuandika bustani ya eden ndani ya mwanza lakini mpaka leo hatujui kama inaendelea kujengwa au mradi ulikuwa feki umekufa? uliwahi kusema machinga wataondolewa makoroboi kupisha kikwangua anga cjui ujenzi umeshaanza au vipi na ni hoteli, ofisi au shopping malls au vyote kwa mpigo na linamilikiwa na nani? ulisema ppf kuendelea kupendezesha mwanza kwa majengo, je kuna ujenzi wowote unaoendelea hapo mwanza ukiwa kama mradi wa ppf au nssf kwa sasa? ulitoa ramani ya soko mwanza je litaanza au limeshaanza kujengwa lini? rumours imevunjwa kunajengwa nini........ pamoja na mangine mengi. nafikiri ukiwa kama mwandishi wa habari unaweza hata kuongea na viongozi wa jiji wakakupa undani wa mambo yalivyo au ni wakali?

2. naweza kupata picha za chuo cha saut pamoja na maeneo mengine yanayojengwa kisasa mwanza mfano. kiseke, nyakato bwiru isamilo, nyegezi, capripoint, ilemela nk si lazima sana ila nikipata nitashukuru haina haraka sana hata kama itapita miezi kadhaa maana najua na wewe uko busy na hii ya blog unajitolea tu. hizo picha ni wewe mwenyewe uzpost au unitumie kwenye email kwangu vyovyote poa tu.

pole kwa maelezo mengi na ahsante kwa kazi unayofanya Mungu akubariki wewe na familia yako.

SIMBA YAIFUNGA YANGA: YATWAA MAPINDUZI.

"HAIJALISHI NI KATIKA MICHUANO GANI: kombe la mbuzi, mechi za mchangani, nje ya afrika iwe bara au visiwani KISASI NI KISASI TU!!" asema PJ wa Power Breakfast. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein akimkabidhi kombe la ubingwa wa michuano ya Mapinduzi nahodha wa Simba Sc Nicco Nyagawa baada ya timu hiyo ya mtaa wa Msimbazi jijini Dar kuilamba Yanga bao 2-0 katika mchezo wa fainali uliofanyika usiku wa kuamkia leo uwanja wa Amaan Stadium Zenji.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein katika pozi na kikosi cha Simba kabla ya mchezo.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein akipozi na kikosi cha Yanga kabla ya mchezo.

Simba na Yanga katika 'eksheni'.

Simba woyeeeeeeeeee…...Mashabiki wa simba hakuna kulala!!

Dakika ya 33 Mussa Hassan ‘Mgosi’ aliipatia Simba bao la kwanza baada ya kupokea pasi safi iliyopigwa kutoka wingi ya kulia na kuachia shuti kali lililomshinda kipa Yaw Berko wa Yanga na kujaa moja kwa moja wavuni. Bao la pili lililoiwezesha Simba kuibuka na ubingwa lilifungwa na Shija Mkina.

Shukran kwa Francis Dande.
Zanzibar.

Wednesday, January 12, 2011

1, 2, 3, 4 ....HATIMAYE THT YATIMIZA MIAKA 5.

Kituo cha THT (Tanzania House Of Talent) kimetimiza miaka 5 tangu kuanzishwa kwake, ndani ya maadhimisho yake yaliyofanyika usiku wa jana katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar, jumla ya wasanii sita wa kituo hicho walizindua album zao kwa pamoja.Hawa ndiyo waliozindua album zao ndani ya usiku huo. Kutoka kulia ni LINAH, BARNABA, MATALUMA, DITTO, MWASITI na AMINI hapa ni kabla ya kuingia ukumbini kwa shughuli.

Pichani ni msimamizi wa kituo cha THT Ruge Mutahaba, kulia mratibu wa mradi wa maralia mpango wa zinduka hapa nchini mama Sadaka Gandi wakijaribu kuweka mambo sawa mwanzo wa shughuli.

THT Dancers waliangusha burudani zaidi ya uwajuwavyo

Aliyetumika kung'arisha kibao kipya chake Sajna kiitwacho 'SITAKI TENA KUUMIZWA', namzungumzia mwanadada LINAH akiimba wimbo ATATAMANI, ambao ni moja kati ya zile kali zinazopatikana ndani ya album yake.

'BEST Vocalist' Banana Zahir Zorro nae alikuwepo kutoa sapoti kwa wana wa THT kutimiza miaka mitano.

HABARI NA PICHA ZAIDI TEMBELEA
www.michuzijr.blogspot.com
PICHA ZOTE KWA HISANI YA JIACHIE.

Tuesday, January 11, 2011

"UTOTO BWANA........."

"Mama nanihiii.... njoo umwone mwanao!" ile kufika tu!..anatupa macho, mtoto kajikandika mafuta usoni, viganjani, kichwani hadi kwenye nguo, kope za macho zinafunguka kwa mahesabu kutokana na wingi wa mafuta. !TOBA!
Upande wa nyuma wa kichwa nako...tu..tu-tu! Nibaraa! Naivuta picha kama bidhaa hii ingekuwa zile za kemikali ingekuwaje!? Ndomana bidhaa nyingi zilizo na kemikali au hata zisizo na kemikali, lebo zasema weka mbali na watoto.

KAMCHEZO KAPYA.
Mara zote michezo inawajengea watoto tunu njema kama umakini, utulivu, furaha, urafiki, ubunifu, kuchemsha bongo, kutulia nyumbani na mengine mengi.

TUWAPE NAFASI WATOTO KUCHEZA NA TUWE WAANGALIFU.

KWETU KWA WAZAZI.

Ilikuwa siku ya jumamosi ya tarehe 8.jan.2011 kaka yangu aliwasiliana nami kwamba anaelekea Mwanza na familia yake kwa likizo fupi na kusema kuwa kabla ya kufika Rock City atapitia kijijini kwetu pale Malampaka Shinyanga kwaajili ya misa fupi kwenye kaburi la marehemu baba yetu George Sospeter Sengo aliyeaga dunia mnamo mwaka 1988. Pichani mbele ni Aliyerithi jina la mzee ni mtoto George (wa bro Adam Sengo) mbele ya kaburi la babu yake. Nami ilinipasa kujumuika nao ingawa kuna misa kuu ya kifamilia tunayotegemea kuifanya siku za baadaye.

Japo kwa uchache familia yetu.

Brother Adam mbele ya kaburi la babu yetu Mzee Sospeter, kaburi lililopo hatua chache toka kaburi la marehemu baba.

Watoto wanapenda sana kujifunza kwa kuuliza maswali tena mengi ya kudadisi, hili nililiona kwa mtoto huyu wa braza ambaye nae aliomba kupiga picha ya kumbukumbu.

Hazina za kwetu milima ya mawe.

Wakati wa umiliki wa eneo hili kupitia Tajiri mmoja aliyekuwa mwekezaji wa magari yaliyokuwa na chata 'REHEMA YA MUNGU' namzungumzia Paul Ng'wani, Kituo hiki cha mafuta kilikuwa kinang'aa kisawasawa yaani hapa ndiyo penyewe, town centre babaake!.

Aya-ya-yaaa Fagia sana kiwanja hapo mbele... 'Home sweet home' nyumbani kwa Mzee Kaseko.

George na Nduguye mpya katika pozi.

Hiki ni moja kati ya kitaa kilicho shiriki kunikuza (just for three years). "Kiukweli kama neema imepotea hivi tofauti" nakumbuka Enzi hizo nyumba zilikuwa smati na hata kama za udongo zilinakshiwa na chokaa huku watu wakishindana kupanda maua mbele ya nyumba yaani full green. Lakini sasa MMMMh!

LIONEL MESSI MCHEZAJI BORA WA FIFA 2010.

Shirikisho la Soka duniani FIFA, limemtangaza mchezaji wa kimataifa wa Argentina, Lionel Messi kuwa mchezaji bora wa soka wa mwaka 2010.Messi scored more than any other player in Europe's top five leagues in 2010, with 42 goals in 36 La Liga games, as well as finishing top scorer in the Champions League in 2010 with 12 goals in 12 games. He totalled 60 goals for the year for club and country.

"To be honest, I didn't expect to win today, but it was already great to be here next to my two mates," Messi said as he accepted the award. "To win it makes it even more special.
"I want to share with all of my friends, my family, all the Barcelonistas and the Argentinians."
Xavi added: "This award is a triumph for the cantera and for the philosophy of the club. It is a moment to savour. We shall see what happens next season.
"My life wouldn't have changed with this award, and I will continue to play like I normally have. The Ballon d'Or remains in Barcelona and there is no problem with this."



Real Madrid coach Jose Mourinho had earlier been named FIFA World Coach of the Year for Men's Football. Mourinho won Serie A, the Champions League and Coppa Italia with Inter Milan in the 2009-10 season and has made an impressive start to life at the Bernabeu. "I'm the best coach in the world for 2010 because I was the coach of the best team in the world in 2010," he said. "We were a family and we continue to be a family. I continue to be part of it from afar. "I want Inter to win every game except those against my team."

:::::::MPANGO MZIMA WA TUZO NI KAMA IFUATAVYO:-
FIFA Men's World Player of the Year: Lionel Messi
FIFA Women's World Player of the Year: Marta
FIFA World Coach of the Year for Men's Football: Jose Mourinho
FIFA World Coach of the Year for Women's Football: Silvia Neid
FIFA FIFPro World XI of 2010: Iker Casillas; Maicon, Gerard Pique, Lucio, Carles Puyol; Xavi, Wesley Sneijder, Andres Iniesta; Cristiano Ronaldo, David Villa, Lionel Messi
FIFA Puskas Award: Hamit Altintop
FIFA Fair Play Award: Haiti Under-17 women's team
FIFA Presidential Award: Archbishop Desmond Tutu

Monday, January 10, 2011

WANAHABARI WALIPOTEMBELEA TBL.

Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia kiwanda chake kilichopo ilemela jijini Mwanza mwishoni mwa wiki ilitoa fursa kwa waandishi wa habari kutembelea kiwanda hicho kwa nia ya kujionea utayarishwaji na utengenezwaji wa vinywaji vyake.

Wanahabari wa walipata maelezo ya kina, hatua kwa hatua huku nao wakiuliza maswali mengi, mengi kama vile nao wanakwenda kuwa wajasiliamali kwa kuanzisha viwanda vyao.

Production juu kwa juu kiwandani hapo, Teknolojia ina athari zake imajin mitambo yote hii yajiendesha kwa mfumo wa kompyuta ikisimamiwa na watu watatu wanne...hivi.

Mitungi ya kupikia kileo aka 'gambe' aka 'bata'.

Teknolojia ya kisasa katika uchanganyaji na upikaji ikielekeza mwonekano toka kwenye mitungi.

Ubebaji wa kinywaji kilicho kamilika kutoka kiwandani hatimaye kuingia sokoni.

Utoaji chupa kwenye masanduku kwaajili ya hatua ya uoshaji.

Chupa husafishwa kwa kutumia maji yenye joto la hali ya juu lenye uwezo wa kuondosha taka za aina zote.

Utengenezwaji wa kinywaji kipya cha kiasili NZAGAMBA, kinacho tengenezwa kwa teknolojia ya kisasa.

Shughuli za kutembelea kiwanda zilipo kamilika 'MIMINAMIMINA TIME' ikawadia, ikiwa ni pamoja na wanahabari kushindanishwa katika zoezi la kutambua vinywaji kupitia ladha, rangi na mengineyo. Zawadi za nguvu zilitolewa kwa washindi.