ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, September 3, 2011

MH. MABULA ASHUSHA TENA NEEMA KUVIWEZESHA VILABU VYA SOKA MWANZA

Diwani wa kata ya mkolani Stanslaus Mabula leo amekabidhi msaada wa vifaa vya michezo vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mbili kwa timu mbili tofauti za soka jijini Mwanza.Msaada wa kwanza ni Jezi seti moja na soksi pea 16 vyote vikiwa na thamani ya shilingi laki sita na nusu vilikabidhishwa kwa mkurugenzi wa jiji la Mwanza Wilson Kabwe (kushoto) ambaye pia ni mlezi wa timu ya Halmashauri ya jiji la Mwanza Fc MCC.

Akikabidhi msaada huo Mabula amesema kwamba yeye akiwa kama mdau wa michezo ametekeleza ahadi yake ya kuchangia timu hiyo baada ya kuombwa na uongozi wa timu hiyo kama sehemu ya chachu ya timu hiyo inayoshiriki ligi ya wilaya ya Ilemela na michuano ya kombe la ng’ombe inayoendelea kwenye uwanja wa michezo wa Jeshi Nyegezi ambapo timu hiyo imetinga hatua ya robo fainali.

Ameongeza kuwa akiwa kiongozi wa wananchi wa kata ya Mkolani na mdau mkubwa wa michezo ataendelea kutoa misaada mbalimbali ambayo italenga kukuza vipaji na kuendeleza michezo na amewaomba viongozi wengine wakiwemo na viongozi wenzake kuendelea kuzisaidia timu mbalimbali badala ya kuliachia jiji pekee ambalo huchukuwa muda mrefu kupitisha fedha za kuzisaidia timu na vifaa hali inayosababisha timu zetu kutofanya vizuri kwenye mashindano mbalimbali zinazoshiriki
.Naye mkurugenzi wa jiji la Mwanza Wilson kabwe amempongeza diwani huyo kwa kuguswa na kuhamasika kutoa msaada huo jambo ambalo limeonyesha kuwa ni kiongozi wa vitendo na anayependa maendeleo kwa wakazi wa jiji na katani kwake kwani si msaada wa kwanza toka kwa diwani huyo.

“Uongozi ni kuonyesha mfano na kuhakikisha unasimamia maendeleo kwa jamii ili kuleta manufaa ambayo yatasaidia vijana kukuza vipaji, kupata ajira na kuendeleza sekta ya michezo kwa kuzingatia ilani zilizo wekwa kuendeleza michezo nchini, jinsi zinavyotekelezwa kwa vitendo basi zinakuza kwa watu walio wachagua” Alisema Mkurugenzi kabwe wakati akitoa shukurani.


Pia diwani huyo amekabidhi jezi seti moja, mipira miwili vyenye thamani ya shilingi laki nne na kiasi cha shilingi laki tatu taslimu kwa timu ya Fc Shadia ya mtaa wa Shadia kata ya mkolani ikiwa ni kutekeleza ahadi wakati alipoalikwa kuwa mgeni rasmi wa hafla ya kumpongeza kuanzisha mashindano ya Kamanda Cup aliyoyaanzisha mwaka jana kabla ya kuwa diwani.

Wakati akikabidhi vifaa hivyo na fedha Diwani Mabula amesema kwamba mwaka huu mashindano hayo ya Kamanda Cup atayabadilisha jina na kuitwa Mkolani Cup na yatashirikisha timu kutoka mitaa yote ya kata hiyo, huku akiwa ameyaboresha zaidi kwa kutoa vifaa vya michezo vyenye ubora na kuongeza fungu kubwa kwa upande wa zawadi hivyo amezitaka timu kuanza maandalizi mapema ikiwemo Fc Shadia ambayo tayari imepata changamoto ya vifaa vitakavyoisaidia timu hiyo kwenye maandalizi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.