ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, January 7, 2011

ALIYEJICHOMA MOTO KUPINGA UKOSEFU WA AJIRA AFARIKI.

Muhitimu wa chuo nchini Tunisia ambaye aliamua kujitoa mhanga kwa kujichoma moto akipinga kukosekana ajira nchi nzima katika taifa hilo la Afrika Kaskazini amefariki dunia.Mohamed Bouazizi (26) alifariki dunia juzi jioni hospitalini nje kidogo ya mji mkuu wa nchi hiyo, Tunis. Kabla ya kifo chake jamaa huyo alikuwa akiuza matunda na mboga mboga kinyume cha sheria katika mji wa sidi Bouzid baada ya kukosa ajira. Mwezi uliopita aliamua kujimwagia mafuta ya petrol na kujitia kiberiti baada ya polisi kuharibu bidhaa zake kutokana na kutokuwa na kibali maalum.
Zaidi ya watu 5000 walihudhuria Mazishi yake huku waombolezaji wakisema "KWAHERI MOHAMMED sisi tutalipiza kisasi kwa ajili yako. Sisi leo tunalia kwa ajili yako, tutawafanya wale ambao wamesababisha kifo CHAKO WALIE"
Polisi walilazimika kuzuia umati mubwa uliofika nje ya ofisi ya gavana ambako bw. Bouazizi alijilipua. “Muhammad alitoa maisha yake kwa kuonesha uchungu na hali yake na kwa ndugu zake”

Ghasia hizo zimesababisha mwandamanaji mmoja kuuawa baada ya polisi kufyatua risasi

USIKU WA MaLaViDaVi NI STONE CLUB LEO.

USIKU WA LEO - NaIzUnGuMzIa ‘IJUMAA HII’ NDANI YA STONE CLUB NI USIKU WA MaLaVIDaVI.

nGoMA NzItO-NzItO ZA MIUZIQ kUPoRoMoShWA NA MADj wAKo WAKAREe WAnAOKUwA BiZe MWANZO MWISHO KUHaKIKISHa KUWA UNaTOTa BURUDANI.
STAGE KuNaKShIWA NA MsANII WA BONGO FLEVA ALLY MOHAMED AKA Z-ANTO ANAYETAMBA NA TRACK Kisiwa Cha Malavidavi. "JuMaMosi NdO UsIsEme"
UPO HAPO?

!!!!!!!!!!!!!!-USKOSE-!!!!!!!!!!!!!!

BILIONEA AAHIDI KUITANGAZA NJE HIFADHI YA SERENGETI.

Mmoja wa matajiri wakubwa duniani, Mukesh Ambani, raia wa nchini India, amemaliza ziara yake katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kutoa ahadi ya kuitangaza hifadhi hiyo ili iweze kupata watalii wengi zaidi kutoka mataifa mbalimbali.Ambani anayedaiwa kuwa ni tajiri namba nne duniani, aliingia nchini tangu Septemba 30, mwaka jana kupitia katika Uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), akiwa na ndege nne binafsi pamoja na ujumbe wa watu 48.

Tajiri huyo juzi alimaliza ziara yake ya kitalii ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, ambapo alipata fursa ya kuzungumza na Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige na waandishi wa habari yaliyofanyika katika hoteli ya Bilila Lodge Kempinski, iliyoko ndani ya hifadhi hiyo. Ambani aliahidi kwamba ataitangaza hifadhi hiyo ili iweze kupata watalii wengi zaidi kutoka mataifa mbalimbali.

Katika mazungumzo yake, tajiri huyo mwenye kumiliki majengo makubwa ya kifari nchini India yenye huduma zote (mojawapo hili kushoto) alisema amefurahishwa na kuvutiwa na vivutio vilivyomo katika hifadhi hiyo. Aidha, tajiri huyo alisema ataisaidia Serikali ya Tanzania kutafuta wawekezaji wa kuwekeza katika hifadhi hiyo ikiwa ni pamoja na kujenga mahoteli makubwa ambayo yatavutia watalii wengi zaidi.

Alibainisha kuwa atakuwa balozi mzuri wa Tanzania katika kuitangaza hifadhi ya Serengeti ambayo ina hadhi ya urithi wa dunia, kwani inavyo vivutio vingi wakiwemo wanyama na ndege mbalimbali.

Kwa upande wake, Waziri Maige alisema alifurahishwa mno na ujio wa tajiri huyo na kwamba hiyo ni changamoto kwa Serikali ya Tanzania kwa kuimarisha miundombinu na kuongeza mahoteli katika hifadhi hiyo.




Aliongeza kuwa atashawishi nchi za mashariki ya mbali, kwa kuona uwezekano wa kuwepo usafiri wa uhakika wa ndege, ambao utaunganisha nchi hizo na hapa nchini, hususani katika Jiji la Dar es Salaam ili watalii wengi wapate fursa ya kuja hapa nchini na kutembelea hifadhi mbalimbali.

TANZANIA SPECIAL OFFERS - Buy 2 Get 1 FREE.



For Advertising Inquiries Contact:
www.hapopapo.com
India Street, Dar Es Salaam
+255 783 500730 begin_of_the_skype_highlighting +255 783 500730 end_of_the_skype_highlighting
Email: admin@hapopapo.com

Thursday, January 6, 2011

HABARI ZILIZOVUNJIKA MUDA HUU: CHADEMA YAULA UMEYA NA UNAIBU MEYA JIJI LA MWANZA. WAJIBEBA KWA MBELEKO YAO WENYEWEee!!.

Hatimaye jiji la Mwanza leo limepata Meya wake mpya baada ya kura za Madiwani wapatao 32 kupigwa nazo kuhesabiwa na mwisho wa mchezo diwani wa kata ya Nyakato bw. Josephat Manyerere wa CHADEMA kutangazwa kuwa ndiye meya mpya wa jiji la Mwanza. Akitangaza matokeo ya umeya Mwanza, msimamizi wa uchaguzi huo ambaye ni mkurugenzi wa jiji bw. Wilson Kabwe amemtaja Bw. Stanslaus Mabula (CCM) kuwa amepata kura 15, na Bw. Josephat Manyerere (CHADEMA) akiibuka mshindi kwa kupata kura 17.

Huyu ndiye meya mpya wa jiji la Mwanza kupitia CHADEMA Bw.Josephat Manyerere(kulia) akipongezwa na mbunge wa Nyamagana Mh.Wenje, na kwa chati pembeni ni diwani wa Mwaloni Kirumba Bw.Novat Manoko.

Mara baada ya mchakato wa kumpata Meya kumalizika na mshindi kutajwa, ungwe iliyofuata ikawa ni kumsaka Naibu Meya ambapo kulikuwa na wagombea wawili nayo matokeo yakataja kuwa diwani Charles Marwa Chichibela (pichani mwenye suti) kutoka CHADEMA ameibuka kidedea kwa kuzinyakua kura 17, dhidi ya 15 za Daudi Mkama wa CUF.

Mbunge wa Kigoma kaskazini Mh.Zitto Kabwe (mwenye leather coat) akifuatilia kwa umakini uchaguzi huo.

Kanuni na taratibu zote za sheria zilizingatiwa ndani ya ukumbi wa uchaguzi huo, pichani ni moja kati ya hatua za kuhesabu kura.

Moja baada ya nyingine hapa ni katika mchakato wa kuhakiki matokeo ndani ya ukumbi wa mikutano, ofisi za jiji la Mwanza Uchaguzi kumpata Meya na Naibu wake.

Hii ndiyo taswira ya sehemu ya safu ya madiwani 30 na wabunge wao wawili kufikisha idadi ya wapiga kura 32 waliohusika na mchakato huo.

KURA HAZIKUTOSHA: Kushoto ni Daudi Mkama aliyegombea nafasi ya naibu meya kupitia CUF na Stanslaus Mabula (CCM) aliyegombea nafasi ya Umeya.

Wafuatiliaji wa uchaguzi na nidhamu ya hali ya juu.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini mh.Zitto Kabwe (kushoto) na mbunge wa Nyamagana mh.Wenje wakipongezana.

Fair Play:- Hapa ni kati ya Wenje na Mabula.

Mbunge wa wilaya ya Ilemela Mh.Hainess Samson akipongezwa na Zitto.

MAHOJIANO NA Z.KABWE :-"Kwanza nawapongeza madiwani wa Mwanza kwa maamuzi haya mazuri waliyoyafanya. Pili kwa lile lililotokea jana sisi kama CHADEMA Tunalaani kwa nguvu zote ubabe na matumizi ya ovyo ya nguvu za dola. Tunalaani jeshi la polisi kuendelea kukubali kutumiwa na wanasiasa katika kuficha udhaifu wao wa kisiasa na kiuongozi. Jeshi la polisi limeendelea kuvunja sheria kwa kuzuia maandamano na mikutano ya hadhara, jeshi la polisi limegeuka kuwa watoa vibali! Watawala wajue kuwa hakuna nguvu ya risasi itakayoshinda nguvu ya umma inayotaka mabadiliko, na wala CCM haitaweza kulazimisha kubaki madarakani kwa nguvu ya risasi. CHADEMA tutaendelea na juhudi za kuhamasisha wananchi kudai haki zao za kidemokrasia ikiwemo kuwajibisha viongozi waliowachaguwa kuwaletea maendeleo"

Wednesday, January 5, 2011

HABARI ZILIZOVUNJIKA MUDA HUU KUTOKA ARUSHA...!

Kufuatia harakati za maandamano ya CHADEMA kupigwa stop na hatimaye vurugu kuzuka na kupelekea watu kadhaa kujeruhiwa vibaya. Wanachama wa Chadema wanaelekea kituo cha polisi cha Arusha viongozi wao wanakoshikiliwa. Polisi wametumia mabomu ya machozi kuwatawanya.UWANJA WA NATION MILLING, UNGALIMITED ARUSHA MAHALA PA MKUTANO.
Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema na wabunge wengine wawili wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini, ni miongoni mwa watu kadhaa waliotiwa mbaroni jana na polisi wa mkoani Arusha, kutokana na vurugu za maandamano.

Wengine waliokamatwa ni Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini na mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema. Katika vurugu hizo, pia walikamatwa mke wa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilibrod Slaa, Josephine Mushumbusi, katibu wa Chadema mkoa wa Kilimanjaro, Basil Lema na makada mbali mbali wa chama hicho, huku baadhi yao wakiwa wamejeruhiwa kwa risasi.

Vurugu zilitokana na kukamatwa wabunge hao ambao walikuwa wakiongoza maandamano ya amani,yaliyoazia katika hoteli ya Mount Meru majira ya saa saba mchana.

Viongozi wa Chadema pamoja na wafuasi wa chama hicho walikusanyika katika hoteli hiyo majira ya saa sita mchana na kuanza maandamano kulekea viwanja vya NMC ulikokuwa umepengwa kufanyika mkutano mkubwa wa hadhara ambao ulikuwa umepengwa kuhutubiwa na Dk Slaa.

Wakiwa katika eneo liitwalo Kwa Dk Mohamed barabara kuu ya Arusha-Moshi, polisi waliwazingira viongozi wa chadema waliokuwa wakiongoza maandamano na kuanza kuwapiga, kuwakamata kisha kuwatupa kwenye magari yao.

Katika purukushani hizo, Mbowe aliangukia kwenye mtaro pembezoni mwa barabara kutokana na kuzongwa na polisi, huku mke wa Dk Slaa, Josephin akishushwa kwenye gari na kupigwa sambamba na polisi hao kuvunja vioo vya gari la mbunge wa viti maalum, Grace Kiwelu.

Hadi jana jioni wabunge hao na wananchi wengine walikuwa bado wakishikiliwa na polisi na habari zaidi zinadai kwamba walikuwa wakiendelea kuhojiwa.

Kituo kikuu cha polisi cha mjini Arusha kilikuwa kimewekewa ulinzi mkali kutokana na hofu ya kuvamiwa na wananchi kwa lengo la kuwakombioa watuhumiwa waliokamatwa.

Barabara ya Makongoro ilifungwa kutokana na vurugu hizo, huku mamia ya wakazi wa Arusha wakiwa pembezoni mwa barabara wakifuatilia vurugu hizo.

Akizungumza kabla ya kukamatwa, Katibu wa Chadema mkoa wa Kilimanjaro, Basil Lema aliwaomba polisi kutambua maandamano yao ni halali kutokana na kuwa na kibali na kwamba yalikuwa ya amani.

Polisi walikuwa wakiongozwa na maafisa kadhaa wa jeshi hilo, Mkuu wa upelelezi mkoa wa Arusha, Mkuu wa usalama wa barabarani wa mkoa, Amir Konja Mkuu wa polisi wilaya ya Arusha, Zuberi Mwombeki na maafisa kadhaa toka mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara.


HABARI KWA HISANI YA Mwananchi.

WAZIRI WA VIWANDA KENYA ATEMA MZIGO.

Waziri wa Ustawishaji wa Viwanda nchini Kenya, Henry Kosgey, ambaye alikuwa amepangiwa kufikishwa maakamani na maafisa wa taasisi ya kupambana na rushwa, amejiuzulu wadhifa wake.KOSGEY.
Kosgey amechukuwa hatua hiyo siku moja baada ya Mwanasheria Mkuu wa serikali ya Kenya, Amos Wako kutoa idhini kwa tume ya kupambana na ufisadi nchini humo, kumkamata na kumfungulia mashtaka kutokana na kashfa ya kuruhusu uagizaji wa magari yaliyopita muda wa kutumika nchini humo.

Bwana Kosgey ni mwenyekiti wa chama cha ODM cha Waziri Mkuu Raila Odinga na pia ni mmoja wa Wakenya sita wanaoshutumiwa na Mahakama ya Kimataifa ya uhalifu, ICC, kupanga machafuko baada ya uchaguzi miaka mitatu iliyopita.

Chama cha ODM hata hivyo kimesema kitaendelea kumuunga mkono Kosgey.

ANKARA KAMA NJUGU.

Nakala za madai ya kulipia Ankara za wateja wa mamlaka ya maji safi na maji taka (MWAUWASA), jijini Mwanza zinauzwa na kutumiwa kama vifungashio katika maduka mbalimbali.Baadhi ya Ankara hizo zinazotumika kama vifungashio vya bidhaa za madukani zinaonesha taarifa muhimu za wateja kama jina, anwani, mtaa, namba ya nyumba, namba ya mita, matumizi ya maji na malipo mteja aliyotakiwa kulipa.

Ankara hizo ambazo ni siri kati ya mteja na MWAUWASA zimeonekana kufunga vifurushi vya bidhaa kama chumvi, sabuni, vitafunwa, misumari, na bidhaa ndogondogo. Pepa hizo za Ankara zinauzwa kwa anayehitaji ambapo furushi moja linauzwa kwa shilingi mia tatu.

Maafisa husika toka MWAUWASA wanasema kuwa kwa kawaida Ankara hizo hupelekwa posta ili ziwafikie wateja wake kupitia masanduku huduma ambayo ilisitishwa rasmi Mei 2010 baada ya wateja kubainika kuwa hawachukui Ankara hizo na wengine masanduku kunyang’anywa bila taarifa kwenda mamlaka ya maji. “inawezekana watumishi wa Posta wasio waaminifu wanazichukuwa Ankara hizo na kuziuza kwa wamiliki wa maduka, lakini tutathibitisha baada ya uchunguzi kufanyika”

Tuesday, January 4, 2011

LADY JAYDEE PURE DRINKING WATER.

LADY JAYDEE katika hafla ya utambulisho rasmi wa mzigo wake sokoni.


LADY JAYDEE PURE DRINKING WATER.
Maji yanayotengenezwa na kampuni ya MeTL,
Mohammed Enterprises Tanzania LTD


KWA MAELEZO ZAIDI na picha TEMBELEA BLOG YA ladyjaydee.

HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA YAUNDA KIKOSI KAZI KUDHIBITI WEZI WA MIUNDOMBINU YA TAA ZA BARABARANI.

Kutokana na kuwepo hujuma na wizi wa miundombinu ya taa za barabarani halmashauri ya jiji la mwanza kwa kushirikiana na Kikosi cha Polisi imechukuwa hatua ya kuunda kikosi kazi kwania ya kukamata wahalifu ili hatua za kisheria zipate kuchukuliwa dhidi yao.WILSON KABWE.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mwishoni mwa wiki, Mkurugenzi wa jiji la Mwanza bw. Wilson Kabwe amesema kuwa kufuatia wizi mkubwa uliofanyika kwa nyaya hizo umepelekea maeneo mengi ya barabara kuwa na giza nene hali iliyosababisha kuripotiwa kwa matukio mengi ya wananchi kuvamiwa na wezi, kuumizwa na hata kuporwa malizao.
Bw. Kabwe amewaomba wananchi wa jiji la Mwanza kutoa ushirikiano mkubwa katika kulinda miundo mbinu ya taa hizo sanjari na kufanikisha zoezi zima kwa kutoa taarifa kwa jeshi la polisi ili hatua za kisheria zipate kuchukuliwa dhidi ya wahalifu hao.

BARABARA YA MAKONGORO.

Hivi karibuni usiku wa tarehe 26 Disemba 2010 wezi walichimba na kuondoa nyaya kwenye eneo lote la barabara ya makongoro kuanzia daraja la mirongo hadi maeneo ya Nyakahoja jijini Mwanza hali iliyosababisha mlipukon wa ripoti kubwa ya matukio ya uhalifu.

Ikiwa ni sehemu ya utoaji wa huduma kwa wakazi wa jiji la Mwanza, Halmashauri ya jiji kwa kushirikiana na wawekezaji waliopitishwa kisheria, ilianza kutekeleza mpango wa kuweka taa hizo za barabarani mnamo mwaka 2007. Mpango uliotekelezwa kwa mafanikio makubwa na kuwawezesha wananchi wa jiji la Mwanza kunufaika na uwepo wa taa hizo hasa katika sekta ya usalama wao na mali zao hususani nyakati za usiku.

Monday, January 3, 2011

HAPPY NEW YEAR 2011.

SALAMU TOKA KWA 'BI-shosti' from Dar at Mwanza Air Port.
ASEMA SALAMU HIZI NI KWA KILA MDAU AITEMBELEAYE BLOGU HII.

Hi My friend...,May this New Year bring many opportunities your way, to explore every joy of life and may your resolutions for the days ahead stay firm, turning all your dreams into reality and all your efforts into great achievements.

My wishes for you, Great start for Jan, Love for Feb, Peace for march. No worries for April Fun for May, Joy for June to Nov, Happiness for Dec, Have a lucky and wonderful new year 2011.

Says Doreen.

Sunday, January 2, 2011

TIGO KANDA YA ZIWA YAUKARIBISHA MWAKA KWA KUMWAGA ZAWADI KWA WAFANYAKAZI WAKE.

Katika kutia changamoto kwa wafanyakazi wake kampuni ya mawasiliano ya mtandao wa simu za mkononi Tigo imefanya sherehe ya kuukaribisha mwaka mpya 2011 tarehe 1january2011 katika viwanja vya BOT pansiasi jijini Mwanza.

Washiriki wa hafla hiyo iliyofana walikuwa ni wafanyakazi wa kampuni hiyo toka mikoa yote ya kanda ya ziwa ambapo humo ndani zawadi kwa wachapakazi bora na wanamichezo bora zilitolewa.

Kombaini ya mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Mara upande wa netibali ilipata ushindi na kukabidhiwa kombe baada kuinyanyasa timu ya kombaini ya mikoa ya Tabora, Kigoma na Bukoba.

Kombaini ya Mwanza, Shinyanga na Mara (red) ikipata bao.

Mchezo wa soka ulichezwa baina ya Timu ya Tigo Kombaini ya mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Mara (red) iliyobanjuliwa kwa kisago cha aibu 4-2 toka kwa kombaini ya Tigo mikoa ya Tabora, Kigoma na Bukoba(blue).

Washindi wa Tigo soka mikoa ya Tabora, Kigoma na Bukoba na kombe lao.

Bendi ya muziki wa dansi inayotikisa kanda ya ziwa Okestra Kamanyola walikamatisha na kupagawisha wafanyakazi nowma.

Kila mmoja alitoka na Tabasamu kwa mazawadi yaliyomwagwa ndani ya hafla. Meneja Matangazo na Promosheni, Redemtus Masanja (kushoto) akikabidhi zawadi.

Wafanyakazi wa Tigo mikoa ya Kigoma, Bukoba na Tabora kiukweli katika suala la style za ushangiliaji walifunika, hapa ni shangwe kwa moja ya wadau wao aliyejinyakulia Mountain bike.

VutaaaaaaaaaH!! Mwisho wa siku kombaini ya mchezo wa kamba mikoa ya Tabora, Kagera na Kigoma ikawazidi nguvu na kuwabwaga Mwanza Shinyanga na Mara pichani walioanguka.

Utaratibu wa zawadi ulikuwa ni ngazi kwa ngazi nao ulitwaliwa kama changamoto kwa wenye bidii kuongeza juhudi na maarifa kazini na kwa wengine kutobweteka. Pikipiki hiyoo wazeya ikiondoka.

'Sipati picha jinsi geto patakavyotisha' Ni mwanadafada kutoka Bukoba akivuna alichopanda kwa kunyakua saundi, na hapa akikabidhiwa toka kwa meneja mawasiliano kanda ya ziwa Joseph Mtalemwa.

Wau mzobemzobe!! style ya kulikwea jukwaa kunyakua zawadi.

Television hiyooooo kwa dada wa tigo Shy-town.

Usafiri kwa shughuli binasfi na ufanisi wa kazi hata sehemu zenye vilima mbele ya 'mountain bike' aaaaaH! halivuji jasho.


Michezo ni burudani michezo ni afya, Washindi wa michezo ya jumla TBR,KG na BK na shangwe zao.

Makamuzi ya ONE N' TWO na Dj Chriss toka Villa park.

KATIKA mahojiano yake na vyombo vya habari Meneja Matangazo na Promosheni, Redemtus Masanja alisema "Tukio kama hili tunalifanya kila baada ya miezi sita nia na madhumuni ikiwa ni kuhamasisha na kuchochea utoaji wa huduma bora tena zilizo makini kwa wateja wetu haiishii hapo bali hata kuona yale malengo yetu yanafikiwa kwa kasi aina gani. Sasa kwa wale wanaofanikisha na hatimaye tukaona juhudi zao hatuna budi kuwaonyesha kwamba wanachokifanya tumekiona hivyo tunawatunuku zawadi na kuwawezesha ili kusukuma mbele gurudumu letu la maendeleo. Na kwa wale watakaokosa zawadi, nafasi ipo waongeze juhudi kamwe hatuto wabania."
Wadau wa habari kutoka Star TV Mwanza James George (kushoto) na Ben Star wakifukunyua zana za maangamizi.