ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, June 2, 2011

PICHA ZA MAJERUHI WA RISASI NA MABOMU SAKATA LA UTEKAJI WA KITUO CHA POLISI MUGUMU MKOANI MARA.

Majeruhi Wambura Itembe Kisera.
Majeruhi wa sakata la kuvamia kituo cha polisi MUGUMU lililotokea wiki hii wako taabani ifuatayo ndiyo hali halisi na hatua zilizo chukuliwa dhidi ya majeruhi hao wenye kesi ya kujibu.

Majeruhi Wambura Itembe Kisera akiwa hospitali akisubiri kupelekwa hospitali ya rufaa ya Bugando Mwanza, baada ya kubainika kuwa risasi alipigwa risasi kwenye nyonga na kuvunja mifupa, wakati wa vurugu za uvamizi wa kituo cha polisi, hata hivyo alisomewa mashitaka akiwa hospitalini hapo.

Pichani majeruhi Mkira Maswi mkazi wa Itununu katika hali tofauti aliyelazwa kitanda no.6 hospitali teule ya Nyerere ddh wilayani Serengeti kutokana na majeraha ya kupigwa mabomu ya moto na askari polisi katika tukio la kuvamia kituo cha polisi Mugumu ili watoe watuhumiwa wawili wa mauaji wawaue.

(picha zote na Anthony Mayunga)

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.