ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, August 22, 2011

AIRTEL YAMWAGA MSAADA WA VITABU SUA SEKONDARI

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imekabidhi msaada wa vitabu vya kiada na ziada kwa shule za sekondari nne za mkoani Morogoro, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kusaidia jamii hapa nchini. Meneja Mauzo Kanda ya Pwani wa kampuni ya simu ya Airtel, Aluta Kweka (kushoto), akikabidhi sehemu ya msaada wa vitabu kwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Alfred Shayo vilivyotolewa na kampuni hiyo kwa Shule za Sekondari za SUA, Mwembesengo, Mji Mpya na Mgulasi Mkoani Morogoro mwishoni mwa wiki. Wa pili kushoto ni Mkuu wa Sekondari ya SUA, Khalfan Millongo, Meneja Huduma za Jamii wa Airtel Tunu Kavishe na Diwani wa Kata ya Mbuyuni, Samuel Msuya. Vitabu hivyo vina thamani ya shs milioni 4

Meneja Huduma za Jamii wa Airtel Tanzania, Tunu Kavishe (wa tatu kushoto) akikabidhi sehemu ya msaada wa vitabu kwa mmoja wa wanafunzi wa Shule ya Sekondari SUA, Rogers Shempemba vilivyotolewa na kampuni hiyo kwa Shule za Sekondari za SUA, Mwembesengo, Mji Mpya na Mgulasi Mkoani Morogoro mwishoni mwa wiki.

Meneja Mauzo Kanda ya Pwani wa kampuni ya simu ya Airtel, Aluta Kweka (kushoto), akikabidhi sehemu ya msaada wa vitabu kwa mmoja wa wanafunzi wa Shule ya Sekondari SUA, Happiness Makundi vilivyotolewa na kampuni hiyo kwa Shule za Sekondari za SUA, Wa pili kushoto ni Meneja Huduma za Jamii wa Airtel, Tunu Kavishe na kulia ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Alfred Shayo. Vitabu hivyo vina thamani ya shs milioni 4.

Meneja Huduma za Jamii wa Airtel Tanzania, Tunu Kavishe (wa tatukushoto) akikabidhi sehemu ya msaada wa vitabu kwa mmoja wa wanafunzi wa Shule ya Sekondari SUA.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Alfred Shayo (kulia) akimshukuru Meneja Huduma za Jamii wa Airtel Tanzania, Tunu Kavishe (kushoto) katika hafla ambayo Airtel ilikabidhi msaada wa vitabu vyenye thamani ya shs milioni 4 kwa Shule za Sekondari za SUA, Mwembesengo, Mji Mpya na Mgulasi Mkoani Morogoro mwishoni mwa wiki. Katikati ni Mkuu wa Shule ya Sekondari SUA, Khalfan Millongo.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Alfred Shayo, akihutubia katika hafla hiyo.

Shule zilizopata msaada wa vitabu ni shule za sekondari ya Mwembesongo, Mji mpya, SUA na Mgulasi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.