ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, May 16, 2011

M-BLOGISHAJI MAARUFU AMBAYE PIA NI MSANII MKUBWA NCHINI JAPANI AJINYONGA.

Msanii mmoja mwenye jina kubwa nchini Japani, Miyui Uehara, mwenye miaka 24, amefariki dunia juzi alhamisi asubuhi baada ya yeye mwenyewe kujinyonga katika nyumba anayoishi katika eneo la Meguro jijini Tokyo.

Polisi amesema kuwa jirani yake aliuona mwili wake mlangoni kwake akiwa amejifunga skafu na kamba shingoni wkati wa saa nane usiku na ndipo tu aliita watu wa huduma za dharura. Uehara alikimbizwa hospitali ambako madakari walidhitisha kuwa alikwishakufa.

Kwa mujibu wa mtandao wa kihabari wa japantoday , Uehara ni mmoja wa watoto 10 waliozaliwa nyumba moja anayetokea mkoa wa Kagoshima, jambo ambalo si la kawaida sana nchini Japani (Watoto wengi katika familia moja) na kipaji chake kilijibainisha wakati akifanya kazi ya uhudumu katika klabu moja ya starehe, wakati huo alikuwa na miaka 18.


Moja ya picha katika mtandao wake www.oodunia.blogspot.com

Hapo alianza kuonekana kwenye majarida ya wanaume akiyapamba kwa picha zake zilizowafanya wanaume wengi hususan vijana kuyanunua kwa wingi na baadaye alifahamika kama “Malkia” miongoni mwa mashabiki wake.

Uehara anamiliki blogi yenye habari kemkem (www.oodunia.blogspot.com) ambamo aliweka picha zake 'Bila kificho', itembelee ujionee mwenyewe, na uchunguzi wa kipolisi unaonyesha kuwa aliutembelea mtandao huo mara ya mwisho saa 2 asubuhi siku ya jumanne ambapo alielezea huzuni kubwa aliyonayo kwa kutoweza kulipata penzi la Kweli.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.