ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, September 3, 2011

FIKIRIA NA WENGINE WALIO NA UHITAJI

Watu hukaa katika majumba ya kifahari meza zikisheheni kila aina ya tunda nayo kwa mafungu makubwa makubwa.

Wakichinja kila aina ya vitoweo, wapishi katika masufuria makubwa walipika vyakula kwaajili ya sherehe yenye nia moja tu nalo ni kupongezana.

Vyakula vya nafaka kwa shehena vikapikwa.

Nao hula na kunywa hata kusaza.

Mara baada ya sherehe chakula kingi kilichosalia humwagwa hata kisibakie kwani marufuku kula kiporo.

Kikimwagwa majalalani kama taka.

Chakula choote hutupwa.

Hayo yakifanyika hebu fikiria juu ya ndugu zetu wengine, wakiishi kama ndege kuokoteza.

Upande wa pili wa dunia unadhoofika kwa kukosa lishe.

Hali si hali kwa kukosa hata kipande cha chakula.

Mtizame mama yule anayenyonyesha.
DON'T WASTE FOODS ANY MORE, Kusanya peleka kwa wenye uhitaji.

Let this be remembered.. . each time we throw away Foods!
People who live in rich countries,, don't know this,, don't want to know
this,, never understand this!

but U,, please U,, understand this .........

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.