ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, November 9, 2011

KAMPENI YA CHANJO KITAIFA 12-15 NOV 2011

SERIKALI ya Tanzania kupitia Wizara yake ya Afya na Ustawi wa Jamii inao mkakati kabambe wa kutokomeza ugonjwa wa SURUA na POLIO kwa watoto wenye umri chini ya miaka 5.

Wizara itaendesha kampeni ya kuwapatia chanjo watoto wote wenye umri kuanzia miezi 0-59 nchi nzima. Pia katika zoezi hili itatolewa Matone ya VITAMINI A na DAWA ZA MINYOO

Rais Jakaya Kikwete, anatarajiwa kuzindua kampeni hiyo ya kitaifa ambayo uzinduzi wake utafanyika mkoani Arusha Novemba 12, mwaka huu na JK ambaye ni balozi wa chanjo kimataifa, atashiriki kutoa chanjo.


<-Ngozi ya mtoto anayeelekea kupona surua.

Kaimu Mkurugenzi wa jiji la Mwanza Tito Jeremiah Mahinya, ametoa rai kwa vyombo mbalimbali vya habari nchini kusaidia kufikisha ujumbe kwa jamii kwa kutoa matangazo, kuendesha vipindi vyenye kuelimisha na kuhamasisha jamii ili walengwa ambao ni ni watoto wadogo wapate haki yao ya msingi katika kulinda afya zao.

Zoezi hilo litakuwa kwa watoto wenye miezi 0 hadi miaka 4 na miezi 11, litafanyika katika vituo 124 katika kata zote za halmashauri ya jiji la Mwanza, kuanzia tarehe 12-15 November, 2011, Wazazi wawapeleke watoto wao kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa kumi na moja kamili jioni kwenye vituo vya chanjo.

CHANJO NI HAKI YA MSINGI YA MTOTO.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.