ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, June 19, 2011

CHEREKO CHEREKO ZAFANA HARUSI YA MARWA & DEBORA

Ni jumamosi ya tarehe 18juni2011 ndiyo ambayo imeweka historia kwa wawili hawa ni Bw. Marwa Slyvanus Zembwela na Bi. Debora Kerenge mara baada ya kufunga ndoa takatifu katika Kanisa Takatifu Musoma mjini.

Maharusi wakitoka kanisani mara baada ya kufunga pingu za maisha.

Mwendo poz-poz kuingia ukumbini.

Si mavazi pekee na mapambo ya ukumbi ndiyo kigezo kilichofanikisha kupendeza kwa harusi hii bali hata jinsi wahusika walivyoweza kujityuni'.

Si wawili tena bali ni mwili mmoja Mr&Mrs Marwa Zembwela.

Mc mashuhuri MaiMatha wa Jesse ambaye walishirikiana vizuri na Mc Abbu wa Musoma (hayupo pichani) kufanikisha mnuso huo akitoa maelezo kwa maharusi kuelekea utambulisho.

Maharusi wakikata ndafu.....

Bibi harusi kwa bwana harusi.

Bwana harusi kwa bibi harusi.

'Ni wakati wa Shampeini mabibi na mabwana maharusi wetu wataelekea eneo la daraja ukumbini hapa kisha nderemo ziendelee....'

Wageni wakubwa maarufu nao walipata fursa kuhudhuria sherehe hii pichani mkuu wa Mkoa wa Mara Kanali Mstaafu, Enos Mfuru (mwenye kipaza sauti) akiwa na mkewe (wa kwanza kushoto) sanjari na wazazi wa Bwana harusi Bwana na Bibi Zembwela.

Mwanasiasa maarufu Mh. Vedasto Mathayo akiwa na wake zake hapa alikuwa akitia zawadi kwa maharusi.

Wadau mwaliona pigo hilo...?

Shine-shine..

Mc Mai na Oly.

Ng'aring'ari za Dada wa Bwana harusi wakati wa pongezi.

Hii ndiyo kamati ya maandalizi sherehe ya kufana ya harusi ya Bwana Marwa Zembwela na Debora Kerenge, Mungu awabariki.

Tupe maoni yako

2 comments:

  1. hongereni Debby and my shem Marwa....it was a unique wedding of a kind,@kaka sengo nimekukubali picha zimetoka bomba....mdau mama K mwanza

    ReplyDelete
  2. Mr.and Mrs Martin Bonphance Chacha....

    familia ya martin chacha inatoa pongez kwa maharusi marwa sylvanus zembwela na bi.deborah kerenge na MUNGU Awabarik sku zote za maisha yao aishi mpka uzee wao wawaone watoto wa watoto wao...........

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.