ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, August 12, 2011

WIMBI LA MAJONZI LATANDA MAZISHI YA MWANDISHI WA HABARI RICHARD MASATU

Mke wa marehemu Richard Masatu ndani ya fikra nzito juu ya safari ya mwisho ya mumewe mara baada ya shughuli za mazishi kukamilika eneo la makaburi ya Mwisenge Msoma mjini.

Mwili wa marehemu Richard Masatu SINCE 1972-2011.

Mwenyekiti wa kamati ya maafa toka Chama cha waandishi wa habari mkoa wa Mwanza Bw. Fredrick Katulanda akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu.

Mwakilishi wa ITV mkoani Mara George Marato akitoa heshima zake za mwisho huku akiwa ameambatana na Peter Fabian toka MPC.

Mfanyabiashara maarufu jijini Mwanza Jack Fish akitoa heshima zake kwa mwili wa marehemu Richard Masatu.

Afisa utumishi wa Sahara Group Bwana Rafael Shilatu akitoa salamu za rambirambi kwa wafiwa.

Bibi wa marehemu akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa marehemu mjukuu wake.

Ripota wa RFA na Star Tv mkoani Mara ambaye pia ni katibu wa siasa na uenezi (CCM) Mkoa wa Mara Bw. Maximilan Ngesi akitoa shukurani na wasifu wa marehemu Richard Masatu.

Mwenyekiti wa Chama Cha Wananzengo Mwanza Bwana Makongoro akitoa neno la shukurani na salamu za rambirambi toka watu wa chama chake waishio Mwanza.

Safari kuelekea nyumba ya milele.

Mapaparazi wote kanda ya ziwa walimiminika eneo hili.

Marehemu akiingia nyumba yake ya milele.

Marafiki wa dhati wa marehemu Richard Masatu toka Chama Cha Nzengo Mwanza.

Ni marafiki wawakilishi toka chama cha MPC kushoto Ntemi Nyanda, James George na Mheshimiwa diwani mtarajiwa.

SehEmu ya Ummati uliojitokeza katika mazishi ya Richard Masatu aliye zaliwa tarehe 8/Dec/1972 na kufariki dunia tarehe 10/Aug/2011.

BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LAKE LIHIMIDIWE.

Tupe maoni yako

1 comments:

  1. Hakika kwake sisi marejeo ni lazima.
    masatu katangulia, sisi jukumu letu kujiombea kwani hatujui siku wala saa.
    hatujui sisi tuliohai tutaondokaje!!
    kweli huu ni mtihani mkubwa....
    pilly.

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.